Chonde chonde Rais Kikwete watanzania tunakuangalia, dunia inakuangalia kuhusiana na matukio yanayoashiria uvunjivu wa amani ya Tanzania tuliyoizoea. Polisi wamegeuka chinja chinja rais umenyamaza kimya kama hakuna linalotokea, angalia yaliyotokea Arusha, songea, morogoro na juzi juzi mwandishi wa habari pale Nyololo Iringa. Kuna tetesi kuwa wewe na chama chako cha CCM ndiyo mnaowatuma polisi ili wapunguze nguvu ya CHADEMA, binafsi imenichukua muda mrefu kuamini lakini sasa nimeanza kuamini
Kinachofanya niamini ni mazingira yenyewe kama vile ukimya wako, hakuna hata polisi aliyekamatwa, hata huyo aliyefikishwa mahakamani Iinga juzijuzi kafichwa sura, Kamhanda aliyeamuru Mwangosi auawe kuna tetesi mnataka kumhamishia makao makuu kwa nini tusianze kuamini hizo tetesi?
Hakuna hata binadamu aliyepewa mamlaka ya kuua na ndiyo maana hata Mungu hakumpa uwezo mwanadamu kuumba.Fikiri juu ya hili ungekuwa wewe ndo unaguswa na matukio haya ungenyamaza kwa utashi tu wa siasa, ungekuwa wewe ndo Mwangosi kuacha watoto wadogo vile. Naomba toa karipio kwa jeshi la polisi waacche kuua raia vinginevyo Mungu ataingilia kati kutokana na manung'uniko ya Taifa hili hata wewe hutakuwa salama. Damu isiyo na hatia haipaswi kumwagika bure si kitu cha kawida kwenye Taifa ambalo wote tuliitana ndugu.
Mwisho nitoe ombi la pekee; hata baada ya uchaguzi mkuu ujao naomba chonde kama Chadema watashinda wape haki yao vinginevyo itakuwa shida kwani hali iko waazi na hatuhitaji mtabiri kutuambia kilicho mbele yetu. Kemea jeshi lako na hata mawaziri wanaojipendekeza kwako hata kwa kusababisha migogoro. Nahitimisha kwa kusema madaraka uliyo nayo ni makubwa mno toa amri gazeti la Mwanahalisi pia lifunguliwe. Unapokuwa na vyombo vinavyokosoa kwa undani ni rahisi kujirekebisha. Sawa na mtu anayekuambia toa tongotongo jichoni anakupenda kuliko yule anayesema umependeza lakini kifungo umefunga vibaya. usipuuze ushauri huu unaweza kuliponya Taifa hili.
Fikiri tangu Polisi walipoanza kuua raia je raia wanaogopa au ndo wanasonga mbele. Mabadiliko yanapokuja huja na hakuna anayeweza kuyabadilisha kwa njia yoyote ile kumbuka ta Libya na Tunisia
Kinachofanya niamini ni mazingira yenyewe kama vile ukimya wako, hakuna hata polisi aliyekamatwa, hata huyo aliyefikishwa mahakamani Iinga juzijuzi kafichwa sura, Kamhanda aliyeamuru Mwangosi auawe kuna tetesi mnataka kumhamishia makao makuu kwa nini tusianze kuamini hizo tetesi?
Hakuna hata binadamu aliyepewa mamlaka ya kuua na ndiyo maana hata Mungu hakumpa uwezo mwanadamu kuumba.Fikiri juu ya hili ungekuwa wewe ndo unaguswa na matukio haya ungenyamaza kwa utashi tu wa siasa, ungekuwa wewe ndo Mwangosi kuacha watoto wadogo vile. Naomba toa karipio kwa jeshi la polisi waacche kuua raia vinginevyo Mungu ataingilia kati kutokana na manung'uniko ya Taifa hili hata wewe hutakuwa salama. Damu isiyo na hatia haipaswi kumwagika bure si kitu cha kawida kwenye Taifa ambalo wote tuliitana ndugu.
Mwisho nitoe ombi la pekee; hata baada ya uchaguzi mkuu ujao naomba chonde kama Chadema watashinda wape haki yao vinginevyo itakuwa shida kwani hali iko waazi na hatuhitaji mtabiri kutuambia kilicho mbele yetu. Kemea jeshi lako na hata mawaziri wanaojipendekeza kwako hata kwa kusababisha migogoro. Nahitimisha kwa kusema madaraka uliyo nayo ni makubwa mno toa amri gazeti la Mwanahalisi pia lifunguliwe. Unapokuwa na vyombo vinavyokosoa kwa undani ni rahisi kujirekebisha. Sawa na mtu anayekuambia toa tongotongo jichoni anakupenda kuliko yule anayesema umependeza lakini kifungo umefunga vibaya. usipuuze ushauri huu unaweza kuliponya Taifa hili.
Fikiri tangu Polisi walipoanza kuua raia je raia wanaogopa au ndo wanasonga mbele. Mabadiliko yanapokuja huja na hakuna anayeweza kuyabadilisha kwa njia yoyote ile kumbuka ta Libya na Tunisia