Rais Mwinyi akilonga kuhusu uchinjaji

Rais Mwinyi akilonga kuhusu uchinjaji

Mzee Mwinyi nakupa Hongera kwa sababu unaonyesha Njia, unaonyesha njia ambayo wengine wanashindwa kuiona; Njia ambayo Mwalimu Nyerere na waasisi wengine kama kina karume wameitengeneza ili Watanzania wote waipite bila kupata misukosuko ya ajabu. Mzee Mwinyi ulipokuwa unaongea na waandishi wa habari nilikuona kama Nabii aliyebaki katika Dunia hii ili kuionyesha Tanzania nyia impasayo Kwenda. Njia inayowaelekeza Watanzania kuwa wao ni ndugu wasiopaswa kugombana kwa kuwa wanaipigania dini zao. Na Kimsingi nakukubali Mzee kwa sababu ni wewe peke yako uliyethubutu kulisemea swala la kuchinja vitoweo. Wengine wote wamekwepa ukweli ulipo. Mungu akubariki Mzee ili tuendelee kuwa nawe kwani wewe ni hazina ya nchi hii, wewe ni chemi chemi ya busara ambayo tunahitajika kuendelea kuteka maji ya busara.

Nawasilisha


Olowarukerikeri

Ni kweli Bwana Olawaru kerikeri pongezi zako kwa mzee Mwinyi ni sawa. Suala la imani ni la watu wanaohusika na imani hiyo na wasiohusika nayo hawalazimiki kuifuata wala kuwazuia wahusika kuifuata imani yao. tukisema mifugo yote ichinjwe na wenye imani fulani italazimu hao wachijnaji wawe na kazi hiyo tu kwani ng'ombe wa kuchinjwa ni wengi, kuku ni wengi, nguruwe ni wengi, bata, mbuzi,....Kwa kweli kipato watakachopata kutokana na kazi hiyo hakitatosha kukidhi mahitaji yao, watahitaji kufanya kazi zingine. Msisahau kazi ya kuchinja pia yahitaji ujasiri wa aina yake.
 
Kama ilivyo ngumu kutokana na imani yake Muislam kuweza kuingia Kanisani na kufanyia Ibada yake humo na kama ilivyo ngumu kwa Mkristo kuingia Msikitini na kuweza kufanyia ibada yake humo IKIZINGATIWA NI SUALA LA IMANI basi na kuchinja kuheshimiwe kama suala la imani kwa kila dini kati ya hizi dini mbili. Muislam kwa kuwa achinjapo sharti awe amemuelekeza mnyama yule huko KIBLA basi achinje na ALE kwa IMANI YAKE. Na Mkristo naye na ACHINJE KWA MKONO WAKE NA ALE KULINGANA NA IMANI YAKE. Mkristo kulazimishwa kula alichochinja Muislam kulingana na imani yake ni sawa na kumlazimisha Mkristo yule kuingia Msikitini kufanyia ibada za Kikristo kitu ambacho hakiwezekani, vivyo hivyo kwa Muislam.

Kama Muislam asivyoweza kumchinjia Mkristo nguruwe akala na iwe pia kwa wanyama wengine.
Tanzania bila UDINI inawezekana, tekeleza wajibu wake kulinda amani yetu na dumisha mapendo.
vipi kuhusu shule za boarding,itakuwaje?
 
Sasa nimepata mwanga kwa nini wakristo wanataka pia kuwa na haki ya kuchinja. Wazee wenye busara kama mwinyi na wengne watusaidie,je kuchinja ni ibada au utamadun au ibada?kama ni utamaduni sawa ila kama ni ibada,kwa vyovyote vile hatutamlazimisha mkiristo kuingia na kushiriki ibada za din nyingne. Pia sitegemei wakristo waanze kuwaza kwa mtindo huo eti kwa kuwa jumapili hakuna kazi wafanyakazi wote lazma waende makanisani,hapana,kila mtu afanye kulingana na imani yake. Angalizo...tukubaliane katika ma sherehe makubwa yanayohusisha imani zote,apo tuweke utaratibu usiokwaza upande wowote.
 
Sasa nimepata mwanga kwa nini wakristo wanataka pia kuwa na haki ya kuchinja. Wazee wenye busara kama mwinyi na wengne watusaidie,je kuchinja ni ibada au utamadun au ibada?kama ni utamaduni sawa ila kama ni ibada,kwa vyovyote vile hatutamlazimisha mkiristo kuingia na kushiriki ibada za din nyingne. Pia sitegemei wakristo waanze kuwaza kwa mtindo huo eti kwa kuwa jumapili hakuna kazi wafanyakazi wote lazma waende makanisani,hapana,kila mtu afanye kulingana na imani yake. Angalizo...tukubaliane katika ma sherehe makubwa yanayohusisha imani zote,apo tuweke utaratibu usiokwaza upande wowote.

Sherehe sio sehemu ya maisha ya mwanadamu. Kila sherehe ina muandaaji wake.

Unafiki ni sehemu ya UPUMBAVU. Mtu hawezi kuniambia hawezi kula nyama niliyochinja sababu ya dini yake at the same time anaweza kunywa BIERE nilizonunua na dini hiyo hiyo inamkataza.

Wao waendelee na maandazi, ubani na chai na sisi tutaendelea na pilau, bia na ndafu. Unataka njoo, hutaki kalisha masaburi home.
 
mbona nguruwe anapigwa nyundo wewe unaseme nini au emekariri acha kukariri mambo jadili kwa busara
Huyu ameonyesha uthubutu ingawa amechanganya mambo. Suala hili bado ni gumu. Hakuna dini inayoruhusu kula vibudu, mnyama ni lazima achinjwe.
 
Back
Top Bottom