Rais Mwinyi na walaji, Bashe na wakulima

Rais Mwinyi na walaji, Bashe na wakulima

USSR

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2015
Posts
11,996
Reaction score
28,298
Leo Rais wa Zanzibar ametembelea maduka ya wauzaji wa nafaka pemba na kuona bei ya vyakula havipandi na kuwa mzigo kwa mlaji

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imepiga marufuku uuzaji wa vyakula nje nchi na kuzuia upandishaji wa bei

Huku bara waziri wa biashara yuko kimya amezidiwa kete na waziri wa kilimo Hussen Bashe ambaye anataka vyakula vipande bei


USSR
Screenshot_20230212-170538.jpg
 
Bashe shikilia hapo hapo ili wadangaji, wanaobet, wacheza pool, machawa na walevi waipate freshi.
Sisi wazee wa kubet hatulii lii hovyo make odds zipo na Muhindi kunamdokoa na tunafanya mahemezi makubwa, kwa bei iliyopo
 
Bashe shikilia hapo hapo ili wadangaji, wanaobet, wacheza pool, machawa na walevi waipate freshi.
Sasa wale wazee wa kuuza skafu za mikutano watakula wapi hapo ufipa

USSR
 
Nendeni shamba mkalime acheni kulia lia mjini!! Huu ndo wakati wa kuingiza trekta na majembe shambani!!

MSije kusema hamkuambiwa msimu wa kulima unaanza lini!!
 
Zanzibar siyo wazalishaji wakubwa wa chakula kama huku bara
 
Huwezi kumridhisha mlaji kwa kumkamua mkulima
Watu wanachoangalia ni mfuko mkubwa wa bei! Mchele unauzwa 3600, halafu mnasema kama hatuwezi kununua tukalime!

Sasa kila mtu akienda kulima, nani atakayetoa huduma katika maeneo mengine? Na kama mkulima anatumia gharama kubwa kwenye kilimo, kwa nini kama serikali msitengeneze mazingira ya kumpunguzia hizo gharama, chakula kipatikane kwa bei rafiki?


Kwa nini serikali ya awamu hii mnapenda sana kutumia njia za mkato kwenye kutatua matatizo ya muda mrefu?

Mnaona mnatumia njia sahihi kweli kuwafurahisha hao wakulima, huku wafanyakazi wenye mshahara ule ule wakiendelea kutaabika?
 
Kwa sisi ambao tumewahi kutoa mazao shamba kuleta masokoni tunajua kuwa bei za vyakula ni za msimu, hupanda na kushuka.
Subirini mwezi wa tatu, wanne na kuendelea hapo kati msimu wa mavuno, kwa baadhi ya mikoa utakuwa umeanza

Halafu wakati mnlalalama hizo nafaka zinapanda bei mbona hamshangai nyama na viazi vya chipsi kushuka bei???

Viazi vya chipsi gunia ni hadi elfu 60
Nyama sasa kilo ni elfu nane
 
Nendeni shamba mkalime acheni kulia lia mjini!! Huu ndo wakati wa kuingiza trekta na majembe shambani!!

MSije kusema hamkuambiwa msimu wa kulima unaanza lini!!
Alafu muwe mnaacha ujinga,kama mnaona wakulima wakishusha bei za mazao wanakuwa wanaonewa basi ni vyema serikali iondoe ruzuku kwenye pembejeo, maana hizo ruzuku nizinatokana nakodi zetu sisi raia tunaonununua mazao bei juu.
 
Alafu muwe mnaacha ujinga,kama mnaona wakulima wakishusha bei za mazao wanakuwa wanaonewa basi ni vyema serikali iondoe ruzuku kwenye pembejeo, maana hizo ruzuku nizinatokana nakodi zetu sisi raia tunaonununua mazao bei juu.

Amsha kalio ulipo kalime wewe acha uvivu wa kipumbavu!! Utaishia kulia lia tu!! Wanaume tukashike jembe uje upatiwe bure!!
 
