Rasimu itapita, chama kitakwama

Rasimu itapita, chama kitakwama

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Chama chetu cha Mapinduzi kimejipanga,tangu mwanzo wa mchakato,kudhibiti mchakato na kulinda maslahi ya kichama. Kinaelekea kuweza. Kuyalinda maslahi ya kichama ni kulinda sehemu kubwa ya Katiba ya sasa ambayo 'inabeba' chama chetu. Pamoja na sauti zinazopazwa kila uchao na wapinzani na wanaharakati,Rasimu inakaribia kupitishwa. Chama kimejiandaa na kujipanga kufanikisha hilo.

Mambo yote yameshawekwa tayari.Ndiyo maana sasa Katibu Mkuu Kinana na ujumbe wake wanatembea pande za Tanzania kwa raha zao kujiandaa na uchaguzi ujao. Hawana hofu juu ya kupita kwa Rasimu. Itapita tu. Katiba 'mpya' itapatikana.

Amini nawaambia, CCM itayumba na kusawajika ikipitaRasimu hii. CCM itajuta bila mafanikio kudhibiti mchakato na kupitisha Rasimu. Itakuwa too late! Kila mwananchi amejiandaa kivyake. Kwasasa Polisi wanaogopwa. Ukifika muda, wananchi watatamba kwa kura zao. Itakuwa heri ungekuwepo kuona ninachokisema hapa.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
hongera sana kwa kuona hilo bado wameziba masikio
 
Ni wengi tu tumeliona hilo, you cannot defend the indefensible!
Sasa hivi mambo yanakwenda kibabe kibabe bila kuchukua maoni ya wananchi, na hii ni hatari.
Kwahili la katiba kwakweli hata mimi nashuhudia masopakyindi umekuwa ukionyesha kutokuridhishwa na jinsi mambo yanavyokwenda pale Dodoma.Inafikia hatua unajiuliza,Mzee Sita kweli kachanganyikiwa au anaona liwalo na liwe kwa kuwa katelekezwa na Mh.Rais katika hili.Juzi ilikuwa aibu tupu wakati wanajadili jinsi ya kupiga kura,aliamua kujitoa ufahamu kabisa dhidi ya wale waliopinga namna ya upigaji wa kura.
 
Last edited by a moderator:
Acheni kuwachimba watu mkwara bana ina maana syndicate yote ile imeshindwa kuliona hili.
 
content ya Katiba itaibeba CCM big time, trust me!!! Wala tunaofuatilia content and process... the document answer citizen priorities of which administration is definetely leaders issues and wananchi issue!
 
Ccm inajichimia kaburi,itakuwa kazi rahisi sana ukawa kuwashawishi wananchi kwa kufanya ulinganifu tu,na kuweka chuki kidogo tu ya utanganyika.
 
Chama chetu cha Mapinduzi kimejipanga,tangu mwanzo wa mchakato,kudhibiti mchakato na kulinda maslahi ya kichama. Kinaelekea kuweza. Kuyalinda maslahi ya kichama ni kulinda sehemu kubwa ya Katiba ya sasa ambayo 'inabeba' chama chetu. Pamoja na sauti zinazopazwa kila uchao na wapinzani na wanaharakati,Rasimu inakaribia kupitishwa. Chama kimejiandaa na kujipanga kufanikisha hilo.

Mambo yote yameshawekwa tayari.Ndiyo maana sasa Katibu Mkuu Kinana na ujumbe wake wanatembea pande za Tanzania kwa raha zao kujiandaa na uchaguzi ujao. Hawana hofu juu ya kupita kwa Rasimu. Itapita tu. Katiba 'mpya' itapatikana.

Amini nawaambia, CCM itayumba na kusawajika ikipitaRasimu hii. CCM itajuta bila mafanikio kudhibiti mchakato na kupitisha Rasimu. Itakuwa too late! Kila mwananchi amejiandaa kivyake. Kwasasa Polisi wanaogopwa. Ukifika muda, wananchi watatamba kwa kura zao. Itakuwa heri ungekuwepo kuona ninachokisema hapa.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Hivi Mzee Tupatupa Wa Lumumba unafikri mtu kama CHOONI, Simiyu yetu, Ifweero, Mmaranguoriginal, Mamndenyi n.k watakuelewa sasa hivi? Kazi ipo!
 
Ni wengi tu tumeliona hilo, you cannot defend the indefensible!
Sasa hivi mambo yanakwenda kibabe kibabe bila kuchukua maoni ya wananchi, na hii ni hatari.

Huu ndio ukomavu wa kisiasa. Kusema ukweli hata kama ni mchungu ni heshima kwa mzungumzaji. Natamani sana baadhi ya watu fulani humu JF wangekusoma na kujifunza kwa faida ya nchi yetu.
Tanzania ni yetu sote. Kesho na keshokutwa Chadema, CCM au CUF vinaweza kutoweka ila taifa litabaki.
 
Sita akili na ufahamu umehamia ma.ta.ko.ni

QUOTE=Nzowa Godat;10691067]Acheni kuwachimba watu mkwara bana ina maana syndicate yote ile imeshindwa kuliona hili.[/QUOTE]
 
Kwa katiba hii sioni kama kulikuwa na haja ya kutumia mabilioni mengi namna ile kuja kutengeneze kitu kama hiki.. Kama katiba hii imepangwa kutuvusha miaka 50 ijayo basi kwa ujumla viongozi wetu wamejisahau sana. Viongozi wetu wamefikia hatua ya kutufanyia maamuzi sisi tuwe tunayafuata hasa kwa kufuata ushabiki wa chama. Wanasahau hata tukiwa wanachama bado tunatumia akili ya kutambua ni kipi kinatufaa kwa Tanzania ya sasa. For this, definitely we are going to fail...!!!
 
Kikwete alichelewa sana kulifuta hili BMK, hamna kitu walichofanya...cut and paste of the old one...
 
Back
Top Bottom