Tangu alipochukua uongozi wa nchi baada ya mtangulizi wake kufariki, Rais Samia amekumbana na upinzani mwingi kutoka ndani na nje ya Chama chake.
Ndani ya Chama chake wapo ambao hawakutaka Samia aapishwe kuwa Rais kama Katiba inavyosema kwani yeye ndiye alikuwa Makamu wa Rais. Hawa walikuwa na hiyo mipango kwa sababu zao binafsi na pia ubaguzi wa Moja kwa moja kwamba kwa kuwa Samia ni mwanamke asingeweza kuongoza nchi. Wakijifanya hamnazo ilhali wanajua Urais ni Taasisi.
Kulikuwa na ufa mkubwa kwetu sisi na nchi nyingine hususani zile za wenzetu. Dunia ni Kijiji, lakini sisi wakati ule kutokana na mtazamo na maono ya kiuongozi ya wakati ule tulikuwa hatuundi Kijiji hicho cha Dunia Moja.
Rais Samia alianza kuturejesha tena kwenye Kijiji cha dunia Moja. Tuliona ziara nyingi za kule na huko. Hilo likapita.
Rais Samia aliona Demokrasia nchini ilikuwa na dosari maana wengine walikuwa ughaibuni wamekimbia baada ya kukumbana na moto wa ngosha. Wengine walikuwa wanatibiwa Ulaya baada ya kupigwa masasi kibao na WASIOJULIKANA chini ya uongozi wa Rais Magufuli. Wengine walikuwa magerezani kwa sababu za Kisiasa. Nikitaja kwa uchache.
Rais Samia na Serikali yake akaona si vema aongoze nchi Kwa mfumo huo. Akabatirisha takribani yote. Waliokuwa wamekimbia wakarudi nyumbani, vyama vya Siasa vikarejeshewa haki yao ya Kikatiba ya kufanya Siasa. Kifupi kukawa na maridhiano. Mambo yakaenda vizuri.
Rais Samia katika kipindi cha miaka minne, ukweli kafanya mengi na ambayo yanaonekana wazi katika sekta nyingi. Ajira, katoaa, nyongezq ya mishahara katoaaa, hospitali, Zahanati, Vituo vya Afya, vyuo, mashule, kajengaaa!! Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Pamoja na changamoto zilizopo lakini kwa muda mfupi kafanya mengi yanaonekana.
Baada ya kuona ulaini wa Rais Samia, ndipo sasa zikaingia hoja za kudai mabadiriko katika baadhi ya mambo kwa nguvu kubwa na vitisho. Tukawa tunasikia no reform no election. Hakuna mabadiriko, hakuna Uchaguzi. Mtu unajiuliza Sasa kama bila mabadiriko hakuna Uchaguzi nini kitafuata? Hii kweli kama ingeachwa iendelee kama wabeba maono hayo wanavyotaka Nini kingetokea?? Kweli yapo mambo ambayo yanatakiwa kuboreshwa zaidi ili kuwe na wigo mpana na ulio sawa wa kiushindani kwa vyama vya Siasa, lakini njia na kauli zinazotumika kudai hizo reforms kweli ziko sawa?
Ilishindikans nini kukaa chini na pande nyingine na kuzungumza? Kwa waungwana mambo yote huanza na mazungumzo. Yapo ambayo yangekubaliwa yatekelezwe ndani ya muda huu na.mengine mbele ya safari.
Kauli ya no reform, no election ikahanikizwa na kakauli kengine kepesi kutamkaka lakini kenye impact kubwa, " kama wasipofanya marekebisho, tutakinukisha kweli kweli". Haka ka kauli ndiko kaliko haribu hali ya hewa. Ikatafsirika kuwa nyuma ya haya mambo Kuna mpango mbaya.
