RC Gambo aichana Halmashauri ya Jiji la Arusha haina uwezo

RC Gambo aichana Halmashauri ya Jiji la Arusha haina uwezo

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2016
Posts
757
Reaction score
1,822
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ameeleza kwamba Jiji la Arusha halina uwezo wa kifedha wa kutekeleza miradi yoyote ya maendeleo kwani miradi yote inayojengwa kwa sasa katika jiji la Arusha inatekelezwa na serikali kuu.

Gambo ametoa kauli hiyo wakati akifungua mkutano wa wadau wa benki ya CRDB unaofanyika katika hotel ya Kitalii ya Mount Meru jijini hapa na kuwataka wananchi waachane na upotoshwaji unaoenezwa na baadhi ya viongozi kuwa miradi hiyo inajengwa na jiji la Arusha.

Amesema kuwa jiji la Arusha linakusanya mapato ya sh,Billion 20.6 lakini gharama za mishahara ya wafanyakazi wake ni sh, bilioni 37 sasa utaona jinsi gani ambavyo halmashauri hiyo haiwezi kuendesha mradi wowote.

Gambo amesema kuwa miradi mikubwa ya kimkakati katika jiji la Arusha ukiwemo mradi wa maji wa bilioni 524,na ujenzi wa vituo vya afya inatekelezwa na serikali ya Rais Magufuli huku akiwataka wananchi waache kudanganywa na kupotoshwa juu ya miradi hiyo.

"Kuna miradi ya barabara inayotekelezwa katika jiji la Arusha ambayo imesainiwa yenye thamani ya shilingi bilioni 26 kwa ajili ya kujenga barabara zote za jiji la Arusha fedha ambazo zimetolewa na serikali " amesema Gambo.

Amesema baadhi ya watu wanaendekeza unafiki ,porojo na uongo juu ya miradi hiyo ,kumbuka ukiwa mnafiki bado kijana ukifikia umri mkubwa utakuwa mchawi"

Gambo aliishukuru benki ya crdb kwa ushirikiano wake wa kifedha katika ujenzi wa miradi mbalimbali mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na serikali hapa nchini.


.......
download.jpeg
 
Asilaumu ameharibu yeye mwenyewe hilo jiji la Arusha, jiji lilikuwa linaingiza mapato ya kutosha kaja na jeuri yake ameharibu sasa ana lia na nani?
 
Pesa za serikali kuu na pesa za halmashauri zote si ni kodi zetu? Sasa tatizo liko wapi, mbona hamna mantiki ya kugombana? Kuku wako manati ya nini?

Cc Unforgetable
 
Pesa za serikali kuu na pesa za halmashauri zote si ni kodi zetu? Sasa tatizo liko wapi, mbona hamna mantiki ya kugombana? Kuku wako manati ya nini?

Cc Unforgetable
Huyu Gambo sijui kawaje,hukua hivo pindi Ukiwa pale Kwanjeka,halimashauri haijashindwa kutekeleza miradi,maana pesa zao mmewanyang'anya Kama vipi mwarudishie uone Kama hawata tekeleza.

Pia wewe umeenda kufungua kongamano au semina ya CRDB,hayo ya halimashauri mbona naona Kama si pahala pake?
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Kwani tatizo ni miradi kutekelezwa na serikali kuu, basi tutafuta halmashauri zote ili kupunguza fitina, majungu na kurogana..
 
Madaraka yanaenda na kuwajibika. Vijana wanajifunza kutokana na makosa. Uongozi mzuri ni ule ambao wengi wenu mnaafikiana
 
RC atupe makusanyo ya kodi Wilaya za Arusha na halmashauri zake tuanzie hapo ,halafu huu ujinga wa kusema pesa za Makufuli mtaacha lini!?
 
RC atupe makusanyo ya kodi Wilaya za Arusha na halmashauri zake tuanzie hapo ,halafu huu ujinga wa kusema pesa za Makufuli mtaacha lini!?
Hii ndio shida wa hizi praise team. Utadhani hii kodi inayokusanywa ni mali yao. Quite stupid
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Back
Top Bottom