DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua aliyekuwa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), CPA. Amos Gabriel Makalla kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha
Kwa mujibu wa taarifa ya leo Agosti 23, 2025 iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, CPA. Makalla anachukua nafasi ya Bw. Kenan Laban Kihongosi ambaye ameteuliwa kuwa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi.
Taarifa hiyo imebainisha kuwa uapisho wa Mkuu wa Mkoa Mteule utafanyika tarehe 26 Agosti, 2025 saa 05.00 asubuhi, Ikulu Chamwino, Dodoma.
Kwa mujibu wa taarifa ya leo Agosti 23, 2025 iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, CPA. Makalla anachukua nafasi ya Bw. Kenan Laban Kihongosi ambaye ameteuliwa kuwa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi.
Taarifa hiyo imebainisha kuwa uapisho wa Mkuu wa Mkoa Mteule utafanyika tarehe 26 Agosti, 2025 saa 05.00 asubuhi, Ikulu Chamwino, Dodoma.