Wadau napenda kutoa assessment yangu juu ya nani anaweza kupiga vita ufisadi kati ya Mheshimiwa Rais John Magufuli na Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa.
Nikianza kwa Rais Magufuli toka alipokuwa kuwa Waziri katika serikali ya awamu ya tatu alionyesha wazi ni mtu anayechukia ufisadi, yeye ndie aliyesimamia zoezi la magari ya miradi yote ya serikali kusajiliwa DFP ili haya magari yatambulike kama ni ya serikali na yatumike kwa kazi zilizopangiwa. Kuhusu uuzaji wa nyumba za serikali Mheshimiwa Magufuli hawezi kulaumiwa kwani ulikuwa uamuzi wa uongozi wa serikali ya awamu ya tatu.
Wakati wa serikali ya awamu ya pili Rais Magufuli alianza kwa kuwa waziri wa ardhi na kwa muda alipokuwa waziri wa ardhi alifanya kazi kubwa sana katika kutatua matatizo ya ardhi na alifanya kazi hiyo kwa ufanisi mkubwa sana, Rais Magufuli alihamishiwa wizara ya uvuvi katika wizara hiyo kama waziri alifanya kazi nzuri mpaka wavuvi waliokuwa wakivua samaki katika pwani ya Tanzania walitiwa mbaroni, uvuvi haramu katika ziwa Victoria ulipungua sana kwani Mheshimiwa Magufuli kuna wakati akiwa kama waziri wa uvuvi yeye mwenyewe alishiriki katika zoezi la doria. Baada ya hapo Mhe. Magufuli alirudishwa kwenye wizara ujenzi ili kusimamia wizara hiyo na alifanya kazi hiyo vizuri sana.
Rekodi inaonyesha Mhe.Magufuli hana doa hata moja inayomhusisha na masuala ya kifisadi kama mnakukumbu wakati wa mkutano wa bunge la bajeti wizara aliyokuwa akisimamia bajeti yake ilikuwa ikiungwa mkono mpaka na vyama vya upinzani na ilikuwa ikipitishwa bila upinzani wowote. Mheshimiwa Magufuli alipoamua kugombea nafasi ya Urais alianza kufanya kampeni zake bila kutoa rushwa na kutokuwa na wapambe na kwa muda wa mwaka mmoja kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonyesha dhamira yake ni jinsi gani anavyouchukia ufisadi.
Mwaka 1995 Edward Lowassa alipoamua kugombea urais alipata kikwazo kutoka kwa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere ambaye alipinga vikali kwa Edward Lowassa kuwa mgombea urais kupitia CCM kwasababu alizozijua Mwalimu Nyerere baada ya kupokea taarifa kutoka Idara ya usalama.
Akiwa waziri katika serikali awamu ya tatu Mhe. Edward Lowassa alifanya kazi vizuri kama waziri. Wakati wa serikali ya awamu ya nne Mhe. Lowassa aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu lakini alitumikia ofisi hiyo kwa muda mfupi mpaka aliposhindikizwa na bunge kujiuzulu kwasababu ya kashfa ya Richmond. Edward Lowassa alihusishwa na kashfa nyingine kama ya mktaba mbovu wa jengo la UVCCM.
Baada Edward Lowassa kujiuzulu kama waziri mkuu kutumia utajiri alionao alianza kampeni ya kutafuta nafasi ya kuwa mgombea urais 2015 kwa kuhakikisha anawafadhili wagombea katika uongozi ndani ya CCM ili waje wamuunge mkono katika mkutano mkuu wakati wa mchakato wa mgombea Urais wa 2015 kupitia CCM.
Baada ya jina la Edward Lowassa kuondolewa katika nafasi ya kugombea urais kupitia CCM 2015, aliamua kuhamia Chadema na Edward Lowassa alichaguliwa kuwa mgombea wa Chadema bila taratibu za kidemokrasia kuchukua mkondo wake.
Edward Lowassa anamiliki hisa na makampuni mengi kwa mgongano wa kimaslahi hawezi kuwa jemadari mzuri katika vita dhidi ya ufisadi.