Rais Mugabe ahusishwa kwenye mafaili ya Jeffrey Epstein

Rais Mugabe ahusishwa kwenye mafaili ya Jeffrey Epstein

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
844
Reaction score
1,608
Rais wa zamani wa Zimbabwe, hayati Robert Mugabe ametajwa katika kundi jipya la faili za Jeffrey Epstein zilizotolewa Marekani.

Katika mawasiliano ya barua pepe ya mwak 2015 na mjasiriamali wa Kijapani Joi Ito, Epstein alipendekeza waende kwa Rais Mugabe wakati huo ili kuipa Zimbabwe sarafu mpya baada ya dola ya ndani kuporomoka kutokana na mfumuko wa bei uliokithiri nchini Zimbabwe.

Aidha, nyaraka za FBI za mwaka 2017 pia zilitoa ushahidi usiothibitishwa kutoka kwa chanzo cha siri kikidai kuwa Epstein alikuwa meneja wa utajiri wa Rais wa Rais wa Urusi Vladimir Putin na alitoa huduma hiyo kwa Mugabe.

Hata hivyo, wataalamu wanasema kutajwa kwenye faili hizo hakumaanishi kufanya kosa lolote, na hadi sasa hakuna ushahidi wa moja kwa moja wa makosa dhidi ya Mugabe.
 
kwenye vyombo vya habari wanawaita babylo nje ya pazia wanakunywa nao
 
Sasa Mugabe katajwa na watu tu hata hawajui. Wewe jambazi anayekufahamu kama mwalimu au muuza duka akikutaja kwenye mazungumzo wakati anakunywa kahawa, tiyari unakuwa jambazi?
 
Back
Top Bottom