Iwensanto
JF-Expert Member
- Mar 7, 2019
- 1,173
- 1,092
Tatizo ni huyo Mudi anajifanya kila kitu anajua
Kwa msimu wa pili mfululizo Simba Sc wanasajili mchezaji idara ya Kiungo kwaajili ya mechi za kimataifa halafu anakuwa galasa!
Wote ni mashahidi mnamkumbuka yule Msudan Sharif El Din "Mhogo Mchungu" alivyokuja kuwa flop. Sasa ni zamu ya kiungo wa Kizambia, Rally Bwalya nae alikuja kwa mbwembwe nyingi ila ameishia kuwa flop. Hajakidhi yale matarajio makubwa ya wapenda kandanda!
Klabu ya Simba ifike wakati wabadilike, badala ya kusajili magarasabya kigeni kwa bei nyingi ni heri wawape nafasi wazawa tu! Huwezi ukamnunua mchezaji kwa bei kubwa halafu mechi kama ya juzi ya Plateau anawekwa benchi na mchezaji mzawa kama Mzamiru Yassin!
Ni hayo tu, povu ruksa!