Rais Magufuli siasa si uadui, Una kifua kweli?

Brigedia Chan-ocha

JF-Expert Member
Mar 7, 2014
1,353
2,846
Nimeshtushwa sana tena sana na taarifa kwamba, Rais Magufuli amewaonya wabunge wake wa CCM wanaogawa Muda wao kwa Wabunge wa Upinzani.

Pia, Rais amemwagiza baba ya mbunge mmoja wa kike amuonye mwanaye kwa kitendo chake cha kuvujisha siri za Chama kwa huyo mbunge wa Upinzani, kwanza, mwanzoni taarifa zilianza kusambaa kwamba, Halima Bulembo ndiye anayetuhumiwa kuvujisha siri za CCM kwa mbunge huyo wa Upinzani, kwamba, Halima ana mahusiano na Mbunge huyo na kwamba wamepanga kuoana na kwamba ana mimba yake, taarifa zikasema, baba yake amekorofishana na mwanaye juu ya hatua hiyo na kwamba Rais naye amechukizwa sana na kitendo cha mbunge huyo kuwa mahusiano na mbunge wa Upinzani, sasa Taarifa rasmi zimemnukuu Rais Jana akiwa na kikao na Wabunge wake wa CCM akimuonya Mbunge huyo vikali na kumwamuru Baba ya mbunge huyo amuonye mwanae...

Pia, Rais amenukuliwa akichukizwa na kitendo cha wabunge wa CCM waliotaka kwenda kumuona Lema Gerezani, nimeshangaa sana.

Rais unajenga nchi ya namna gani? yaani hujui kuwa Siasa si uadui? hulka ya watanzania ni upendo, sasa sijui unataka watanzania tusipendane?

Naamini sasa, kwa kuwa umeanza hivyo, muda si mrefu utapiga marufuku wana CCM kuhudhuria misiba ya wanachama wa upinzani.

Muda si mrefu, utachukizwa na kupiga marufuku wana CCM kutembea barabara moja au kuchota maji au kusali pamoja na wale wa upinzani, kumbuka Mh. Rais, Mwalimu Nyerere alisema, "Ukila nyama ya mtu huwezi kuacha" kwa kuwa umeanza hivo, sasa ndivyo utakavyoenenda hivo hivo, nchi ikija kushtuka, tayari tutakuwa tumishagawanyika vipande vipande.

Nawaomba sana Viongozi wa Dini mkemee hii tabia ya Mh. Rais kuanza kuonyesha dalili ya kuwagawa watanzania, watanzania wana maadili yao ambayo ni ya pekee, sasa anapotokea mtu kuanza kuyamomonyoa ni lazima akemewe sana, mbona wakati wa JK. mlikuwa mnakemea? awamu hii mmekuwaje enyi viongozi wa dini? nini kimewapata?

Ni lazima Rais aambiwe ukweli na bayana kuwa awe mvumilivu, yaan awe na kifua kipana cha kupokea au kusikia jambo na mengine ayanyamazie, si kila kitu ni cha kusema sema hadharani, pia, Rais aambiwe, kabla ya kusema jambo lazima apime athari zake kwa jamii au nchi.

Mwisho: Nawaomba Ndugu zangu watanzania, Tuendelee kuwa wamoja, tupendane na tuendelee na utamaduni wetu ambao umekuwepo tangu Enzi na Enzi, huyu ni Rais tu, kesho hayupo madarakani, kwa hiyo ni lazima tujitambue, mimi sioni tofauti kati ya CCM na Chadema au CUF kwa muktadha wa WANACHAMA, maana wote tu watanzania, tofauti ni mitizamo tu na Imani.

Nawapenda sana Watanzania.
 
Nawaomba sana Viongozi wa Dini mkemee hii tabia ya Mh. Rais kuanza kuonyesha dalili ya kuwagawa watanzania, watanzania wana maadili yao ambayo ni ya pekee, sasa anapotokea mtu kuanza kuyamomonyoa ni lazima akemewe sana, mbona wakati wa JK. mlikuwa mnakemea? awamu hii mmekuwaje enyi viongozi wa dini? nini kimewapata?