Unajiuliza wakinukishe katika kipindi hiki? Mbona hawakufanya hivyo vipindi vilivyopita wakati mifumo ilikuwa hivi hivi? Jibu ni rahisi kwamba, walimtafsiri Rais Samia kuwa ni lege lege
anawaogopa ndio maana aliwarudisha hata waliokuwa wamekimbia moto.
kwa kujaribu jaribu huku, tukipuuza na kama Rais asiposhupaza Shingo kweli jamaa zetu watakinukisha kweli kweli. Wanaosema na kushabikia kauli zao wengine ni wakimbizi wanajificha ficha humu kama nguchiro, kikinuka haooo!! Wengine hata watoto wao na wake zao wako Ulaya. Wakikinukishs haooo Ulaya. Wengine wanalipwa ili wakinukishe Kisha haoo. Tutakaobaki ni sisi walalahoi ambao kikinuka hatuna pa kwenda.
Haya ndani ya CCM nako wamejitokeza baadhi ya watu wanataka mabadiriko yafanyike Tena ndani ya muda mfupi. Ukiangalia kwa kina unaona wazi kuwa yanayofanyika ndani na nje ya CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu ni mkakati ambao ukiruhusiwa kwa muda huu, utaleta sintiofahamu katika nchi hii ikiwa ni pamoja na kuvurugika kwa amani na utulivu. Ndio maana nimesema, Rais Samia ashupaze Shingo ili haya mambo yapite kushoto.
Ndg yangu Polepole ana haki ya kusema ayasemayo, lakini alikuwa wapi tangu Januari mpaka leo ndipo anasema mchakato ulikosewa? Ndio maana nasema yanayotokea ndani na nje ya CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu ni mkakati wa pamoja wa watu waliopanga kipi kianze wakati gani na nani aibuke na hoja zipi wakati gani!
Rais Samia endelea kushupaza Shingo, huu ni ujumbe kutoka kwa bibi yangu ambaye anasema kikinuka Hana nguvu za kukimbia.
Uchaguzi ufanyike kwa amani na utulivu. Wanao tiki wa tiki, wanaompa kura Mwalimu na Luhsgs Mpina na watiki pia.
Baada ya Uchaguzi tutakaa kupanga yaliyoko mbele yetu, safi!
Ndani ya Chama chake wapo ambao hawakutaka Samia aapishwe kuwa Rais kama Katiba inavyosema kwani yeye ndiye alikuwa Makamu wa Rais. Hawa walikuwa na hiyo mipango kwa sababu zao binafsi na pia ubaguzi wa Moja kwa moja kwamba kwa kuwa Samia ni mwanamke asingeweza kuongoza nchi. Wakijifanya hamnazo ilhali wanajua Urais ni Taasisi.
Kulikuwa na ufa mkubwa kwetu sisi na nchi nyingine hususani zile za wenzetu. Dunia ni Kijiji, lakini sisi wakati ule kutokana na mtazamo na maono ya kiuongozi ya wakati ule tulikuwa hatuundi Kijiji hicho cha Dunia Moja.
Rais Samia alianza kuturejesha tena kwenye Kijiji cha dunia Moja. Tuliona ziara nyingi za kule na huko. Hilo likapita.
Rais Samia aliona Demokrasia nchini ilikuwa na dosari maana wengine walikuwa ughaibuni wamekimbia baada ya kukumbana na moto wa ngosha. Wengine walikuwa wanatibiwa Ulaya baada ya kupigwa masasi kibao na WASIOJULIKANA chini ya uongozi wa Rais Magufuli. Wengine walikuwa magerezani kwa sababu za Kisiasa. Nikitaja kwa uchache.
Rais Samia na Serikali yake akaona si vema aongoze nchi Kwa mfumo huo. Akabatirisha takribani yote. Waliokuwa wamekimbia wakarudi nyumbani, vyama vya Siasa vikarejeshewa haki yao ya Kikatiba ya kufanya Siasa. Kifupi kukawa na maridhiano. Mambo yakaenda vizuri.
