Nafikiri kabla ya kuibinafshisha, serekali iwe ina NIA ya dhati ya kuondoa matatizo ya umeme nchini na UELEWA wa chanzo/vyanzo vya huduma MBAYA za umeme kutoka TANESCO.
Baada ya kuwa na uelewa huo, ndio wajiridhishe kama jawabu la kuviondoa/kuvidhibiti vyanzo hivi ni kueweka TANESCO chini ya umiliki binafsi au la.
Je matatizo ya TANESCO yapo kwenye uzalishaji, usambazaji (transmission), ugawaji, rasilimali watu au vyote?
Nadhani moja ya changamoto la TANESCO katika ugawaji wa umeme ni MIPANGO MIJI mibovu. Hii huondoa mantiki na hitaji la TANESCO kuweka miundombinu ya kudumu katika ugawaji wa umeme, kwa mfano kupitisha umeme chini ya ardhi, kuweka nguzo za zege/chuma, kuweka transformer kwenye vyumba maalumu, n.k. Uwekaji wa miundombinu ya ya kudumu ya ugawaji wa umeme utaipunguzia sana TANESCO gharama za matengenezo na hasara itokanayo na ukosefu wa huduma, wakati huohuo ikiwapa wananchi huduma bora.
Siwezi kuelezea vya kutosha UMUHIMU wa kuwa na miji/vitongoji vilivyopangwa vyema.
Ndio, huduma ya umeme wa TANESCO ni MBAYA sana! Lakini je chanzo chake ni kipi? Na tunakitatua vipi?