Rais Samia apewe ushirikiano ili alibadilishe Taifa

Hamatan

JF-Expert Member
Nov 10, 2020
3,183
7,645
Nchi yetu imepita vipindi vingi, vyote vikiwa chini ya utawala wa TANU na baadaye CCM. Kila lililo jema na lililo baya katika Taifa letu lazima lishikamanishwe na CCM kama chama, japo tofauti zilikuwepo vipindi mbalimbali kutokana na matakwa ya Rais aliyekuwepo katika kipindi fulani.

Kuna tawala, mambo yalikuwa afadhali, kuna tawala mambo yalikuwa mabaya, na kuna utawala mambo yalikuwaabaya sana.

Mimi siyo shabiki wa Rais Samia wala mtu yeyote bali ni shabiki wa kudumu wa nchi yangu Tanzania ambayo kuna watu wanaihangaikia kila siku ili paweahali pema, lakini wapo wanaohangaika kuimaliza.

Ukilinganisha katika vipindi vyote, kipindi hiki, chinibya uongozi wa Samia, kila mmoja akienenda kwa hekima, kuna nafasi kubwa ya kujenga misingi bora mipya kwa Taifa letu katika nyanja zote, yaani kuanzia haki, demokrasia, uhuru wa maoni, na uchumi huru.

Rais Samia siyo malaika, kuna hapa na pale anaweza kutenda yasiyo matarajio ya baadhi yetu, lakini kwa ujumla, chini ya uongozi wa Rais Samia, kuna nafasi kubwa sana ya kuitengeneza Tanzania mpya, yenye mambo mengi yaliyo chanya. Jambo la muhimu tumpe moyo, tushirikiane naye (bila ya kujali tofauti za kivyama) ili kuijenga Tanzania iliyo njema kwa kila Mtanzania. Lakini tusitarajie mabadiliko yote kwa haraka na kwa wakati mmoja. Tujue kila atakalofanya kuna uoinzani mkubwa, na hasa ndani ya chama chake.

Nawasihi viongozi wa upinzani, jengeni ukaribu na ushirikiano na huyu Rais (hamzuiwi kukosoa, kwa staha), kwa lengo moja tu , ili Rais katika katika kipindi chake cha uongozi, amalize akiwa ameweka misingi imara maeneo yote. Tanzania imara ni faida kwa kila Mtanzania.
 
SAWA ipo Imani kwake ila waliomzunguka ndio sii watu wema, akianzia Kwa akina siro na kundi lake, kwani bado wanamtazamo na mambo ya awamu tangulizi, ongeza na wafuasi wao wanaoamini katika matumizi ya mabavu na dhuluma , naamini ameshaweza kuufahamu ukweli na asiwacheleweshe awanyoe haraka , Ili malengo yake mazuri kwa taifa yawezetimia.
 
Nina uhakika huyu mama atatuletea Katiba mpya.

Atuletee katina mpya kama alivyofanya Mzee Karume mwaka 2010 huko Zanzibar
JamiiForums-1916849608.jpg
JamiiForums1943670800.jpg
 
Yaani huwezi kusema eti nchi ilikuwa imefungwa blah blah wakati yeye alikuwa makamu wa rais
 
SAWA ipo Imani kwake ila waliomzunguka ndio sii watu wema, akianzia Kwa skins siro na kundi lake, kwani bado wanamtazamo na mambo ya awamu tangulizi, ongeza na wafuasi wao wanaoamini katika matumizi ya mabavu na dhuluma , naamini ameshaweza kuufahamu ukweli na asiwacheleweze awanyoe haraka , Ili malengo take mazuri kwa taifa yawezetimia.
Rais Samia anawatambua. Ndiyo maana wakati mmoha alisema kuwa kuna mzee mmoja mstaafu aliwahi kumwambia kuwa watakaopinga ni wanakijani wenzake, siyo wapinzani.

Wapinzani wanachotaka ni haki, demokrasia na uhuru wa maoni. Lakini huko ndani ya kijani kuna watu ni mashetani, hawataki kabisa mambo hayo.
 
