Rais Magufuli ni mfano hai wa 'nabii hakubaliki kwao'. Nchi nyingi zinamtamani, Watanzania tusiipoteze zawadi hii

Ndiyo maana huyo JPM anakataliwa maana hata yeye amejaa ubaguzi na chuki zisizo na maana na tutamtandika achakae!
Ahaaaa.. Alichakaaje.. Vipaja sasa.. 😂
🤸🏾‍♂️🤸🏽‍♀️🤸🏾‍♂️🤸🏽‍♀️🤸🏾‍♂️🤸🏽‍♀️🤸🏾‍♂️🤸🏽‍♀️🤸🏾‍♂️
 
Hakuna mpinzani wakumuondoa Magufuli Kwa sasa Never
Magufuli ndio Rais wetu Mpaka 2025
😂😂😂😂
🤸🏾‍♂️🤸🏽‍♀️🤸🏾‍♂️🤸🏽‍♀️🤸🏾‍♂️🤸🏽‍♀️🤸🏾‍♂️
 
Ule usemi wa Nabii hakubali kwao, ni mfano hai uliopo hapa Tanzania, nchi jirani zinamtamani Mh. Magufuli akaitawale nchi zao angalau hata kwa dakika moja lakini haiwezekani. Mh magufuli amefanya mengi kupita hata matarajio yake, Watanzania tukiyaona machozi ya furaha yanatububujika, tunayafuta machozi na Mh anaona kweli watanzania wanayo furaha, wakiangalia zahanati kila kona ya nchi zipo, barabara, shule na elimu bure, maji, umeme vijijini nk.

Watanzania tuna mengi ya kujivunia, Mwenyezi mungu akaongea naye na kumpa maono ya kukataa katakata kuwaweka watu wake kwenye lockdown akiitisha ibada maalum nchi nzima ya kumuomba mwenyezi mungu atuondolee hili balaa la korona, watanzania wake kwa waume, watoto kwa wazee tukapiga magoti tukamlilia muumba, akasikia kilio chetu, shetani akashindwa. Mwenyezi mungu akaongea naye kwa kukataa misaada na vipimo feki vya korona tukashinda huo mtego wa pili na maisha yanaendelea.

Sasa kuna bwana mmoja anadai ugonjwa bado upo na huyo huyo anautangazia ulimwengu, cha ajabu ndiyo anazidi kuleta misongamano ya watu eti anahitaji udhamini agombee urais- URAIS? "shame on you", hapo unajiuliza huyu mtu anaakili timamu au ubongo wake ni kologete? Kama ugonjwa upo atamuongoza nani iwapo kasababisha maambukizi makubwa kiasi hicho cha ugonjwa kwa misongamano hiyo? Nani atakaye mpigia na kumpa KULA ili aje atule vizuri na mabeberu wake iwapo kama Watanzania wakiambukizana ugonjwa huo ambao anauaminisha ulimwengu kuwa bado upo? Sasa hata hao mabwana zake wakimfatilia wakao misongamano hiyo siwanamshangaa? Ama kweli nyumbu bado mnasafari ndefu, mto mara bado unawahusu kuuvuka sijui kama wote mtaweza kuvuka

Alituaminisha mikataba feki ya madini ikivunjwa serikali ya JMT inayoongozwa na Mteule wetu Mh. JPM itashitakiwa MIGA, jemedali akasema na mungu naivunja na kama kweli Mungu umeamua watu wako hawa ulionipa niwaongoze na kuwavusha bahari ya shamu na kuwapeleka katika nchi ya asali na maziwa, basi hawa wanyonnyaji watushitaki. Mungu akasimama nasi wakashindwa kwa jina la YESU leo tunaona matunda ya maliasili zetu, Bwawa la Umeme Stigler akavunja mkataba wa UNESCO, tuna tarajia kuwa supplier wa umeme siku sinyingi zijazo n.k

Kwa ujasili huu, nchi nyingi na dunia kwa ujumla imemuelewa, Mh. Mgufuli watanzania tumekuelewa usiwe na shaka baba, kura zote nizako. Endelea kutafuta wadhamini kimyakimya sisi tunakuelewa hatutaki mikusanyiko isiyo ya lazima kwa wakati huu, kampeni bado baba, usijichoshe ukifika wakati utaona kweli Watanzania tumekuelewa.

Ni hayo tu. NABII HAKUBALIKI WAKO ILA WATU WA NCHI ZINGINE WANAKUHITAJI UKAWE RAIS WAO HATA KWA LISAA LIMOJA TUU, UKAWAFANYIE KAMA HAYA NA ZAIDI YA HAYA KATIKA NCHI ZAO, WEWE UMEKUWA NI KIOO CHAO, ila Watanzania tunatamani uwe Rais wa Mihura minne mfulurizo. SIJA TAJA JINALA MPINZANI YEYOTE
zaidi ya uganda , Rwanda nchi gani zinamtamani?

