Rais Mstaafu Kikwete aliwahi kulalamika kutengwa na majirani zetu, siyo wa kuwaamini sana

Tuwe na staha bandugu
Tz ni yetu sote ushauri ni jambo jema kwa faida ya Taifa
Majirani zetu sio wa kuwaamini kiviiilee
Mama ashauriwe vyema taratibu na hawa watu
Huku kukurupuka 'italigharimu Taifa'
Kenya watakuja kununua mbao korosho kahawa mahindi Maparachichi kwa bei ndogo wakauze nje waseme ni mali ya Kenya

Serikali iwaamuru waje wajenge viwanda ndani ya Tanzania na kutumia airport na Bandari zetu kuimport na export.
Mahindi yasafirishwe kupitia bandari ya Dar kwenda Mombasa kuua panya road
Maparachichi wajenge viwanda kunakozalisha zao hili na kusafirisha nje

Vyote iwe ni Mali ya Tz sio Kenya
Hapo tutakwenda sawa si vinginevyo
 
Kwani uhuru ameomba kitu toka kwetu? Uhuru hajawahi kanyaga Chatto mzee ni Raila
Ni kweli siasa ikiingia kwenye ubongo, ubongo unakuwa hauna kazi tena?
Yaani kabisa unabisha Kenyatta hajawahi kwe da chato? Kenyatta na Magufuli walikuwa marafiki, achana na hiyo misuguano ya kimaslahi uliyokuwa unaiona.
Haya habari hii hapa, ukitaka naa video niambie maana alilala kabisa huko chato asubuhi akapewa tausi akasepa
Screenshot_20210505-163246_1.jpg
 
mkuu unachokisema ni sawa lakini a story has always 2 sides you have jst narated one side of the story,kwaiyo ni swala la kuketi na kuweka mambo sawa bila uzito kuegemea pande moja.
 
Mimi binafsi Kuna mengi ambayo nimefurahi hasa kwenye ziara ya Mama huko Kenya, ikiwemo kuwauzia gesi maana tutapata faida kubwa.

Kikwete anahesabika moja ya maraisi wapole,wenye busara na diplomasia ya Hali ya juu. Lakini pamoja na yote hayo Mh. Kikwete aliwahi kupata shuruba ya Hawa majirani hasa Kenya tu kwa sababu ya kuwakatalia baadhi ya mambo yao waliokuwa wakihitaji.

Kikwete kwa haiba aliyonayo na alivyokuwa akisemwa kuwa anachekacheka basi isingekuwa ngumu kwake kukataa hayo mambo, Ila hadi anadiriki kukataa tafsiri yake Kuna vitu alivyiona.

Mama Samia Mimi ni mfuasi wako, hivyo pamoja na Huo ujirani mwema Kuna vitu inabidi kuvikataa katakata, Wala ukwepeshe.

Kwenye kikao wanakubaliana wakatae kusani ila nyuma ya pazia Kenya anaenda kusaini, mfano ni: EPA
Ilifikia kipindi wakawa wanafanya meetings za EAC bila hata kumjulisha Mh. Kikwete.

Hivyo Mama nakuomba usifurahie Sana maneno yao matamu bali Pima maslahi ya watanzania.

Chini ni habari ya kipindi hicho 2013 Kikwete akilalamikia Hawa majirani zetu.

Zaidi soma > Hotuba ya Rais Kikwete, Bungeni Dodoma - Novemba 07, 2013

Tukumbuke pia kuvunjika kwa Jumuia ya Afrika, 1977, hadi Rubani wa Tz kutorosha ndege moja na Shirika la Reli kugawanyika.

Mwaka 1977, Jumuiya ya Afrika Mashariki ilivunjika kutokana na Kenya kuomba viti zaidi katika vyombo vya kufanya maamuzi, kutoelewana kati ya nchi wanachama, na mifumo tofauti ya kiuchumi kati ya nchi, hasa kati ya Tanzania na Kenya.

Hivyo, Serikali ya Awamu ya Sita isipokuwa makini, kujitegemea tulikoanza kuonja tutarudi kule kule kuwa tegemezi wa bidhaa za viwanda vya Kenya na tukabaki kuwauzia malighafi. Iwapo viwanda vyetu vitasimama kwa sababu ya ushindani, ndoto za ajira 8m zitabaki kuwa ndoto.
 
Ni kweli siasa ikiingia kwenye ubongo, ubongo unakuwa hauna kazi tena?
Yaani kabisa unabisha Kenyatta hajawahi kwe da chato? Kenyatta na Magufuli walikuwa marafiki, achana na hiyo misuguano ya kimaslahi uliyokuwa unaiona.
Haya habari hii hapa, ukitaka naa video niambie maana alilala kabisa huko chato asubuhi akapewa tausi akasepa
View attachment 1774368
Photoshop mkuu
 
Hata hiyo gesi ni mauzauza kwn tulishaambiwa gesi ni ya mabeberu..labda kama mnazungumzia gesi tofauti
 
mkuu unachokisema ni sawa lakini a story has always 2 sides you have jst narated one side of the story,kwaiyo ni swala la kuketi na kuweka mambo sawa bila uzito kuegemea pande moja.
Kabisa, wao wameskia side moja wakaidandia kama dala dala. Na pia mbona hamjiulizi kwa nini hizi nchi tatu ziliamua kufanya kazi pamoja na kuitenga 🇹🇿.

Kufikiria ni bure lakini duuh
 
Back
Top Bottom