GE2025 Rais Mwinyi alipa deni lote la Zanzibar lililodaiwa na TANESCO

GE2025 Rais Mwinyi alipa deni lote la Zanzibar lililodaiwa na TANESCO

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

tonicimmobility

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
493
Reaction score
1,038
Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameupiga mwingi katika sekta ya nishati ya umeme visiwani Zanzibar na kufanikisha kulipa deni la shilingi bilioni 291, ambalo Zanzibar ilikuwa ikidaiwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Gulioni, kuhusu mafanikio ya miaka minne ya uongozi wa Rais Dk. Mwinyi, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la umeme Zanzibar (ZECO), Haji Muhamed Haji, amesema kwa miaka mingi Zanzibar ikidaiwa deni hilo lakini kwa sasa haina deni la umeme.

Soma pia: Deni la Taifa ni deni la Tanzania sio Zanzibar!.

Screenshot 2025-08-14 040840.png


Mkurugenzi huyo amesema licha ya kulipa deni hilo lakini pia serikali ya awamu ya nane chini ya uongozi wa Rais Dk. Mwinyi imefanikiwa kuunganisha umeme zaidi ya vijiji 186 kati ya hivyo asilimia 33 ni vya Pemba.

Chanzo: Nipashe digital
 
ni zaidi ya 100 million usd, thats a lot of money na kama ni kweli ilipaswa iisaadie sana tanesco, lkn najua hiyo fedha inachukuliwa na kupelekwa kwa waarabu, ni fedha nyingi sana, tena nyingi mno kwa shirika ...
 
Angesema tutaanza kujitegemea wenyewe kuanzia sasa
Kuna Umeme wa Solar na hata wa upepo (wind turbines)
Na hata wa nuclear chagua ni lake
 
Back
Top Bottom