SUKUMA GANG bado mnatapa tapa kwenye maji, wenzenu MATAGA wameamua kutulia na kuanza kumsifia MAMA.
 
Wizi, ndio mlikuwa mnamsifu na kuiba mali za Watanzania, Ni Nchi gani ambayo inaweza kumruhusu Kiongozi kufanya vitu bila kufata Sheria au Katiba , yaani maneno yake ndio sheria Nchi gani inaruhusu upumbavu huo,

Mmezoea kuishi kwa uongo kama yule mkalimani wenu

Ndio maana tulikuwa tunaona Mabarozi wa Nchi fulani wakiongea kitu, mnakuja na tafsiri tofauti, mkibanwa na walioelewa mbamwita Barozi na kumwonya
 
Hata kama amefariki lazima tuseme ili waliopo wajifunze

1. Alikuwa mtu mwenye roho mbaya, mshenzi, muuaji na aliyependa kuona watu wenye maendeleo au waliotofautiana nae wakiteseka sana. Mfano wa haya ni kwa vile walivyowafanyia Manji, Erick Kabendera, Ben saanane, Rwabaje, Mama yake Erick Kabendera, Mdude Nyangali, Zacharia na watu wengine wengi

2. Alikuwa mtu Mbinafsi sana, aliyependa sifa zote zirudi kwake. Alipenda kusifiwa, kuonekana yeye ni bora kuliko wenzake. Hata kwenye hotuba zake alipenda kujionesha ni yeye zaidi na wala sio wenzake. Rejea hotuba alizokuwa akisema bila yeye miradi haitofanikiwa. Aliwapa vyeo bila aibu watu waliokuwa wakimsifu yeye binafsi. Mf. Katambi, Sabaya, kafulila, Mrema, Babu

3. Alikuwa mkabila na mbaguzi wa kikanda aliyetukuka. Kwenye awamu yake alijaza watu wa kanda ya ziwa hasa wasukuma na mapandikizi wenzake kutoka Rwanda na Burundi kwenye nafasi nyeti serikalini. Bashiru, Kakoko, Doto James na wengineo wengi ni mifano michache tu. Hawa watu walikuwa hawagusiki na waliweza kufanya lolote lile kwa jina lake na yeye hakusema lolote. Hawa watu waliweza hata kuwadharau waziwazi Waziri Mkuu na Makamu wa Rais na wala hawakujali mfumo wa utendaji serikalini. Waliweza kupiga simu au kupita moja Kwa moja ikulu hadi kwa Magufuli bila kupita kwa waziri, waziri mkuu au hata Makamu wa Rais.

4. Kwa kujua kwake kuwa ni kweli aliharibu uchumi wa nchi kwa sera zake mbaya, aliwekeza sana kwenye propaganda za kujitangaza sana kupitia vyombo vya Habari ili kuwa brainwash watu wasiofikiri vizuri. Tv zote, magazeti, blogu na hata viongozi wa dini aliwatumia kumtangaza yeye muda wote na kumsifu yeye muda wote ili aonekane ni Bora kuliko wenzake. Ofisi za Taifa zilifanywa kutengeneza data za uongo ili aonekane anafanya vizuri kumbe nchi ilikuwa inaenda pabaya sana. Rejea taarifa aliyotoaga kuwa ATCL inapata faida ya bil 28.

5. Aliwadharau sana wenzake. Na alifanya kila jitihada wenzake waonekane watu wasiofaa ( hasa viongozi waliopita). Aliishi nao kiunafiki akiwatumia vijana wake Kama Msiba, Sabaya , Makonda na Aly Happi kuwatukana na kuwatisha ili aharibu taswira yao kwa jamii na ajitengeneze kuwa ni Bora kuliko wao.

6. Alianzisha mambo ili kuwakomoa watu waliokuwa tofauti nae. As Kofi niwemugizi, Aidan Eyakuze, Yusuph Manji ni wachache kwenye hii list, walianza kuhojiwa uraia, wakanyang’anywa passport na kupewa kesi mbalimbali ili kukomolewa kutokana na kutofautiana nae.

7. Kwa sera zake mbovu, aliharibu kwa kiasi kikubwa uchumi hivyo kupelekea kuwepo tatizo kubwa la ajira . Ili kujiokoa na Tatizo hili Kwa kuwapumbaza watanzania wajinga alianzisha utaratibu wa kujifanya kuwa karibu na Mama lishe na bodaboda huku akisema kuwa wanaruhusiwa kufanya Biashara popote pale. Alifanya hili Kwa sababu alijua kabisa kuwa ameharibu uchumi wa Tanzania na amesababisha watu wengi kukosa ajira. Kuepuka lawama akataka kuifanya nchi nzima kuwa nchi ya wachuuzi huku akiharibu mipango miji na kusababisha walipa kodi wapungue kwa kasi.

