G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Rais wangu Magufuli. Nimepewa taarifa kuwa fedha walizofungulia "fixed account" bodi ya wakurugenzi wa TRA ni fedha za kawaida za uendeshaji wa miradi ya TRA. Fedha hizi hazihusiani kabisa na fedha za mapato kutoka vyanzo mbalimbali (mapato yanayotuumiza na yale yasiyotuumiza). Sasa rais wangu hadi hili kweli ni vibaya kufungua "fixed account" ili kupata faida? Kwanini umewatenda wakusanyaji wako wazuri wa mapato hivyo?
Rais wangu naomba nikueleze kuwa hivi karibuni nitaandika makala humu kukushauri kwa dhati kabisa na wewe ufungue fixed account ila utakapochukua mikopo basi ile "interest rate" iwe sawia na ile ya kupata kutoka katika hizo "fixed account" Rais wangu uchumi unakufa! Amini hivyo!
Turudi kwenye mada! Hivi kweli hawa watu wana kosa gani? Kutokutii amri yako? Ipi? Ulichoagiza kisipelekwe huko kwenye mabenki yanayoenda mufilisi ni fedha za mapato ya serikali na siyo hizo zao binafsi kama TRA? Unajua kuwa bado jengo jipya la TRA halijakamilika? Bado wanadaiwa na wakandarasi? Kwanini wasijiongeze?
Kwakweli rais wangu kama tutaendelea kwenda hivi hatutafika mbali, naomba kukueleza kwa dhati kabisa kuhusu hilo.
Rais wangu naomba nikueleze kuwa hivi karibuni nitaandika makala humu kukushauri kwa dhati kabisa na wewe ufungue fixed account ila utakapochukua mikopo basi ile "interest rate" iwe sawia na ile ya kupata kutoka katika hizo "fixed account" Rais wangu uchumi unakufa! Amini hivyo!
Turudi kwenye mada! Hivi kweli hawa watu wana kosa gani? Kutokutii amri yako? Ipi? Ulichoagiza kisipelekwe huko kwenye mabenki yanayoenda mufilisi ni fedha za mapato ya serikali na siyo hizo zao binafsi kama TRA? Unajua kuwa bado jengo jipya la TRA halijakamilika? Bado wanadaiwa na wakandarasi? Kwanini wasijiongeze?
Kwakweli rais wangu kama tutaendelea kwenda hivi hatutafika mbali, naomba kukueleza kwa dhati kabisa kuhusu hilo.