Hawa ni akina mama na watoto wao wamefika leo kwenye ofisi za Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam wakidai kutelekezwa na wazazi wenzao.
Wakati Lyatonga Mrema akiwa waziri wa Mambo ya ndani alianzisha deski la akina mama kueleza matatizo waliyonayo kwenye ndoa zao.
Nakumbuka Mrema alikuwa akiwapa siku 7 wanaume waliotelekeza familia zao kuripoti ofisini kwake.
Walipofika ofisini kwa Mrema wanaume wengi walikuwa wakiomba kesi zipelekwe mahakamani. Kesi nyingi ziliamuliwa zikasikilizwe nje ya mahakama kwa sababu pesa ya matunzo ambayo ingeamuliwa na mahakama isingekidhi mahitaji ya wakati huo.
Mahakama ilikuwa bado inaitambua sheria ya ndoa ya mwaka 71 kuhusu matunzo ya mtoto kuwa ni shilingi mia (100) kwa mwezi.
Hadi leo sheria hiyo haijabadilishwa.
Sina uhakika Makonda amejiandaa kiasi gani, lakini ningeshauri kama kweli ameamua kuwasaidia ajenge ushawishi kwa bunge kubadili sheria ya ndoa kuendana na mazingira ya sasa. Vinginevyo anaenda kuongeza matatizo juu ya matatizo.
Wakati Lyatonga Mrema akiwa waziri wa Mambo ya ndani alianzisha deski la akina mama kueleza matatizo waliyonayo kwenye ndoa zao.
Nakumbuka Mrema alikuwa akiwapa siku 7 wanaume waliotelekeza familia zao kuripoti ofisini kwake.
Walipofika ofisini kwa Mrema wanaume wengi walikuwa wakiomba kesi zipelekwe mahakamani. Kesi nyingi ziliamuliwa zikasikilizwe nje ya mahakama kwa sababu pesa ya matunzo ambayo ingeamuliwa na mahakama isingekidhi mahitaji ya wakati huo.
Mahakama ilikuwa bado inaitambua sheria ya ndoa ya mwaka 71 kuhusu matunzo ya mtoto kuwa ni shilingi mia (100) kwa mwezi.
Hadi leo sheria hiyo haijabadilishwa.
Sina uhakika Makonda amejiandaa kiasi gani, lakini ningeshauri kama kweli ameamua kuwasaidia ajenge ushawishi kwa bunge kubadili sheria ya ndoa kuendana na mazingira ya sasa. Vinginevyo anaenda kuongeza matatizo juu ya matatizo.