Mbunge wa CCM Vwawa ashauri Afrika iungane na kuwa taifa moja ili kupunguza umasikini wa Watanzania

Mindyou

JF-Expert Member
Sep 2, 2024
2,081
5,507
Mbunge wa Vwawa (CCM), Japhet Hasunga, amemsifu Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayofanya katika kuleta maendeleo nchini, akisisitiza kuwa ni kiongozi shupavu anayehakikisha Tanzania inapiga hatua.

Akizungumza bungeni wakati wa kuchangia hoja, Hasunga alipendekeza kuwa Afrika iungane na kuwa taifa moja ili kuimarisha uchumi na kupunguza umasikini.

"Kama Afrika ikiungana na jinsi ambavyo Rais Samia anasimamia upatikanaji wa nishati safi, itasaidia sana kupunguza umasikini wa Watanzania," alisema Hasunga.

Mbunge huyo alisisitiza kuwa upatikanaji wa umeme na nishati safi utasaidia kuinua uchumi kwa kuongeza fursa za ajira na kuboresha maisha ya wananchi.

Mbunge.png

Source: Nipashe
 
Kwa viongozi gani?? Kwa watu gani?? Wazungu watatutawala hadi wakati wa unyakuo. Nafikiri ngozi hii ina ka laana.
 
Sijui amekula maharage ya wapi huyu mpiga makofi na praise team ya mgombea aliyeizidi maarifa kamati kuu.
Tumeungana na Zanzibar miaka 60+ sasa na Watanzania bado choka mbaya.
Nimecheka sana ila kwa zenji ule ni mkoa wa Tanganyika tuna haki zetu pale .
 
Mbunge wa Vwawa (CCM), Japhet Hasunga, amemsifu Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayofanya katika kuleta maendeleo nchini, akisisitiza kuwa ni kiongozi shupavu anayehakikisha Tanzania inapiga hatua.

Akizungumza bungeni wakati wa kuchangia hoja, Hasunga alipendekeza kuwa Afrika iungane na kuwa taifa moja ili kuimarisha uchumi na kupunguza umasikini.

"Kama Afrika ikiungana na jinsi ambavyo Rais Samia anasimamia upatikanaji wa nishati safi, itasaidia sana kupunguza umasikini wa Watanzania," alisema Hasunga.

Mbunge huyo alisisitiza kuwa upatikanaji wa umeme na nishati safi utasaidia kuinua uchumi kwa kuongeza fursa za ajira na kuboresha maisha ya wananchi.


Source: Nipashe
HUYU NI ZERO BRAIN 😀
 
Back
Top Bottom