8. Kutokana na kuwa na sera mbovu za kiuchumi huku akiiba Mali za watanzania Kwa kigezo cha uzalendo, akiogopa kupinduliwa na jeshi na wasaidizi wake, aliamua kufuatilia maongezi ya wasaidizi wake wote akiwemo Makamu wa Raisi , Mawaziri na viongozi wa Ccm. Alikuwa hadi meseji zao anasoma na alivyo mshamba alikiri hadharani kuwa anafuatilia mawasiliano ya watu. Alianzisha pia utaratibu wa wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama kuwa nae popote pale anapokuwepo. Huu utaratibu ulikuja kuonekana katika awamu ya 5 tu maana Kwa awamu ya 1 hadi ya 4 haikuwai kutokea wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na spika na Jaji mkuu kuambatana na Rais popote pale anapokuwa.

9. Alikuwa muuaji
Niliwai bishia watu wengi kwenye hili ila nilikuja kuthibitisha alipokuja tamka hadharani kuwa huwezi kuwa msaliti alafu uka survive na baada ya hotuba yake iyo Tundu Lissu alikuja kushambuliwa kwa Risasi 38 huku 16 zikiingia mwilini wake.

10. Alijiona ni Bora kuliko mtu yeyote yule na alitaka neno lake ndo liwe mwisho. Alisema hadharani kuwa hashauriki na kila mtu aliyekuwa akimshauri alimchukulia kama adui yake. Siku za mwisho za uhai wake alitofautiana na kupingana Hadi na viongozi wa dini wa kanisa katoliki ambao waliamua kushauri nchi kuchukua hatua tofauti dhidi ya corona.

Mungu fundi sana! Alale anapostahili mwendazake.
Natamani afufuke, asome haya, halafu afe tena.
 
Wasiompenda JPM ni wale wachawi, wenye hirizi na majini kwasababu JPM alikua mtu wa Mungu hawezi kupendwa na wachawi.

Wala usijihangaishe ukiona mtu hampendi JPM au alikua hampendi JPM ujue ni mchawi. Wale wote wenye hirizi viunoni hawawezi kumpenda JPM hata mara moja kwasababu JPM alikua akihubiri habari za Mungu.

Mchawi yeyote huwa hapendi mtu anayehubiri habari za Mungu. Mchawi yeyote hufurahi mhubiri wa habari za Mungu anapokufa.

Watu wenye mapepo hawawezi kumpenda JPM hata mara moja. Mimi naelewa sana jinsi haya mambo yalivyo. Kuna watu wamepata vyeo kwa kutumia hirizi na wengine wamepata uongozi kwa kupitia mapepo. Na wengine wamepata uongozi kwa kupitia majini. Kuna watu wamefuga majini sasa watampendaje mtu anayehubiri ufalme wa Mungu.

Hayo yalisha nitokea sana nikiwa nahubiri na kuitangaza injili.
Jaribu kutafakari kwenye mkutano wa JPM hakuwezi kukosa watu wenye hirizi viuoni. Sasa akisema Mungu hoyee hirizi zinaanza kushituka.

Hata Petro na Yohan walipokuwa wakitaja juu ya ukuu wa Mungu walipata upinzani mkubwa kutoka kwa wachawi. Wachawi hawakupenda zile habari za akina Petro na Yohan zilizokuwa zikitaja juu ya ukuu wa Mungu zikiambatana na nguvu ya Mungu aliyeziumba mbingu na nchi.
Ukimpenda wewe inatosha sio lazima wote tumpende,hata wewe mwenyewe hupendwi na wote
 
zaidi ya uganda , Rwanda nchi gani zinamtamani?

SUKUMA GANG bado mnatapa tapa kwenye maji, wenzenu MATAGA wameamua kutulia na kuanza kumsifia MAMA.
mnasifia kwa sababu mnaelewa mumeshapata mteremuko wa kumujumu huyu mama, eti munafuraha, furaha ipi hata tarehe 1 may 2021 bado. Bajeti ya serikali bado, furaha inakuja baada ya hivyo vyote kupitiwa. Au mnafuraha kwa vile ameshadecleare kupungua kwa mapato kwa muda wa miezi 3 hadi 6, kama siyo miaka 3 hadi 6. NO DEVELOPMENT, MASHINGO YAMEWASHUPAA HUKO BUNGENI, KUABANDON KAZI ZILIZOASISIWA NA AWAMU YA TANO. SAWA ENDELEEENI TU KUMSIFIA KWA MGONGO WA CHUPA. Tutawashitaki kwa mungu kama siyo mwaka 2025
 