Yaani huwezi kusema eti nchi ilikuwa imefungwa blah blah wakati yeye alikuwa makamu wa rais
Kwa katiba yetu hii mbovu, kila kitu ni Rais. Awamu ya 5, mabaya yote yaliyofanyika, au yalikuwa na maagizo ya Magufuli au yalikuwa na baraka zake. Kipindi cha Magufuli,watu walikuwa wanashindana kwa uovu dhidi ya wananchi. Ya awamu ya 5, ni ya Magufuli na genge lake, hayamhusu mwingine yoyote.
 
Hii mada ya kistaarabu sana. Inahitaji Uvumilivu umoja na mshikamano wa ki-Taifa ili tuweze kuona mabadiliko tunayoyategemea. Kitu kimoja cha kusisitiza sana ni kuwa wapinzani halisi wa Raisi Samia wala hawatoki vyama vya upinzani, yuko nao na anawafahamu maana amekuwa nao muda mrefu. Vikao vya kupiga ramli bado havijaanza au labda hajapenda kuvikumbatia sana. Tuvute subira Watanzania wenzangu, tena kwa matumaini tuu.
 
Nchi yetu imepita vipindi vingi, vyote vikiwa chini ya utawala wa TANU na baadaye CCM. Kila lililo jema na lililo baya katika Taifa letu lazima lishikamanishwe na CCM kama chama, japo tofauti zilikuwepo vipindi mbalimbali kutokana na matakwa ya Rais aliyekuwepo katika kipindi fulani.

Kuna tawala, mambo yalikuwa afadhali, kuna tawala mambo yalikuwa mabaya, na kuna utawala mambo yalikuwaabaya sana.

Mimi siyo shabiki wa Rais Samia wala mtu yeyote bali ni shabiki wa kudumu wa nchi yangu Tanzania ambayo kuna watu wanaihangaikia kila siku ili paweahali pema, lakini wapo wanaohangaika kuimaliza.

Ukilinganisha katika vipindi vyote, kipindi hiki, chinibya uongozi wa Samia, kila mmoja akienenda kwa hekima, kuna nafasi kubwa ya kujenga misingi bora mipya kwa Taifa letu katika nyanja zote, yaani kuanzia haki, demokrasia, uhuru wa maoni, na uchumi huru.

Rais Samia siyo malaika, kuna hapa na pale anaweza kutenda yasiyo matarajio ya baadhi yetu, lakini kwa ujumla, chini ya uongozi wa Rais Samia, kuna nafasi kubwa sana ya kuitengeneza Tanzania mpya, yenye mambo mengi yaliyo chanya. Jambo la muhimu tumpe moyo, tushirikiane naye (bila ya kujali tofauti za kivyama) ili kuijenga Tanzania iliyo njema kwa kila Mtanzania. Lakini tusitarajie mabadiliko yote kwa haraka na kwa wakati mmoja. Tujue kila atakalofanya kuna uoinzani mkubwa, na hasa ndani ya chama chake.

Nawasihi viongozi wa upinzani, jengeni ukaribu na ushirikiano na huyu Rais (hamzuiwi kukosoa, kwa staha), kwa lengo moja tu , ili Rais katika katika kipindi chake cha uongozi, amalize akiwa ameweka misingi imara maeneo yote. Tanzania imara ni faida kwa kila Mtanzania.
Akiwa fair kwenye uwanja wa siasa ndo utakuwa mwisho wa chama tawala.
 
Nchi yetu imepita vipindi vingi, vyote vikiwa chini ya utawala wa TANU na baadaye CCM. Kila lililo jema na lililo baya katika Taifa letu lazima lishikamanishwe na CCM kama chama, japo tofauti zilikuwepo vipindi mbalimbali kutokana na matakwa ya Rais aliyekuwepo katika kipindi fulani.

Kuna tawala, mambo yalikuwa afadhali, kuna tawala mambo yalikuwa mabaya, na kuna utawala mambo yalikuwaabaya sana.

Mimi siyo shabiki wa Rais Samia wala mtu yeyote bali ni shabiki wa kudumu wa nchi yangu Tanzania ambayo kuna watu wanaihangaikia kila siku ili paweahali pema, lakini wapo wanaohangaika kuimaliza.