(THUBUTU)
 
Kwani nani kasema ni ugomvi

Mkuu hali ni mbaya, umeyapata aliyoyasema kwenye kikao chake na wabunge wa CCM?

Hivi wewe ukimtembelea mwanachama wa Upinzani hospitalini kumjulia hali, nini kitakupata? kuna tatizo gani? sijui unanielewa concern yangu hapa?

au wewe ukiwa na mahusiano na mwanachama wa Upinzani kuna tatizo lolote? ujue hayo aliyoongea Rais hayaishii huko, yatakuja hadi huku tulipo, fikiria Zaidi nje ya box
 
Heee hata wewe ccm mwenzake umegundua huyu raisi ana tatizo, amelewa madaraka, ni limbukeni huyu

Nimeshutushwa sana mkuu, sasa Maadili ya watanzania yanaanza kupotea, watanzania hatujazoea kuishi kwa namna Rais Magufuli anavyotaka watu wawe, yaani tusiwe na mahusiano na wanachama wa vyama vingine, au tusitembeleane katika shida na raha, hii si sahihi kabisa napinga kabisa
 
Daaah hii hatar imenikumbusha hii...
"Nitakua rais wa watz wote, wanaccm, wanachadema, wanacuf na hata wasio na chama" -mgombea urais cccm 2015

Sasa Naona Rais anayotamka na kutenda ni tofauti, na tukinyamazia hili, shauri yetu, namba hata Gwajima issue ya Makonda aache kwanza, akemee hili kwanza ndo arudi huko kwa makonda.

Viongozi wote wa DINI Waungane pamoja kukemea sana huu mwenendo wa Rais.
 
Akili zinaanza kuwarudia, kwa dhambi CCM iliyofanya 2015 huyu mtu kaja kama malipo ya laana!! Tutasikia na kuona mengi.... Muda utatuambia.

Mkuu ni hatari sana, na kibaya Zaidi, Watanzania hatupo hivyo kabisa, yaan hatujawahi kuishi kwa namna ambayo Rais anataka tuishi, halafu sijui Magufuli anauchukuliaje huo Urais? namshangaa sana huyu jamaa.
 
Napata mashaka sana na roho mbaya ya huyu jamaa. Watanzania hatunaga Roho za hivi mbona. Mange hebu fanya uchunguzi huyu anaweza kuwa mhutu au mtusi

Kabisa Mkuu, Watanzania jinsi tulivyo na tunavyojuana, hakika hatupo kama ambavyo magufuli anataka tuwe au tuishi, Viongozi wa Dini huu ulikuwa ni wakati wao kupaza sauti na kukemea hizi mbegu anazopanda Rais.
 
Sasa Naona Rais anayotamka na kutenda ni tofauti, na tukinyamazia hili, shauri yetu, namba hata Gwajima issue ya Makonda aache kwanza, akemee hili kwanza ndo arudi huko kwa makonda.

Viongozi wote wa DINI Waungane pamoja kukemea sana huu mwenendo wa Rais.
Gwajima hawezi,hii ni shu yetu sote,si unaona Gwajima hata akimponda bashite anawaomba waumini wampigie makofi mtukufu ingawa deep in his heart atakuwa anamsanifu tu
 
Serikali ya magufuli, ccm ameishaichukua nayo sasa ni ya magufuli, mahakama alishaichukua nayo in ya magufuli, hatimae kuanzia Jana kawaambia kuwa na bunge lazima liwe la magufuli, kwa sasa ukitaka hata kwenda kukojoa lazima uruhusiwe na magufuli.
 
hata wale wanaobembeleza mtu wale tigo huwa wanaanza kuingiza kidogokidogo mpaka mtu anazoea sasa watanzania tunaanza kuzoeshwa very soon internet itafungwa hakyamungu na siku katiba inabadilishwa hakuna mtu kutoka madarakani sijui tutafanya nini,as a nation tuko kwenye hali ya kusikitisha sana.

Mkuu ni heri afanye yote lakini atuache sisi watanzania tuishi kama alivyotukuta, kuna madhara makubwa sana RAIS kuanza kupenyeza haya mambo ya mgawanyiko nchini, sijui tutafanyaje.
 
Back
Top Bottom