PreGE2025 Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said aboresha taarifa zake za Mpiga Kura Kigamboni

PreGE2025 Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said aboresha taarifa zake za Mpiga Kura Kigamboni

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Rais wa Klabu ya Yanga, Injinia Hersi Said, ameungana na Watanzania wengine katika zoezi la kuboresha taarifa za Mpiga Kura kwa mwaka 2025, ambapo leo ameboresha taarifa zake katika shule ya Amani Gomvu, iliyopo Mtaa wa Minondo, Kata ya Somangila, wilayani Kigamboni.

1747892994959.png
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Hersi ameandika: "Leo nimejumuika na Watanzania wenzangu wa Kigamboni kuboresha taarifa zangu za Mpiga kura. Zoezi hili lilifanyika katika shule ya Amani Gomvu, Mtaa Minondo, Kata ya Somangila, wilaya ya KIGAMBONI."

Aidha, ametumia fursa hiyo kuwaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwenye daftari la Mpiga Kura ili waweze kutimiza haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa miaka mitano ijayo.

Hersi alihitimisha kwa kusema: "Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Kigamboni."

5.PNG
 
Sijui kama ni habari.
Lajini tulisikia anajiandaa kugombea ubunge Kongwa (kwa Ndygai).
 
"Katika uongozi wangu, nitahakikisha naijengea Yanga uwanja wake, afe kipa afe beki" - Hersi

NB: bado miezi miwili muda uishe. Atatuchagulia kipa wa kufa (Diara au Mshery) na beki wa kufa (Baka au Mwamnyeto)
 
Sijui kama ni habari.
Lajini tulisikia anajiandaa kugombea ubunge Kongwa (kwa Ndygai).
Wanaoshughulika na hili zoezi ni wanufaika wa moja kwa moja wa "uchaguzi"...kama hutegemei kugombea nafasi yoyote utaamua mwenyewe😏
 
Back
Top Bottom