Ramadhani Mtoro Ongara a.k.a Dr. Remmy documentary.. Mnyonge lakini mtata..

Ramadhani Mtoro Ongara a.k.a Dr. Remmy documentary.. Mnyonge lakini mtata..

sosoliso

Platinum Member
Joined
May 6, 2009
Posts
8,543
Reaction score
9,480
Members..

Nimebahatika kuiona hii documentary ya nguli wa muziki wa miaka ya kati hapa (1977 - 1996) Ramadhani Mtoro Ongala au maarufu kama Dr. Remmy.. Kusema ukweli pamoja na kumfahamu Dr. Remmy kuna mengi sana ambayo nimeyajua kwenye hii documentary.. Nimeona niiweke hapa ili members muone pande zote za gwiji huyu.. kauli na nyimbo zake tata, ujumbe wake kwa wanyonge wenzie na kila kitu.. Pia ameshiriki rafiki yake Cosmas Chidumule ambae sasa ameokoka na anatangaza injili.. Kuna kila kitu humu, kuanzia vicheko, vijembe na kauli tata.. Unajua kwanini aliitwa mtoro..? Angalia hii na hakika utashngaa..!

 
Last edited by a moderator:
nimefurahi snaa kw hii documentary..nimependa wakati wako kwenye bus wanaenda njombe ule ubishani ndani ya bus kuhusu maswala ya mbinguni.....

jamaa alikuwa kichwa sana....
 
Ongala!kuna shindano la sura mbaya lilifanyika sikumbuki mwaka gani but kuna kijana anaitwa masudi sura mbaya alikuwa mitaa ya sharif shamba ndo alishinda kisha bakari mbelemba(jangala)akawa wa pili Ongala akawa wa tatu.Duh!ongala akasema"nimedhulumiwa nafasi ya pili kuhusu huyo kijana wa kwanza sina ugomvi nae huyu kijana ni mbaya kwelikweli"
Miaka ya 90 alitoa wimbo mambo kwa soksi wakasema hauna maadili leo condoms kila duka mnauza jamaa alichungulia mbali R.I.P. Ramadhani mtoro Ongala.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom