Rais Magufuli ni mzuri katika kuleta maendeleo kwa kasi na kupigana na umasikini. Je, ni nani kutoka upinzani anaweza kufanya hivi?

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
2,590
4,601
Toka alipokuwa waziri katika wizara tofauti, Rais Magufuli alikuwa mtu wa kasi, viwango na ubora. Aliweza kumudu majukumu yake katika hali ya kiwango cha hali ya juu na utendaji kazi wake ulikuwa ni wa kasi na ubora. Hasa alipokuwa waziri wa ujenzi, Rais Magufuli atakumbukwa kusimamia ujenzi hasa wa barabara na madaraja katika kasi, viwango na ubora unaotakiwa. Hakika matokeo tuliyaona, nchi ilitapakaa barabara na madaraja ya kutosha.

Usimamizi huo mzuri wa shughuli za ujenzi katika ubora na kasi inayotakiwa, kwa kiwango kikubwa imeleta kasi kubwa katika maendeleo. Kusema kwamba Rais Magufuli ni mzuri katika kuleta maendeleo kwa kasi ina maana kwamba matokeo ambayo pengine tungeyapata kwa miaka 10-15 ijayo tumefanikiwa kuyaona na kuyapata ndani ya miaka 4 ya uongozi wake. Hii ni kasi kubwa sana katika ujenzi wa taifa letu. Kwa kasi hii, ndoto ya kuwa na uchumi wa kati inawezekana.

Katika kupambana na umasikini, Rais Magufuli kaiva vizuri sana. Moja ya njia za kumkwamua mwananchi dhidi ya umasikini ni Kazi na Rais Magufuli akaja na kauli ya ‘ Hapa kazi tu’ ikiwa na lengo la kutuhamasisha na kutuelekeza umuhimu wa kazi. Katika Uongozi wa Magufuli watu wameshirikishwa na kushiriki vya kutosha katika shughuli za kimaendeleo kama njia ya kuwafikia watu na kuwapatia ujuzi wa kuleta maendeleo na kujikwamua na umasikini. Mabadiliko chanya makubwa yameonekana baada ya watu kuhamasika katika ujasiriamali kama njia ya kuondoa umasikini. Hii ni mifano ya kuonesha ushiriki wa Rais Magufuli katika kupigana na Umasikini ulivyo mkubwa sana.

swali langu ni: je, ni nani kutoka upinzani ana rekodi nzuri kama hii? Kama hamna mtu mwenye rekodi kama hii, Je watanzania watakuwa wana uhakika gani kuwa wakichagua upinzani wataweza kupata maendeleo ya kasi na kupungua kwa umasikini? Mwandishi mmoja aliwahi kusema kuwa’ kosa ambalo utakuja kujuta ni kufanya majaribio ya uongozi’. Kwa maneno hayo ya huyo mwandishi ni ujumbe unaotuasa umakini wa kuchagua na tusimchague mtu kujaribu kama ataweza ama laa.
 
Ni kasi ya hiyo reli, au sijui hilo bwawa la umeme au?

Nafikiri pia na angeleta kasi kunyanyua hali za maisha ya watu angekuwa bora zaidi kuliko kasi ya kuvunja majumba kupisha ma barabara, kuingilia nguvu soko (refer korosho) bureau de change

Kwangu atakuwa Rais bora tu pale uhakika na unafuu wa maisha ya m Tanzania yakiimarika na aachane na dhana ya kila mtu mpigaji
 
CORRECT hakuna Mpinzani atakayeweza kufanya kama anayofanya magufuli
1.Kutoza wamama wauza mchicha 20,000/-
2.Kutolipa wakulima korosho zao.
3.Kuwekeza pesa za ndani katika miradi isiyoingiza fedha kwa muda (current income inflow)
4.Kuvuruga demokrasia kwa kutumia makada katika kuendesha chaguzi.

Narudia tena hakuna mpinzani atakayeweza kufanya kama anayofanya magufuli.
 
Mm true ni mpinzani ambaye naweza mshinda kasi ya kuleta maendeleo -sasa shida sina JESHI-WANAUCHUMI NA WANANCHI ili nikisema neno liwe sheria kwa sasa magu aongoze there after apishe wengine UCHUMI umemshinda
 
Tatizo anaamini katika umimi na sio ushirikishwaji ili kuleta uwajibikaji Wa pamoja...
 
Mtu au watu? Nani kakwambia maendeleo yanaletwa na mtu? Wakati JK anasafiri kulete misaada aliitwa vasco, sasa imekata mnadhani tunasonga mbele kumbe tunafirisi hata kile kilichokuwepo. Acha wafanyakazi wa Benki kuu wakupe mrejesho wa kinachojiri huko ndo uje na hadithi zako.

Nchi yoyote haijengwi na mtu bali watu ndo maana walipotoka ma dictator kama Ghadaffi, Hitler, Sadaam Hussein nchi zao ziliteteleka. Angalia Madulo alivyojaribu kuvaa kiatu cha Chavez kilivyomshinda sasa anahaha. Nchi inaendeshwa na watu siyo mtu. Mtu mmoja hawezi kwenda kwenye mikutano na kutatua matatizo ya watu wawili au watatu wakati kuna watu wana shida kibao. Collective accountability ndo uongozi siyo personal applause itatusongesha mbele.
 
comment za Wanachadema zinachekesha sana
una washwa wewe, humu wapo watu wa dunia nzima, ni sawa na man u wapost kitu alafu boya mmoja aseme comments za wana liverpool zachekesha wakati kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni.

wewe ni mwoga sana, upo kwenye kun di la panya buku na ngedere, wakiona manati wanakimbia kama wameona kifo
 
una washwa wewe, humu wapo watu wa dunia nzima, ni sawa na man u wapost kitu alafu boya mmoja aseme comments za wana liverpool zachekesha wakati kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni.

wewe ni mwoga sana, upo kwenye kun di la panya buku na ngedere, wakiona manati wanakimbia kama wameona kifo
Wewe pia ni mwanachadema tu, majibu yenu na malugha yenu, easy to spot.
 
To be honest, sioni mpinzani wa kweli Tanzania hii atakaeweza kufanya anayoyafanya Magufuli leo. Hata kama ingekuwa mpinzani huyo kalewa chakari kabla hajaamua bado hawezi kufanya vituko hivyo avifanyavyo Magufuli sasa.
mie huwa nashangaa sana mnaompa big up huyu jamaa, hebu tembeleeni vijijini ndio muone hali ilivyo, unampa elf 1 mwanaume mwenzako anakupigia magoti anakushukuru mpaka chozi linamtoka, acheni hizo, maendeleo ni watu na sio vitu,labda kama kuteka,kuweka mahabusu, kufungwa kwa amri kutoka juu, kupiga risasi na kuua , hapo kwa kweli naungana na wewe
 
Back
Top Bottom