Rais Magufuli nisamehe,nakushauri kwa mara ya mwisho. Tafadhali shaurika!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Kila ugonjwa una tiba au kinga au vyote. Rais wangu na Mwenyekiti wangu wa CCM Taifa,Dr. J. P. J. Magufuli,tafadhali niwie radhi nikushauri kwa mara ya mwisho. Shaurika.

Mimi sikuwahi kuwa Rais. Mwenzangu ndiwe Rais. Lakini,mimi nimekuwa mwanasiasa mwandamizi na hata mtumishi mwandamizi wa idara nyetinyeti Serikalini kuliko wewe. Najua jambo moja kubwa:mgawanyo wa majukumu na kuwa ukomo wa jukumu fulani

Kiserikali,kuna mambo ya Rais;ya Makamu wa Rais;ya Waziri Mkuu;ya Waziri na kadhalika na kadhalika. Kila kiongozi Serikalini ana majukumu na mipaka yake. Ndiyo kusema,si kila jambo lamhusu Rais. Si kila jambo halimhusu Rais. Si mambo yote yanayomhusu Rais kuyashughulikia.

Mhe. Rais,wewe kuandikwaandikwa kwenye media kila uchao si jambo jema sana. Kuandikwa kwako kwa kila litokealo Serikalini ni mchoro wa kutia kihoro. Mchoro huoneshao kuwa unafanya au kusemea kila jambo-hata yale ya Mawaziri,Makatibu Wakuu wa Wizara na kuendelea. Hoja ya jeshi la mtu mmoja huanzia hapo. Haivutii

Mhe. Rais,nakushauri uwaruhusu wasaidizi na wateule wako wafanye kazi zao ulizowaamini wazifanye. Wakizifanya zao,kazi zako zitapungua na kuonekana vyema. Yapo mambo ya kutendwa au kuzungumziwa na wasaidizi au wateule wako. Hata Wasemaji wa Wizara wangetosha na kutisha!

Ushauri wangu unalenga kukupunguzia kazi. Tafadhali epuka kuona kila jambo Serikalini ni lako. Ikifika hapo,yote utayatenda wewe. Wengine watatumbua mishahara ya bure. Tena,utaandikwa na kusemwa sana. Utafurahi na kukereka sana. Utaona na kusikia sana. Utafanya kazi sana. Utachoka sana. Utasema sana. Utatutisha sana!

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Kila ugonjwa una tiba au kinga au vyote. Rais wangu na Mwenyekiti wangu wa CCM Taifa,Dr. J. P. J. Magufuli,tafadhali niwie radhi nikushauri kwa mara ya mwisho. Shaurika.

Mimi sikuwahi kuwa Rais. Mwenzangu ndiwe Rais. Lakini,mimi nimekuwa mwanasiasa mwandamizi na hata mtumishi mwandamizi wa idara nyetinyeti Serikalini kuliko wewe. Najua jambo moja kubwa:mgawanyo wa majukumu na kuwa ukomo wa jukumu fulani

Kiserikali,kuna mambo ya Rais;ya Makamu wa Rais;ya Waziri Mkuu;ya Waziri na kadhalika na kadhalika. Kila kiongozi Serikalini ana majukumu na mipaka yake. Ndiyo kusema,si kila jambo lamhusu Rais. Si kila jambo halimhusu Rais. Si mambo yote yanayomhusu Rais kuyashughulikia.

Mhe. Rais,wewe kuandikwaandikwa kwenye media kila uchao si jambo jema sana. Kuandikwa kwako kwa kila litokealo Serikalini ni mchoro wa kutia kihoro. Mchoro huoneshao kuwa unafanya au kusemea kila jambo-hata yale ya Mawaziri,Makatibu Wakuu wa Wizara na kuendelea. Hoja ya jeshi la mtu mmoja huanzia hapo. Haivutii

Mhe. Rais,nakushauri uwaruhusu wasaidizi na wateule wako wafanye kazi zao ulizowaamini wazifanye. Wakizifanya zao,kazi zako zitapungua na kuonekana vyema. Yapo mambo ya kutendwa au kuzungumziwa na wasaidizi au wateule wako. Hata Wasemaji wa Wizara wangetosha na kutisha!

Ushauri wangu unalenga kukupunguzia kazi. Tafadhali epuka kuona kila jambo Serikalini ni lako. Ikifika hapo,yote utayatenda wewe. Wengine watatumbua mishahara ya bure. Tena,utaandikwa na kusemwa sana. Utafurahi na kukereka sana. Utaona na kusikia sana. Utafanya kazi sana. Utachoka sana. Utasema sana. Utatutisha sana!

