Raisi wa Ukraine ni wanted

Raisi wa Ukraine ni wanted

Dingswayo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
4,019
Reaction score
2,932
Raisi wa Ukraine Yanokovich anatafutwa akamatwel kwa mauaji ya raia waliokuwa wakiandamana kumpinga. Haijulikani alipihificha.



Sent from my Lumia phone using Tapatalk
 
Nimemsikia yule kiongozi wa upinzani aliyekuwa amefungwa gerezani miaka kama miwili hivi akisema maneno ya busara sana, kuwa walimueleza akajifanya kutowasikiliza kwa sababu ya jeuri ya madaraka aliyokuwa nayo. Sasa anakuja kukimbia nchi baada ya watu wengi kupoteza maisha wakati angeliwasikiliza haya yote yasingetokea!! Sasa madaraka hana tena na anatafutwa.
Ukiwauliza wanasiasa wetu hapa watakwambia "hapa kwetu kitu kama hili hakiwezekani"! Ngoja tusubiri tu.
Ukraine imetoa waranti wa kukamatwa kwa Rais aliyeondolewa madarakani Viktor Yanukoviych ambaye anasakwa na polisi kwa kuhusika na mauaji ya umma wa watu wakati nchi hiyo ikikabiliwa na jukumu la dharura la kuunda serikali mpya na kumteua waziri mkuu kuingoza nchi hiyo kufuatia machafuko ya kisiasa yaliodumu kwa miezi kadhaa. Zaidi kuhusu hali ya Ukraine,tembelea ukurasa wetu wa mtandao.
Source: DW
 
130216092115_yanukovych_victor_304x171_bbc_nocredit.jpg



Rais wa Ukraine aliyeondolewa madarakani Victor Yanukovych amefunguliwa mashtaka


Ukraine imetoa hati ya kukamatwa kwa Rais aliyeondolewa madarakani, Victor Yanukovych, Waziri wa mambo ya ndani wa mpito ametangaza hatua hiyo.
Arsen Avakov amesema katika ukurasa wa Facebook amesema kesi dhidi yake imefunguliwa dhidi ya Yanukovych na maafisa wengine kuhusu mauaji ya makubwa ya watu.
Wabunge walipiga kura kumuondoa Yanukovych siku ya jumamosi baada ya maandamano ya miezi kadhaa yaliyojitokeza baada ya kupinga kujiunga na Umoja wa Ulaya.
Machafuko yaliyotokana na maandamano hayo yalisababisha watu kadhaa kupoteza maisha juma lililopita.
Avakov amesema Yanukovych alionekana mjini Balaklava siku ya jumapili, lakini mpaka sasa hajulikani mahali alipo.

source;BBC
 
Back
Top Bottom