Ukilinganisha katika vipindi vyote, kipindi hiki, chinibya uongozi wa Samia, kila mmoja akienenda kwa hekima, kuna nafasi kubwa ya kujenga misingi bora mipya kwa Taifa letu katika nyanja zote, yaani kuanzia haki, demokrasia, uhuru wa maoni, na uchumi huru.

Rais Samia siyo malaika, kuna hapa na pale anaweza kutenda yasiyo matarajio ya baadhi yetu, lakini kwa ujumla, chini ya uongozi wa Rais Samia, kuna nafasi kubwa sana ya kuitengeneza Tanzania mpya, yenye mambo mengi yaliyo chanya. Jambo la muhimu tumpe moyo, tushirikiane naye (bila ya kujali tofauti za kivyama) ili kuijenga Tanzania iliyo njema kwa kila Mtanzania. Lakini tusitarajie mabadiliko yote kwa haraka na kwa wakati mmoja. Tujue kila atakalofanya kuna uoinzani mkubwa, na hasa ndani ya chama chake.

Nawasihi viongozi wa upinzani, jengeni ukaribu na ushirikiano na huyu Rais (hamzuiwi kukosoa, kwa staha), kwa lengo moja tu , ili Rais katika katika kipindi chake cha uongozi, amalize akiwa ameweka misingi imara maeneo yote. Tanzania imara ni faida kwa kila Mtanzania.
Akiwa fair kwenye uwanja wa siasa ndo utakuwa ndio mwisho wa chama tawala.
 
Rais Samia anawatambua. Ndiyo maana wakati mmoha alisema kuwa kuna mzee mmoja mstaafu aliwahi kumwambia kuwa watakaopinga ni wanakijani wenzake, siyo wapinzani.

Wapinzani wanachotaka ni haki, demokrasia na uhuru wa maoni. Lakini huko ndani ya kijani kuna watu ni mashetani, hawataki kabisa mambo hayo.
Huyo alikuwa mfitini kwa 100%. Na ni kupungukiwa hekima useme eti mpinzani mkubwa wa mipango ya maendeleo ni mtoto wako au mumeo, yaani unaambiwa ni bora jirani yako kuliko familia, yaani ni bora mchepuko kwa wanaume badala ya mke wake na watoto wake.

Kwa ufupi sisi wachambusi wa siasa ndani ya Chama chetu cha CCM ni kuwa huyo mzee alisema hivyo kwa sababu wanataka 2025 huyo mzee na kundi lake and waweke mtu wao wa kugombea urais.

Yaani iko hivi ukitaka kumtawala mtu au kumteka mawazo yake mfitinishe kwanza na familia yake, yaani ni kama walivyofanya wakoloni, walihakikisha kwaza sisi watanganyika hatuelewani kwa kutugawa, na ndicho huyo mzee mwenye akili za kikoloni alichomfanyia Mama.

Mama naye bila kutumia hekima na uwezo wake wa uanauke kaingia mkenge wa kuanza kugawa chama kwa kusema eti wabaya wake wote ni CCM.

Huyo mzee sasa hivi anachokifanya anaangalia jinsi mama anavyokigawa chama na mitafaruku then ikifika 2025 watamuambia sasa wewe chama umekigawq mmno tumchague Makamba ili kuleta umoja. Kwa sababu akina huyo mzee na kundi lake watakuwa wamejijenga (kumbuka utatu mtakatifu, Makamba -nishati, nape - habari, Mwigulu-fedha) inamaana wana uhakika wa kumchafua mama kupitia nape na makamba (kupitia umeme etc) na kukusanya hela za kuhonga tiss, jeshi, polisi na wajumbe wa nec kupitia mwigulu.

Mama angejua alitakiwa aje na sura mpya with very thorough vetting aanze na timu siyoegamia upande wowote, na chamani angefanya hivyo hivyo.
 
Samia huyuhuyu ambae kila siku mnasema anadanganywa na wasaidizi wake? Kama kiongozi mkuu kila Mara unadanganywa na wasaidizi, hayo Maendeleo yatatoka wapj?
 
Watanzania tumempa ushirikiano lakini yeye ameishia na kuupa ushirikiano utawala wa kifisadi wa bwana JK.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom