Njaa zinakuvuruga, na mwisho wa Maisha ya mwajiri wako ni april pale mjengonikama kuna video footage basi Bashite yupo in trouble!
=====
Msomaji, vema pia ukasoma hapa > Mwanamama kupitia Uhuru FM, adai kuzalishwa na Askofu Gwajima na kutelekezwa!
=====
Makonda hua anafika office za clouds mara kwa mara. Siku zingine anashinda hapo mpaka jioni. Siku ya Alhamis Makonda alifika office za Clouds Cha ajabu siku hiyo alikaa mpaka usiku akawa anamtafuta soudy Brown na Qwisser wa SHILAWADU muda huo walikuwa bado hawajafika kazini basi akawa anazungukazunguka tu ofisi hii anatokea ile kama mfanyakazi wa Clouds.
Kwenye Mida ya Saa kumi hivi akakutana na kina Soudy pamoja na prodyuza wa kipindi wakawa wanaongea kwa uficho hivi na usiri tukajua tu ni mambo ya kawaida ya kuhitaji uprivate lakini siku ile ulikuwa unatia mashaka sana.
Kumbe Makonda alikuja na Story ya mwanamke mmoja ambaye yeye Makonda alisema huyo mwanamke amezaa na mchungaji Gwajima na ametelekeza akawa anataka arekodiwe na ubuyu uruke kwenye kipindi cha SHILAWADU.
Basi wakakubalia kwa kuwa ni habari itabidi huyo mwanamke arekodiwe na kipindi kiruke siku ya jana lakini kawaida ya Kipindi cha SHILAWADU ubuyu ukipatikana lazima kila mtu apewe Natural Justice ya kusikilizwa pande zote mbili sababu huwa ndiyo kawaida ya kipindi.
Makonda siku hiyo hiyo ya Alhamisi akamwambia Soudy ajiandae then huyo mwanamke mnayemuona kwenye video na mtoto aliletwa na wasaidizi wa Makonda ahojiwe na Soudy Brown tayari kwa kurushwa kwa kipindi.
Siku ya Ijumaa ambayo ilikuwa ni jana SHILAWADU wakamtafuta Gwajima kwa upande wake kama anaifahamu hiyo ishu na je mwanamke huyo aliyetajwa ni kweli kwasababu tunaelewa ugomvi uliopo kati ya Makonda na Gwajima isijekuwa SHILAWADU wanatumika kuwafitinisha watu vibaya!
kwa bahati mbaya Gwajima hakupatikana jana ijumaa kwa ajili ya kurekodiwa na kufanyiwa mahojiano.
SHILAWADU wakatumia busara mpaka apatikane Gwajima scene ya Dada mwenye mtoto ziende kwa pamoja na ya mchungaji Gwajima kama kawaida ya POVU inavyokuwaga.
Jana usiku sasa kumbe Makonda alikuwa anafuatilia kipindi cha SHILAWADU aone kama kile kipande kitaruka hewani wapi ndiyo akaamua kuja Clouds na magari mawili yeye mwenyewe Makonda na Watu kama nane hivi wakiwa na Bunduki aina ya SMG geti la kawaida mlinzi alifungua geti kwasababu amezoeleka Mh anakujaga mjengoni wakafunguliwa kisha wakaingia ndani.
Walipofika reception wakazuiwa kuingia ndani sababu hatuna utaratibu wa kuruhusu wageni baada ya saa Nne usiku kuingia ndani ya Ofisi kama siyo mfanyakazi wa CLOUDS.
Alipoona wanazuiwa wakatoa bunduki zao mlinzi akashurutishwa afungue mlango kwa nguvu sababu walimtishia na Silaha mlimzi akafungua mlango wakaenda naye hadi studio kipindi kilikuwa kinaendelea hewani.
Makonda akawatoa nje Soudy na Mwenzake Qwisser akawauliza kwanini video aliyowaletea haijachezwa wakaelezea utaratibu jinsi utaratibu ulivyokuwa Qwisser wakati anajielezea akapigwa mtama akaanguka chini wakavamia mitambo ya transmission kwenye traycaster wakitaka kile kipande kirushwe hewani prodyuza wa kipindi akamuambia Makonda kwanini anavunja utaratibu na kutumia nguvu na ameshapewa utaratibu akapigwa na kitako cha Bunduki mgongoni akaanguka chini bahati mbaya kipindi kilikuwa kimefika mwisho.
Wakamshurutisha Prodyuza wa SHILAWADU anaitwa Chriss awape kile kipande wakaondoka naye wakati wanaondoka Ruge alikuja na Polisi akaingia lakini tayari walikuwa wameondoka ofisini wamechukua hicho kipande cha Video ya huyo mwanamke.
Hizo video zilichukuliwa kwa nguvu na Makonda na hao watu waliokuwa na Silaha inasemekana Makonda ana timu yake wanazisambaza kwa kasi na hatujui lengo lake ni nini.
Hata mkihitaji footage za Camera zipo jinsi tukio lilivyokuwa usiku wa jana.