mnasifia kwa sababu mnaelewa mumeshapata mteremuko wa kumujumu huyu mama, eti munafuraha, furaha ipi hata tarehe 1 may 2021 bado. Bajeti ya serikali bado, furaha inakuja baada ya hivyo vyote kupitiwa. Au mnafuraha kwa vile ameshadecleare kupungua kwa mapato kwa muda wa miezi 3 hadi 6, kama siyo miaka 3 hadi 6. NO DEVELOPMENT, MASHINGO YAMEWASHUPAA HUKO BUNGENI, KUABANDON KAZI ZILIZOASISIWA NA AWAMU YA TANO. SAWA ENDELEEENI TU KUMSIFIA KWA MGONGO WA CHUPA. Tutawashitaki kwa mungu kama siyo mwaka 2025
Sikia OTTER, ni kweli hajaongeza mshahara wala hajagawa fedha barabarani lakini kauli yake,unyenyekevu wake, uungwana wake na kusudio la kufuata utawala Sheria ni sababu tosha kumuunga mkono mama SSH. Tunaamini unaweza kukusanya kodi na kujenga miundombinu bila kutumia mabavu kama JK na BWM walivyofanikiwa.

Mwendazake alikuwa mwizi, mwongo, mropokaji, mwenye dharau na tapeli.
 
Sikia OTTER, ni kweli hajaongeza mshahara wala hajagawa fedha barabarani lakini kauli yake,unyenyekevu wake, uungwana wake na kusudio la kufuata utawala Sheria ni sababu tosha kumuunga mkono mama SSH. Tunaamini unaweza kukusanya kodi na kujenga miundombinu bila kutumia mabavu kama JK na BWM walivyofanikiwa.

Mwendazake alikuwa mwizi, mwongo, mropokaji, mwenye dharau na tapeli.
Huihui2 acha bhana. Tangu lini mama akawa na ziara za kusalimia wananchi? kujua kama amaegawa fedha njiani au lah?. naona unatoa majibu yakusadikika. Waliofurahi ni wafanyabiashara maaana hawatoi risiti, tembelea kwenye baadhi ya vituo vya mafuta, mfumo wa utoaji risiti ni mibovu na bado mafuta yanauzwa kama kawa. Nenda madukani kanunue bidhaa risiti hawatoi hadi umkomalie. ukikomaa sana anakwambia bei inabadilika, hivyo kuna bei ya risiti na bei yakutotoa risiti. HATARI
 
Huihui2 acha bhana. Tangu lini mama akawa na ziara za kusalimia wananchi? kujua kama amaegawa fedha njiani au lah?. naona unatoa majibu yakusadikika. Waliofurahi ni wafanyabiashara maaana hawatoi risiti, tembelea kwenye baadhi ya vituo vya mafuta, mfumo wa utoaji risiti ni mibovu na bado mafuta yanauzwa kama kawa. Nenda madukani kanunue bidhaa risiti hawatoi hadi umkomalie. ukikomaa sana anakwambia bei inabadilika, hivyo kuna bei ya risiti na bei yakutotoa risiti. HATARI
Mimi hata wakati wa Mwendazake sijawahi kuchukua risiti. Hii Sheria ya kulazimisha mtu kuchukua risiti ilikuwa ya KISHAMBA tu. Nimetembea nchi nyingi duniani kuchukua risiti ni HIARI tu.

Usidhani kwa kulazimisha risiti watu hawaibi, waliiba Kama kawaida.

Mwendazake alikosea sehemu moja. Aliwafirisi wafanya biashara wakubwa then akakosa mahali pa kukusanya kodi, ndiyo akaja na wimbo wa KIJINGA wa EFD machine.

Mkapa na Kikwette ndiyo waliojenga uchumi imara bila hiyo EFD yako.

Ukiwa kiongozi unapswa ufuate Pareto principle kwenye kujenga uchumi. Pareto Principe inasema ni Asilimia 20% tu ya walipa kodi ndiyo huleta 80% ya mapato yote. Hao ndiyo una deal nao kama Twiga Cement, TCC, TBL, BAKHRESSA, MODEWJI, IPP etc. Hawa akina kajamba nani waliobakia ambao ni 80% wanachangia 20% tu ya mapato ambao ni vituo vya petrol station, maduka ya Kariakoo, mabaa, guest house, mabasi etc.

Yaani nguvu kubwa inatumika kwenye chanzo kikubwa cha kodi. Hiyo ndiyo AKILI

Lakini akili mbovu ya Mwendazake iliwakera na kuwa harass wafanyabiashara Kama Yusuf Manji ikasahau kuwa ni mlipa kodi kupitia wafanyakazi aliowaajiri, bidhaa anazo nunua na ku export as well as anazo import
 
Back
Top Bottom