Rais wetu umesema unataka Tanzania mpya wananchi tunataka katiba pendekezwa ya Warioba

mwembemdogo

JF-Expert Member
Feb 28, 2016
2,282
1,251
Mh.Magufuli katika kampeni zako uliahidi unataka kujenga Tanzania Mpya.Ni wazo zuri sana tumelikubali.Ombi letu kwako Kwa kuwa una uchungu Na nchi hii tunakuomba ufikirie jinsi Kodi za walala hoi wa Nchi hii zilivyotumika kuandaa Rasimu ya Katiba , Kurekebisha Jengo la bunge, Kuwalipa posho wajumbe 600 Na mwisho wa siku hakuna cha Katiba.Mh.Magufuli tunaitaka Rasimu ya Warioba kwani ndio maoni Yetu Na sio vinginevyo.Mh.Magufuli Haya majipu unayohangaika nayo in ubovu wa Katiba iliyopo.Mh.Magufuli tukamilishie
Katiba Yetu Kwa kuwaacha wanasiasa kando kwani wao ndio walioharibu Rasimu ya Warioba iliyokuwa Na Misingi mizuri.
 
Nafikiri umechanganya mada katiba inayopendekezwa siyo ya Warioba, ya Warioba ni Rasimu ya II. Na ndiyo watu wengi tu ayoipenda ipitishwe kuwa katiba mpya ya familia
 
Nashukuru MKUU tunata Rasimu ya warioba ndio iboreshwa kwani ndio maoni yetu
 
Aaaaaah! Kwa kweli katiba mpya ni sawa lakini haikuwa kwenye ilani yetu, kwa hiyo katiba ni jambo la ziada japo inahitajika.


Namkumbuka Dk Slaa aliyetuahidi katiba mpya ndani ya siku mia tu, mlikosea kumfanyia figisu-figisu.
 
Back
Top Bottom