====
Kutoka kwa wadau wa Clouds Media
Habari kama hizi za kichochezi na za uzushi ndizo zinazotuponza wanaJf mbona tuliokuepo mjengoni mda huo hatujasikia lolote na hakuna chochote kilichotokea.
Au umetumwa?
Clouds ni taasisi kubwa inayoongozwa kwa misingi na taratibu zake haiwezekani mtu from no where aje tu aingie mpaka peoduction bila kufata utaratibu!
Acha uzushi watanzania puuzeni hizi taarifa si za kweli!!.
He is on Death row..Makonda must go
Sawa le mutuzsasa ni ukweli usio shaka kuwa kuna vita kubwa sana dhidi ya paol Makonda na imefikia hadi watu wanatangeneza kudai video eti kuuaminisha umma kuwa ni makonda kwenye iyo video. Jamani achani propaganda uchwara na kwa taarifa yenu hizo propaganda zenu uchwara ndo zinasababisha magufuli awaone hamna la maana zaidi ya vita binafsi dhidi ya makonda.
Mliotengeneza video hiyo mlichokosea ni kuwa Mkuu wa mkoa halindwi na askari wanaovaa mabaka mabaka(kwa tanzania ni JWTZ), pili ni kuwa Jeshi Polisi Tanzania halina nguo za mabaka mabaka kama kenya na tatu ni kuwa Jwtz hawajihusishi na shughuli za usalama zilizoko chini ya polisi. Alafu how comes JW waende clouds wameshika bunduki alafu polisi asishike bunduki????? kweli kitengo cha propaganda dhidi ya makonda na mange wenu. Period.
Wametoa Clouds na si mtu mmoja, unadhani kuna mtu ndani ya Clouds atakuwa amefurahishwa na alichofanya Makonda?Hivi hiyo clip imetolewa na Clouds au staff mmoja ameivujisha? ndo nawasha kimeo changu hapa msishangae swali langu
Mkuu mambo kama hya yamezoeleka kwenye Nchi zenye machafuko ambapo kiongozi anaweza kuvamia Kituo cha redio akiwa na askari wenye bunduki sasa leo tunayaona kwetu hii ni hatari Magu na huyu Bashite sijui wana mahusiano ganiBashite gaidi wa jiji this round amekwenda na maji
Habari kama hizi za kichochezi na za uzushi ndizo zinazotuponza wanaJf mbona tuliokuepo mjengoni mda huo hatujasikia lolote na hakuna chochote kilichotokea.
Au umetumwa?
Clouds ni taasisi kubwa inayoongozwa kwa misingi na taratibu zake haiwezekani mtu from no where aje tu aingie mpaka peoduction bila kufata utaratibu!
Acha uzushi watanzania puuzeni hizi taarifa si za kweli!!.
Maskini mzee mkavu,wakaelezea utaratibu jinsi utaratibu ulivyokuwa Qwisser wakati anajielezea akapigwa mtama akaanguka chini
Saa 4 usiku akiwa na majambazi wenzake.
Kweli kabisa,jamaa udalali umewafikisha hapa.Clouds wanastahili walicho fanyiwa
Kwa Mara ya Kwanza nimeanza kuamini kuwa JF ni Mtandao Makini Kabisa, Mimi ni Mfanyakazi wa Clouds Media Group, Nipo Marketing department. Mwanzo Tulikua tumezuiwa kueleza Ukweli wa Hili Jambo, lakini Kutoka na Maadili ya Uandishi imebidi wakuu wa Idara waruhusu lizungumzwe, Leo Asubuhi Karibu wafanyakazi wote wamezungumza kuhusu ukweli huu. Ninasikitika sana kuona watanzania wajinga kama wewe Kubisha kitu ambacho hukijui halafu unadanganya Umma kuwa Ulikuwepo Mjengoni, huu ni Unafiki wa Kijinga. Jamaa yako kafanya Tukio kweli, na Mbaya zaidi aliyekua anambeba na kuendekeza huu Ujinga wake ni boss Ruge, lakini kwa mara ya kwanza Baada ya Kikao cha Jana Kizito Kapigwa marufuku, wafanyakazi wote tumefurahi maana tulikua tumemchoka na Tabia zake hapa Ofisini utafikiri yeye ndo Boss wetu. Kiufupi aliyezuia ile Video ya Mama mwenye mtoto ni Sisi wote kama Idara, tulimuomba ufanyike Uchunguzi kwanza ili kubalance Stori kabla haijaruka. Sasa Kaka, hayo ni Machache tu, Makonda ajitokeze Akanushe halafu sisi tutaweka Ushahidi wote.Habari kama hizi za kichochezi na za uzushi ndizo zinazotuponza wanaJf mbona tuliokuepo mjengoni mda huo hatujasikia lolote na hakuna chochote kilichotokea.
Au umetumwa?
Clouds ni taasisi kubwa inayoongozwa kwa misingi na taratibu zake haiwezekani mtu from no where aje tu aingie mpaka peoduction bila kufata utaratibu!
Acha uzushi watanzania puuzeni hizi taarifa si za kweli!!.