PreGE2025 RC Mara ateta na viongozi wa dini akifuturisha

PreGE2025 RC Mara ateta na viongozi wa dini akifuturisha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi amewataka Viongozi wa Dini kusaidia Serikali katika mapambano ya dhidi ya Vitendo vya Ukatili na Mmomonyoko wa maadili,Ulinzi na amani kuelekea Uchaguzi Mkuu.

1743148714623.png

Mtambi ametoa kauli hiyo Wakati alipowaalika Viongozi wa Dini katika Futari Ikulu ndogo ya Mkoa wa Mara ambapo amewataka kuwa sehemu ya kukemea watu ama kundi linalojaribu kupotesha dhidi ya utulivu uliopo nchini.

"Niwaombe Sana viongozi wa Dini tusaidieni katika hili kwenye maeneo yenu hasa ya ibaada tuanahitaji kila moja kuwa mlinzi wa imani yetu na kuhakikisha hadi hapa alipotufikisha Dkt. Samia Suluhu Hassan tunapalinda."

1743148749597.png
Mtambi amewakumbusha viongozi wa Dini kukumbuka kukemea Mmomonyoko wa maadili kwenye jamii inayowazunguka kufuatia kuwepo kwa viashiria vinavyoonesha maadili kuharibika miongoni mwa vijana.

Katika hatua nyingine RC Mtambi amesema Serikali itashirikiana na viongozi hawa katika kuunganisha nguvu katika mapambano dhidi ya Vitendo viovu.

1743148776103.png
 
Back
Top Bottom