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam


Wewe ni nani Nchi hii hadi utake ushahuri wako Raisi wa Nchi auchukuwe? Kamshauri Mbowe jinsi ya kuishi na Wema na Mamake, kama ukipenda!
 
Mkuu Vuta NKUVUTE si unamuona Nape kafanya kazi yake bila ajizi kaishia kutumbuliwa bila kosa lolote lile na yule mwenye kosa kaachwa aendelee kupeta! Kaamua wamuogope kuliko hata wanavyomuogopa Mungu wao na kafanikiwa kwa kiasi kikubwa sana. Sasa anapeta tu katika safari yake ya kuiangamiza Tanzania yetu, Oops! kuinyoosha.
 
Kila ugonjwa una tiba au kinga au vyote. Rais wangu na Mwenyekiti wangu wa CCM Taifa,Dr. J. P. J. Magufuli,tafadhali niwie radhi nikushauri kwa mara ya mwisho. Shaurika.

Mimi sikuwahi kuwa Rais. Mwenzangu ndiwe Rais. Lakini,mimi nimekuwa mwanasiasa mwandamizi na hata mtumishi mwandamizi wa idara nyetinyeti Serikalini kuliko wewe. Najua jambo moja kubwa:mgawanyo wa majukumu na kuwa ukomo wa jukumu fulani

Kiserikali,kuna mambo ya Rais;ya Makamu wa Rais;ya Waziri Mkuu;ya Waziri na kadhalika na kadhalika. Kila kiongozi Serikalini ana majukumu na mipaka yake. Ndiyo kusema,si kila jambo lamhusu Rais. Si kila jambo halimhusu Rais. Si mambo yote yanayomhusu Rais kuyashughulikia.

Mhe. Rais,wewe kuandikwaandikwa kwenye media kila uchao si jambo jema sana. Kuandikwa kwako kwa kila litokealo Serikalini ni mchoro wa kutia kihoro. Mchoro huoneshao kuwa unafanya au kusemea kila jambo-hata yale ya Mawaziri,Makatibu Wakuu wa Wizara na kuendelea. Hoja ya jeshi la mtu mmoja huanzia hapo. Haivutii

Mhe. Rais,nakushauri uwaruhusu wasaidizi na wateule wako wafanye kazi zao ulizowaamini wazifanye. Wakizifanya zao,kazi zako zitapungua na kuonekana vyema. Yapo mambo ya kutendwa au kuzungumziwa na wasaidizi au wateule wako. Hata Wasemaji wa Wizara wangetosha na kutisha!

Ushauri wangu unalenga kukupunguzia kazi. Tafadhali epuka kuona kila jambo Serikalini ni lako. Ikifika hapo,yote utayatenda wewe. Wengine watatumbua mishahara ya bure. Tena,utaandikwa na kusemwa sana. Utafurahi na kukereka sana. Utaona na kusikia sana. Utafanya kazi sana. Utachoka sana. Utasema sana. Utatutisha sana!

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Bavicha mnasimamia nini? Maana kila siku nyie hamuelezei Sera zenu Bali kusubiri rais amefanya au kusema nini mpate la kuongea
 
Wewe ni nani Nchi hii hadi utake ushahuri wako Raisi wa Nchi auchukuwe? Kamshauri Mbowe jinsi ya kuishi na Wema na Mamake, kama ukipenda!
Povu la nini? Ushauri anapewa rais povu likutoke wewe! Buku saba bana, rais wetu akiupata huu ushauri ni haki yake kuamua kuuchukua au kuacha. Usimpangie
 
Moja ya sababu kwanini watu siku hizi wanakuwa wanamtukana Rais hovyo hovyo.

Maana wameshamzoea vya kutosha coz president mwenyewe amekuwa pia msemaji wa issues ambazo zingetakiwa kusemwa na makatibu wa wizara. Too bad..

Rais angepaswa kuwa na ule uraibu wetu wa kiafrika kwa baba mwenye nyumba. Anajenga ukuta wa mazoea ya kipuuzi kati yake na family lakini anakuwa kwa mlango wa nyuma anayajua na kuyapanga yote yanayohusu family kwa weledi mkubwa.

Magu alipoteza hiyo sifa tangu mwanzo na ndo kinachomgharimu kwa sasa. Hata akinguruma sahiv hawajali tena, wameshamzoea..
 
Back
Top Bottom