Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 2,081
- 5,507
Mbunge wa Vwawa (CCM), Japhet Hasunga, amemsifu Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayofanya katika kuleta maendeleo nchini, akisisitiza kuwa ni kiongozi shupavu anayehakikisha Tanzania inapiga hatua.
Akizungumza bungeni wakati wa kuchangia hoja, Hasunga alipendekeza kuwa Afrika iungane na kuwa taifa moja ili kuimarisha uchumi na kupunguza umasikini.
"Kama Afrika ikiungana na jinsi ambavyo Rais Samia anasimamia upatikanaji wa nishati safi, itasaidia sana kupunguza umasikini wa Watanzania," alisema Hasunga.
Mbunge huyo alisisitiza kuwa upatikanaji wa umeme na nishati safi utasaidia kuinua uchumi kwa kuongeza fursa za ajira na kuboresha maisha ya wananchi.
Source: Nipashe
Akizungumza bungeni wakati wa kuchangia hoja, Hasunga alipendekeza kuwa Afrika iungane na kuwa taifa moja ili kuimarisha uchumi na kupunguza umasikini.
"Kama Afrika ikiungana na jinsi ambavyo Rais Samia anasimamia upatikanaji wa nishati safi, itasaidia sana kupunguza umasikini wa Watanzania," alisema Hasunga.
Mbunge huyo alisisitiza kuwa upatikanaji wa umeme na nishati safi utasaidia kuinua uchumi kwa kuongeza fursa za ajira na kuboresha maisha ya wananchi.
Source: Nipashe