RC Chalamila: Golikipa asipofungwa leo aje kuchukua crown kwangu

RC Chalamila: Golikipa asipofungwa leo aje kuchukua crown kwangu

tonicimmobility

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
493
Reaction score
1,038
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, Agosti 22, 2025 ametangaza motisha ya Shilingi milioni 20 kwa wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kuelekea mchezo wa robo fainali ya Michuano ya CHAN dhidi ya Morocco, unaotarajiwa kupigwa usiku huu katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.



Akizungumza na waandishi wa habari, Chalamila amesema fedha hizo zitakabidhiwa kwa wachezaji bila kujali matokeo ya mchezo huo. Aidha, ameeleza kuwa motisha hiyo imeambatana na viwanja viwili vilivyopo Kigamboni ambavyo pia vitatolewa kwa timu hiyo.

Amefafanua kuwa kwa kila goli litakalofungwa, kiasi cha Shilingi milioni 5 kitatolewa. Mfungaji wa bao atazawadiwa Shilingi milioni 1, huku mtoaji wa pasi ya bao akipata Shilingi laki tano.

Chalamila amesema hatua hiyo inalenga kuongeza morali kwa wachezaji wa Taifa Stars katika mchezo huo muhimu dhidi ya Morocco.
 
Wanasiasa watuachie mpira wetu bana
 
Hicho kitu anachoongea hakiwezekani maana lazma tufungwe ni sawa na konda awe kiziwi
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, Agosti 22, 2025 ametangaza motisha ya Shilingi milioni 20 kwa wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kuelekea mchezo wa robo fainali ya Michuano ya CHAN dhidi ya Morocco, unaotarajiwa kupigwa usiku huu katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

View attachment 3449010

Akizungumza na waandishi wa habari, Chalamila amesema fedha hizo zitakabidhiwa kwa wachezaji bila kujali matokeo ya mchezo huo. Aidha, ameeleza kuwa motisha hiyo imeambatana na viwanja viwili vilivyopo Kigamboni ambavyo pia vitatolewa kwa timu hiyo.

Amefafanua kuwa kwa kila goli litakalofungwa, kiasi cha Shilingi milioni 5 kitatolewa. Mfungaji wa bao atazawadiwa Shilingi milioni 1, huku mtoaji wa pasi ya bao akipata Shilingi laki tano.

Chalamila amesema hatua hiyo inalenga kuongeza morali kwa wachezaji wa Taifa Stars katika mchezo huo muhimu dhidi ya Morocco.
Hiyo siyo kutia Morari ni kind of wanga, crown kweli?
 
Back
Top Bottom