Bashe shikilia hapo hapo ili wadangaji, wanaobet, wacheza pool, machawa na walevi waipate freshi.
Kuna ukweli umeuweka hapo japo umeweka kwa lugja ya mzaha.

Nchi hii wazalishaji ni wengi sana. Jitu lenye nguvu kabisa, kijana, badala ta kufanya kazi, anashinda anabeti. Amemalizia pesa yote kwenye kubeti, akitoka hapo anaenda sokoni anakuta mchele sh 3,000 kilo anaingia JF kulalamika kuwa bei ni kubwa.

Ujinga mkubwa. Kama unashinda umekaa au unashinda unabeti, au unashinda unazunguka unatembeza shanga na bukta, unataka nani akazalishe ili wewe uviokote vinavyozalishwa kwa mateso, gharama na jasho, kwa bei poa? Watu wengi wakiingia kwenye uzalishaji, vyakula vitakuwa vingi, kanuni basic ya uchumi ya demand and supply itashika nafasi yake, na bei zitashuka.

Tumeifanya nchi yetu kuwa wachuuzi wa bidhaa zenye ubora hafifu za China, badala ya kuwekeza kwenye uzalishaji.
 
Kwa hiyo Bara kuna wakulima wa mazao ya chakula, halafu hakuna walaji!
Tunatakiwa kujenga mazingira ya kuhamasisha zaidi uzalishaji. Mzalishaji ana faida nyingi zaidi kuliko mlaji.

Umewahi kuwaona wachina wakija huku kutuuliza sisi walaji wa bidhaa zao tuna maoni gani? Lakini Serikali yao inazidi kuwapa mikopo zaidi watu wao ili wazidi kuzalisha, watuletee sisi walaji wa bidhaa zao duni.

Uzalishaji ndio unaoongeza pato la Taifa, na hasa uzalishaji unaolenga zaidi soko la nje ya nchi.
 
Huyu Bashe naona origin yake imezidi umuhimu wa maisha ya watanzania.

Hajali namna wananchi wanavyoteseka kwa ugumu wa maisha.

Hana uzalendo wowote.

Ingawa kuna factors nyingi zinzosababisha kupanda kwa bei ya vyakula ila kitendo cha kuruhusu wageni kwenda mpaka kwa wakulima kununua chakula moja kwa moja that is suicide.

Ni mtu mjinger tu anaweza kubaliana na jambo hili.

Hata kama huko ndiko kunaitwa kufungua nchi ila lazima tuwe na mipaka na mpaka wa kwanza ni usalama wa wananchi.
 
Kuna ukweli umeuweka hapo japo umeweka kwa lugja ya mzaha.

Nchi hii wazalishaji ni wengi sana. Jitu lenye nguvu kabisa, kijana, badala ta kufanya kazi, anashinda anabeti. Amemalizia pesa yote kwenye kubeti, akitoka hapo anaenda sokoni anakuta mchele sh 3,000 kilo anaingia JF kulalamika kuwa bei ni kubwa.

Ujinga mkubwa. Kama unashinda umekaa au unashinda unabeti, au unashinda unazunguka unatembeza shanga na bukta, unataka nani akazalishe ili wewe uviokote vinavyozalishwa kwa mateso, gharama na jasho, kwa bei poa? Watu wengi wakiingia kwenye uzalishaji, vyakula vitakuwa vingi, kanuni basic ya uchumi ya demand and supply itashika nafasi yake, na bei zitashuka.

Tumeifanya nchi yetu kuwa wachuuzi wa bidhaa zenye ubora hafifu za China, badala ya kuwekeza kwenye uzalishaji.
Kama hawa lialia watakuelewa nitag kabisa!! Mwisho wa msimu wataanza kulia lia tena badala ya kwenda kulima!!
 
Zanzibar ni nchi, kwahio Bashe akizuia vyakula visiende nje ya nchi ni pamoja na Kenya uganda na nchi ya Zanzibar, Kama ambavyo nchi ya Zanzibar imezuia ndizi kutoka nchi ya Jamhuri ya muungano
 
Back
Top Bottom