Rais wa China kuhutubia Afrika leo

Rais wa China kuhutubia Afrika leo

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,686
Rais wa China, Xi Jinping aliwasili nchini jana saa 10:5 akitumia ndege Boeng 747 ya Shirika la Ndege la China na leo atazungumza kwa mara ya kwanza na Afrika akitumia jukwaa la Tanzania.
Jinping atatoa hotuba yake kwenye jengo jipya la kisasa la Mwalimu Nyerere ambalo limejengwa na Serikali ya China likiwa na uwezo wa kuchukua watu 1,800 kwa mara moja lilipo jijini.
Rais huyo ambaye ameambatana na mkewe pamoja na maofisa mbalimbali wa Serikali yake,anatajiwa kutambulisha sera kwa Bara la Afrika huku wachunguzi wa mambo wakisema kuwa hotuba yake hiyo huenda itazingatia juu ya uimarisha uhusiano mwema baina ya pande zote mbili.
China ndiyo dola inayotajwa kuwa na ushawishi mkubwa barani Afrika na katika kipindi cha muongo mmoja uliopita kiwango cha ufanyaji biashara baina ya pande hizo mbili kinatajwa kukua kwa asilimia 70. China pia ndiyo mshirika pekee kwa Afrika ambaye misaada yake inaambatana na masharti nafuu.
Hata hivyo ushawishi wa China barani Afrika unakosolewa na baadhi ya nchi za Magharibi zinazoituhumu China kwamba inazinyonya nchi za Afrika.
Alipowasili jana kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Rais huyo alipokewa na mwenyeji wake Rais Jakaya Kikwete na kisha alipigiwa mizinga 21 na baadaye alikagua gwaride. Baada ya mapokezi hayo ya uwanjani, Rais Jinping na mwenyeji wake walioogoza kwenda jijini ambapo jioni ya jana walikuwa na mazungumzo ya faragha na baadaye walijumuika na halaika kwa ajili ya kushiriki dhifa ya taifa.
Wakati wa mapokezi vikundi vya ngoma vya utamaduni vilipendezesha mapokezi hayo kutokana na burudani ya kusisimua iliyotolewa. Hata hivyo baadhi ya wapiga picha walijikuta kwenye wakati mgumu baada ya Maofisa Usalama wa China waliokuwa wakiwatimua wapiga picha hao.
Katika ziara yake, Rais wa China na Tanzania zitatiliana saini mikataba 17 inayohusu maendeleo na uimarishwaji uhusiano wa kidiplomasia. Waziri wa Mambo ya Nchi na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe alisema kuwa China inakusudia kuipiga jeki Tanzania katika maeneo ya miundo mbinu, soko la kibiashara na sekta ya habari na mawasiliano.
“ Pamoja na kwamba leo Rais Jinping atazungumzia sera yake kuhusu Afrika, lakini pia anatazamia kukabidhi rasmi funguo za jengo la Mwalimu Nyerere kwa Rais Kikwete ambalo Serikali ya China imejenga. Jengo hili lina uwezo wa kuchukua watu 18,000 na kwetu sisi ni fahari kubwa” alisema Waziri Membe.
Hii ni ziara yake ya kwanza barani Afrika tangu alipochukua wadhifa huo wiki tatu zilizopita. Tanzania inakuwa nchi ya kwanza kutembelewa na kiongozi huyo ambaye pia serikali yake imehaidi kujenga bandari mpya ya Bagamoyo.
Baada ya kutoa hutuba yake kwenye ukumbi mpya wa Mwl. Nyerere Jinping atatembelea makaburi ya wataalamu wa China na baadaye ataelekea Afrika Kusin ambako kesho atashiriki mkutano unaoshirikisha nchi tano zilizopiga hatua kimaendeleo Brics. Nchi zinazounda umoja wa huo ni pamoja na China, Brazil, Urusi na Afrika Kusin.

CHANZO: Rais wa China kuhutubia Afrika leo - Kitaifa - mwananchi.co.tz
 
huyu jamaa natafuta nini hapa nchini baada ya kutuingiza katika siasa za ujama na kujitegemea tukatawaliwa mpaka Mtwara wakatembea Uchi? Yeyey kaja Tanzania, leo hii kutaka kuhutubia africa kupitia jukwaa la Tanzania ni utoto mtupu. Tulipokuwa wajamaa na kujitegemea, china iliipenda africa kupita nchi zote africa ingawa Ujamaa ulikuwa unatutia umasikini. sasa hivi hawa wachina baada ya kusikia kuna demokrasi africa, wanaipenda Kenya na South africa na kidogo misri kupita Tanzania maaana huko nchi za Kenya, south Africa na Misri wameweka miradi mikubwa sana ya maendeleo inayotoa ajira kubwa kwa wananchi wa huko. kumbuka nchi hii mpaka leo haija koma kuleta bidhaa mbovu hapa nchini , na ilifikia wakati walithubutu hata kuleta maziwa ya sumu ya kwa matumizi ya watoto. je kwa nini apewe mapokezi makubwa namna hiyo mtu nchi yake iliyowahi kuleta maziwa ya sumu ya kudhulu watoto wetu?

Kwangu mimi hili jitu liitwalo raisi wa china halina tofauti na chunusi mkamata watoto baharini.
 
Hata haiingii akilini! Anahutubia Africa kwani yeye ni rais wa dunia?
 
Ataenda lini kariakoo kwa wenzake??

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
huyu jamaa natafuta nini hapa nchini baada ya kutuingiza katika siasa za ujama na kujitegemea tukatawaliwa mpaka Mtwara wakatembea Uchi? Yeyey kaja Tanzania, leo hii kutaka kuhutubia africa kupitia jukwaa la Tanzania ni utoto mtupu. Tulipokuwa wajamaa na kujitegemea, china iliipenda africa kupita nchi zote africa ingawa Ujamaa ulikuwa unatutia umasikini. sasa hivi hawa wachina baada ya kusikia kuna demokrasi africa, wanaipenda Kenya na South africa na kidogo misri kupita Tanzania maaana huko nchi za Kenya, south Africa na Misri wameweka miradi mikubwa sana ya maendeleo inayotoa ajira kubwa kwa wananchi wa huko. kumbuka nchi hii mpaka leo haija koma kuleta bidhaa mbovu hapa nchini , na ilifikia wakati walithubutu hata kuleta maziwa ya sumu ya kwa matumizi ya watoto. je kwa nini apewe mapokezi makubwa namna hiyo mtu nchi yake iliyowahi kuleta maziwa ya sumu ya kudhulu watoto wetu? Kwangu mimi hili jitu liitwalo raisi wa china halina tofauti na chunusi mkamata watoto baharini.
Baada ya kuacha siasa Ujamaa na Kujitegemea tumepiga hatua yoyote?
 
Back
Top Bottom