Rais Samia Suluhu imulike NHIF

Huduma hii ipo kwenye hospital chache sana, nyingi bado hazijafikiwa na hii
 
Huu mfuko unatakiwa uvunjwe haraka
Alafu ukishavunjwa?.Toa ufumbuzi wanini kifanyike sio kusema uvunjwe tu.maana huo mfuko bsdo ni msaada kwa wananchi wengi kwahiyo kama kuna mapungufu ni jukumu la wadau kuyazungumza na wahusika kuyafanyia kazi.
 
Huu mfuko lengo lilikuwa nzuri lakini baadae serikali ya awamu ya mwendazake ilianza kutumia pesa hizi kama chanzo cha mapato hivyo kuharibu kabisa mfumo wa matibabu.
 
Hata ya kimila wanatoa cheti,alafu unataka wakupe kadi bila cheti hivi inaingia akilini kweli?nani anauhakika umeoa bila kuwepo na document,je kama ni hawara yako nawe ukasema ni mke wangu?
 
Alafu ukishavunjwa?.Toa ufumbuzi wanini kifanyike sio kusema uvunjwe tu.maana huo mfuko bsdo ni msaada kwa wananchi wengi kwahiyo kama kuna mapungufu ni jukumu la wadau kuyazungumza na wahusika kuyafanyia kazi.
Mapungufu yamezungumzwa miaka yote lakini hakuna kinachobadilika zaidi ya upigaji, bora ku-outsource
 
Hata ya kimila wanatoa cheti,alafu unataka wakupe kadi bila cheti hivi inaingia akilini kweli?nani anauhakika umeoa bila kuwepo na document,je kama ni hawara yako nawe ukasema ni mke wangu?
Hiyo bima unapewa sio kama msaada kuna hela ambayo unakatwa ili kucover hizo gharama za matibabu mchangiaji ndio mwenye mandate ya kuamua amuweke nani huo urasimu wa kuzuia mtu asimweke anayemtaka unatokana na sababu zipi zenye mashiko mbali na kuhofia kupungua kwa kibubu chao ambacho obviously kujaa kwake kumetokana na michango ya mchangiaji.Kama ni sheria au kanuni lazima ifanyiwe amendment
 
Kitu kingine cha ajabu kwa huo mfuko ni pale unapotaka kumuweka mnufaika ambaye lazima awe mzazi au mtoto na uweke cheti cha kuzaliwa.

Kwa upande wa watoto sina tatizo shida upande wa wazazi lazima awe mzazi wako na cheti chako cha kuzaliwa kidhihirishe hivyo je kwa wale ambao walisomeshwa na ndugu wanapokosa fursa hiyo ya kupatiwa kadi watakuwa wanatendewa haki?

Maskini wa Mungu utakuta mchangiaji alishafiwa na wazazi zamani na waliomsomesha ni hao wanaokatatazwa kwa sheria za NHIF kugharamiwa matibabu na mfuko
 
Kwa Sasa gharama ulizotumia.... Zinatumwa.
 
Kuna wakati mtu unaamua uingie tu mfukoni kutibiwa kuliko kutegemea hiyo bima.
 
Kuna wakati mtu unaamua uingie tu mfukoni kutibiwa kuliko kutegemea hiyo bima.
Nhif ni majizi, borra kuzama mfukoni kuliko kuhangaika na urasimu wao
 
Hapa ndio penye shida ,sijui waliwaza nini
 
NHIFTZ

Naomba kufahanu mfuko ulitumia kigezo Gani kuwaondoa ndugu wengine kama waanaufaika!

Katika jamii zetu Kuna watu walifiwa na wazaI wakatunzwa na ndugu wengine ...kama wazazi ,Sasa Kuna ubaya gani mtu huyu akimwingiza huui mlezi wake kuwa mnufaika!

Kiafrika kusomesha au kumtunza mtoto ni uwekezaji, no kama hifadhi ya Jamii isiyo Rasmi ,iqeje Mfuko usitambue hili!

Au kwa kudura ya Mnyazi Mungu Mwanachama hakubahatika kupata m/watoto Kuna ubaya Gani akawaingiza ndugu wengine...ambapo pia atajuwaa anatanua WiGo was Hifadhi ya Jamiikatika Afya Kwa familia yake?!

Naomba ufafanuzi ktk hili!
 
NHIF Ina maana hujauona huu mchango😣
 
Hawa watu wa NHIF wana mambo ya hovyo sana unaenda hospitali nzuri inafika wakati wa dawa dr kufanya prescription analazimisha dawa flani

, Kuna siri nliipata kua kama una NHIF na unastahili dawa fulani hasa za nje ya tz Dr anakuambia tu hiyo hapa hatuna ili usilalamike kumbe ni vile miongozo ya bima inazuia maana ina “bei” !
 
Umeandika kishabiki vitu vingi ulivyoandika si vya kweli
 
Hospital ya Ben Mkapa kila huduma unayopewa na gharama ipo kwenye risiti na hata msg ikija kwenye simu inakuja na jumla ya gharama ulizotumia
NHIF walazimishe Hospital iandike gharama za biadhaa ma huduma zao. Bei iandikwe Mapokezi, kwenye fomu na ukiondoka upewe risiti ya huduma na bidhaa husika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Landcruiser ndo mpango mzima
 
Umeandika kishabiki vitu vingi ulivyoandika si vya kweli
Yawezekana wewe ni NHIF, nakushauri wewe na timu yako mwende mkakutane na watumiaji wa NHIF msikie live dukuduku zao dhidi yenu, itisheni mikutano na wadau wawaambie wanayokutana nayo huko mahospitalini, msijifungie vyumbani kuogopa mashambulizi, kama mnazo hoja mbona hamjitokezi hadharani kujibu mapigo?
 
DAAH MIE NMEKATA JUZI JUZI YA 240K , NATUMAINI WATAKUWA WAMEISHA BORESHA HIZI CHANGAMOTO ZA HAPA NA PALE.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…