Nimesikiliza hotuba ya Rais juu ya uwekezaji kwenye madini na gesi. kwa kifupi imenisikitisha sana. Mbali na kukubaliana na mengi uliyoyafanya Rais wangu hili la madini nakupinga mapema sana. Rais kutoa kauli kuwa eti kuchimba kisima kimoja kutafiti gesi ni zaidi ya dola milioni 100 na kuuliza nani ataweza .... ni udhaifu na dharau kubwa kwa nchi na watu wake. Utafiti wa gesi ulianza miaka ya 1950s hapa Tanzania. Hebu tujiulize ni kwa nini mwalimu Nyerere aliacha madini yetu kwa miaka yote hii?Hakukuwa na wazungu wenye uwezo wa kuja na kuyafyonza yote na kutulipa % iwe 65% au 75%? Jibu ni moja kujenga uwezo kwa watanzania kumiliki na kuendeleza sekta hiyo ya madini. Hakuna unafiki hapo.
Sidhani kama Rais alitoa hotuba ya jana kwa kuambiwa au kusikia. Nilitegemea hili, Serikali iwaandae watanzania kumiliki na kuendeleza uwekezaji kwenye gesi na madini. Kauli ya kuwambia watashirikishwa IFUTWE kabisa ni uongo na dharau nyingine. Unaweza kushirikiswha kwa kutolewa hotuba tu kama hizi. Pamoja na kuwa ni biashara kubwa duniani kiundwe chombo cha kuwawezesha hao wenye mitaji midogo kuunganishwa kwa shares na kuwekeza kwenye gesi. vinginevyo isichimbwe tusubiri capacity building ifanyike. Hata makampuni mengi ya nje hayakutoka mbinguni na uwezo huo,yamewezeshwa na mitaji midogo iliyokusanywa na kuthibitiwa. Kupitia TPDC watanzania na mitaji yao wawezeshwe kwanza na sio wadharauliwe kama alivyofanya katibu mkuu wa wizara, waziri Muhongo na sasa Rais.
Njia moja pia ni kwa hayo makampuni yanayosifiwa kutoka nje yalazimishwe kuwapa shares watanzania moja kwa moja kwenye shughuli za gesi na madini. Yalazimishwe kuwaajiri watanzania asilia. Kama hiyo haifanyiki WAONDOKE. Tuangalie wenzetu wa Asia kusini wanafanya nini. tufahamu kwamba wao sasa hivi wanatuhitaji sisi zaidi kuliko hapo kabla.
Kwa hili Rais umekosea kama ilivyo kwenye sekta ya Ujenzi (Construction) ambapo tunaona miradi mikubwa wanapewa wageni kwa vigezo vya kutokuwa na uwezo. Baada ya ujenzi kukamilika hatuna wazalendo wanaokuwa na uwezo kuisimamia miradi hiyo tunawaita tena wageni hao na kuwapa ajira hizo for the life time of the project. Tutaona tu kwenye daraja la Kigamboni.Serikali imenunua vifaa vya ujenzi kwa mfano na kuwakodishia wazalendo ili kushindana kimataifa kama CRJC etc?
Hotuba ya Rais ni sawa na kudharau chakula cha nyumbani ukisema pamoja nakuwa mnajua kupika hamuwezi kupikia kwenye JIKO hili.Utakula huko nje hadi lini?
Rais wafanye watanzania waweze KUMILIKI NA KUTHIBITI SEKTA YA MADINI NA GESI KWANZA ( sio washirikishwe) Vinginevyo yote uliyofanya kwa kipindi chako yatakuwa hayana maana.
wana jf endeleeni...........
Sidhani kama Rais alitoa hotuba ya jana kwa kuambiwa au kusikia. Nilitegemea hili, Serikali iwaandae watanzania kumiliki na kuendeleza uwekezaji kwenye gesi na madini. Kauli ya kuwambia watashirikishwa IFUTWE kabisa ni uongo na dharau nyingine. Unaweza kushirikiswha kwa kutolewa hotuba tu kama hizi. Pamoja na kuwa ni biashara kubwa duniani kiundwe chombo cha kuwawezesha hao wenye mitaji midogo kuunganishwa kwa shares na kuwekeza kwenye gesi. vinginevyo isichimbwe tusubiri capacity building ifanyike. Hata makampuni mengi ya nje hayakutoka mbinguni na uwezo huo,yamewezeshwa na mitaji midogo iliyokusanywa na kuthibitiwa. Kupitia TPDC watanzania na mitaji yao wawezeshwe kwanza na sio wadharauliwe kama alivyofanya katibu mkuu wa wizara, waziri Muhongo na sasa Rais.
Njia moja pia ni kwa hayo makampuni yanayosifiwa kutoka nje yalazimishwe kuwapa shares watanzania moja kwa moja kwenye shughuli za gesi na madini. Yalazimishwe kuwaajiri watanzania asilia. Kama hiyo haifanyiki WAONDOKE. Tuangalie wenzetu wa Asia kusini wanafanya nini. tufahamu kwamba wao sasa hivi wanatuhitaji sisi zaidi kuliko hapo kabla.
Kwa hili Rais umekosea kama ilivyo kwenye sekta ya Ujenzi (Construction) ambapo tunaona miradi mikubwa wanapewa wageni kwa vigezo vya kutokuwa na uwezo. Baada ya ujenzi kukamilika hatuna wazalendo wanaokuwa na uwezo kuisimamia miradi hiyo tunawaita tena wageni hao na kuwapa ajira hizo for the life time of the project. Tutaona tu kwenye daraja la Kigamboni.Serikali imenunua vifaa vya ujenzi kwa mfano na kuwakodishia wazalendo ili kushindana kimataifa kama CRJC etc?
Hotuba ya Rais ni sawa na kudharau chakula cha nyumbani ukisema pamoja nakuwa mnajua kupika hamuwezi kupikia kwenye JIKO hili.Utakula huko nje hadi lini?
Rais wafanye watanzania waweze KUMILIKI NA KUTHIBITI SEKTA YA MADINI NA GESI KWANZA ( sio washirikishwe) Vinginevyo yote uliyofanya kwa kipindi chako yatakuwa hayana maana.
wana jf endeleeni...........