Nsubhi
Senior Member
- Jan 27, 2015
- 159
- 51
Wakati kikao cha raisi na wadau wa madini kikiendelea. Napenda kumpongeza raii kwa juhudi anazozifanya ili kuona Tanzania ya viwanda, lakini kuna watendaji wake wanamwangusa aidha kwa makusudi au kwa kutojua wanachokifanya.
Nimewahi kusikia viongozi wakisema, eti wafanyakazi wa sector binafsi ya madini wakilipwa mshahara mkubwa watakua walevi, wengine wakasema itasababisha wafanyakazi wa serikali kuacha kazi na kukimbilia migodini nk.
Kuna maswali ya kujiuliza, hivi migodini nafasi za kazi hazihesabiki? Au wanaruhusu walevi kuingia kazini wamelewa? Majibu ni hapana. Viongozi wenye mawazo kama hayo niliyo yataja hapo juu ni wabinafsi na wala rushwa wazuri tu. Ndiyo maana hawataki taifalao lineeneke na wawekezaji.
Hoja ya msingi hapa ni kwamba serikali ingeweza kukusanya mapato makubwa sana zaidi ya sasa kutokana tu PAY. Kama serikali ingefanya yafuatayo:-
1.Kupandisha kima cha chini kwenye sector ya madini angarau kikawa 2,500,000Tshs. Serikali ingekusanya kodi kubwa sana kwa kila mtanzania anaefanya kazi mgodini. Na ndiyo maana wafanyakazi wanapoona uzalishaji ni mkubwa, wakiomba kuongezewa mshahara, utasikia mgodi mnasema oooh kwanza tulisha vuka kima cha chini. Na wanaenda mbali zaidi kwamba eti sera ndivyo inavyowaelekeza.
2. Kila mfanyakazi anaefanya kazi mgodini angepata TIN ingejulikana kila mtanzania anaefanya kazi mgodini anachangia kiasi gani, tofauti na sasa inaonekana migodi ndiyo inayochangia hata kile anachokatwa mfanyakazi PAY, kwa sababu tu PAYya mfanyakazi inapitia kwenye TIN ya mgodi. Hivyo ongefanyika hivi hata mwekezaji angejulikana analipa kiasi gani nasiyo kujificha kwa wafanyakazi. Utasikia ACACIA katipa kodi 36Billion kumbe 30Billion ni PAY ya wafanyakazi yeye kalipa kiduchu.
Ukifata haya mheshimiwa raisi nakuhakikishia tutafika mbali. Ushawahi kujiuliza kwenye nchi wanazotoka hawa wawekezaji wakubwa wa madini kwanini hawalipi mishahara kama hii ya kwetu? Kwamba watanzania hawajui kutumia hela?
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimewahi kusikia viongozi wakisema, eti wafanyakazi wa sector binafsi ya madini wakilipwa mshahara mkubwa watakua walevi, wengine wakasema itasababisha wafanyakazi wa serikali kuacha kazi na kukimbilia migodini nk.
Kuna maswali ya kujiuliza, hivi migodini nafasi za kazi hazihesabiki? Au wanaruhusu walevi kuingia kazini wamelewa? Majibu ni hapana. Viongozi wenye mawazo kama hayo niliyo yataja hapo juu ni wabinafsi na wala rushwa wazuri tu. Ndiyo maana hawataki taifalao lineeneke na wawekezaji.
Hoja ya msingi hapa ni kwamba serikali ingeweza kukusanya mapato makubwa sana zaidi ya sasa kutokana tu PAY. Kama serikali ingefanya yafuatayo:-
1.Kupandisha kima cha chini kwenye sector ya madini angarau kikawa 2,500,000Tshs. Serikali ingekusanya kodi kubwa sana kwa kila mtanzania anaefanya kazi mgodini. Na ndiyo maana wafanyakazi wanapoona uzalishaji ni mkubwa, wakiomba kuongezewa mshahara, utasikia mgodi mnasema oooh kwanza tulisha vuka kima cha chini. Na wanaenda mbali zaidi kwamba eti sera ndivyo inavyowaelekeza.
2. Kila mfanyakazi anaefanya kazi mgodini angepata TIN ingejulikana kila mtanzania anaefanya kazi mgodini anachangia kiasi gani, tofauti na sasa inaonekana migodi ndiyo inayochangia hata kile anachokatwa mfanyakazi PAY, kwa sababu tu PAYya mfanyakazi inapitia kwenye TIN ya mgodi. Hivyo ongefanyika hivi hata mwekezaji angejulikana analipa kiasi gani nasiyo kujificha kwa wafanyakazi. Utasikia ACACIA katipa kodi 36Billion kumbe 30Billion ni PAY ya wafanyakazi yeye kalipa kiduchu.
Ukifata haya mheshimiwa raisi nakuhakikishia tutafika mbali. Ushawahi kujiuliza kwenye nchi wanazotoka hawa wawekezaji wakubwa wa madini kwanini hawalipi mishahara kama hii ya kwetu? Kwamba watanzania hawajui kutumia hela?
Sent using Jamii Forums mobile app