Rais tumtakae 2015 ni lazima:Awe mzalendo kwa vitendo;
Awe na uchungu na Rasilimali zetu;Achukie ufisadi na rushwa na lazima atuonyeshe kuwa anakerwa na mambo kwa dhati;Aheshimu Demokrasia;Asiwe mKabila,mDini au mKanda;Asiwe na kashfa za Ufisadi;Asiwe na tamaa ya madaraka;Asiwe ni miongoni mwa walio laaniwa na Baba wa Taifa;Awe ni mwanaSiasa anayependelea siasa safi;
Anayechukia na kuzikemea siasa chafu;Awe ni mwenye maono ya mbali;Mwenye mawazo ambayo yalileta matokeo mazuri iwe katika Chama chake cha Siasa au serikali aliyowahi kuitumikia;Awe anapendelea uwazi na awe tayari kutuambia Watanzania kiasi cha mali anachomiliki na atuambie namna alivyoipata hiyo mali;
Aiunge mkono Rasimu ya Katiba mpya;Akerwe na matumizi makubwa yasiyo na tija kwa Taifa yanayofanywa na Serikali;Achukie uchumi unaendeshwa kwa Mikopo;Akerwe na deni la Taifa;Achukie mfumko wa Bei;Achukie uduni wa miundo mbinu yetu ya barabara na reli;Na awe anapendelea diplomasia ya kiuchumi na Mataifa mengine.
Huyo ndiye hasa Rais tumtakae 2015.
Awe na uchungu na Rasilimali zetu;Achukie ufisadi na rushwa na lazima atuonyeshe kuwa anakerwa na mambo kwa dhati;Aheshimu Demokrasia;Asiwe mKabila,mDini au mKanda;Asiwe na kashfa za Ufisadi;Asiwe na tamaa ya madaraka;Asiwe ni miongoni mwa walio laaniwa na Baba wa Taifa;Awe ni mwanaSiasa anayependelea siasa safi;
Anayechukia na kuzikemea siasa chafu;Awe ni mwenye maono ya mbali;Mwenye mawazo ambayo yalileta matokeo mazuri iwe katika Chama chake cha Siasa au serikali aliyowahi kuitumikia;Awe anapendelea uwazi na awe tayari kutuambia Watanzania kiasi cha mali anachomiliki na atuambie namna alivyoipata hiyo mali;
Aiunge mkono Rasimu ya Katiba mpya;Akerwe na matumizi makubwa yasiyo na tija kwa Taifa yanayofanywa na Serikali;Achukie uchumi unaendeshwa kwa Mikopo;Akerwe na deni la Taifa;Achukie mfumko wa Bei;Achukie uduni wa miundo mbinu yetu ya barabara na reli;Na awe anapendelea diplomasia ya kiuchumi na Mataifa mengine.
Huyo ndiye hasa Rais tumtakae 2015.