Rais Samia katika kipindi cha miaka minne, ukweli kafanya mengi na ambayo yanaonekana wazi katika sekta nyingi. Ajira, katoaa, nyongezq ya mishahara katoaaa, hospitali, Zahanati, Vituo vya Afya, vyuo, mashule, kajengaaa!! Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Pamoja na changamoto zilizopo lakini kwa muda mfupi kafanya mengi yanaonekana.
Baada ya kuona ulaini wa Rais Samia, ndipo sasa zikaingia hoja za kudai mabadiriko katika baadhi ya mambo kwa nguvu kubwa na vitisho. Tukawa tunasikia no reform no election. Hakuna mabadiriko, hakuna Uchaguzi. Mtu unajiuliza Sasa kama bila mabadiriko hakuna Uchaguzi nini kitafuata? Hii kweli kama ingeachwa iendelee kama wabeba maono hayo wanavyotaka Nini kingetokea?? Kweli yapo mambo ambayo yanatakiwa kuboreshwa zaidi ili kuwe na wigo mpana na ulio sawa wa kiushindani kwa vyama vya Siasa, lakini njia na kauli zinazotumika kudai hizo reforms kweli ziko sawa?
Ilishindikans nini kukaa chini na pande nyingine na kuzungumza? Kwa waungwana mambo yote huanza na mazungumzo. Yapo ambayo yangekubaliwa yatekelezwe ndani ya muda huu na.mengine mbele ya safari.
Kauli ya no reform, no election ikahanikizwa na kakauli kengine kepesi kutamkaka lakini kenye impact kubwa, " kama wasipofanya marekebisho, tutakinukisha kweli kweli". Haka ka kauli ndiko kaliko haribu hali ya hewa. Ikatafsirika kuwa nyuma ya haya mambo Kuna mpango mbaya.
Unajiuliza wakinukishe katika kipindi hiki? Mbona hawakufanya hivyo vipindi vilivyopita wakati mifumo ilikuwa hivi hivi? Jibu ni rahisi kwamba, walimtafsiri Rais Samia kuwa ni lege lege
anawaogopa ndio maana aliwarudisha hata waliokuwa wamekimbia moto.
kwa kujaribu jaribu huku, tukipuuza na kama Rais asiposhupaza Shingo kweli jamaa zetu watakinukisha kweli kweli. Wanaosema na kushabikia kauli zao wengine ni wakimbizi wanajificha ficha humu kama nguchiro, kikinuka haooo!! Wengine hata watoto wao na wake zao wako Ulaya. Wakikinukishs haooo Ulaya. Wengine wanalipwa ili wakinukishe Kisha haoo. Tutakaobaki ni sisi walalahoi ambao kikinuka hatuna pa kwenda.
Haya ndani ya CCM nako wamejitokeza baadhi ya watu wanataka mabadiriko yafanyike Tena ndani ya muda mfupi. Ukiangalia kwa kina unaona wazi kuwa yanayofanyika ndani na nje ya CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu ni mkakati ambao ukiruhusiwa kwa muda huu, utaleta sintiofahamu katika nchi hii ikiwa ni pamoja na kuvurugika kwa amani na utulivu. Ndio maana nimesema, Rais Samia ashupaze Shingo ili haya mambo yapite kushoto.
Ndg yangu Polepole ana haki ya kusema ayasemayo, lakini alikuwa wapi tangu Januari mpaka leo ndipo anasema mchakato ulikosewa? Ndio maana nasema yanayotokea ndani na nje ya CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu ni mkakati wa pamoja wa watu waliopanga kipi kianze wakati gani na nani aibuke na hoja zipi wakati gani!
Rais Samia endelea kushupaza Shingo, huu ni ujumbe kutoka kwa bibi yangu ambaye anasema kikinuka Hana nguvu za kukimbia.
Uchaguzi ufanyike kwa amani na utulivu. Wanao tiki wa tiki, wanaompa kura Mwalimu na Luhsgs Mpina na watiki pia.
Baada ya Uchaguzi tutakaa kupanga yaliyoko mbele yetu, safi!