Rais Magufuli,kwanini usimpe Hussein Bashe hata Unaibu Waziri wa Wizara ya Fedha?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,034
144,387
Raisi Magufuli,japo mimi si mwana-CCM,lakini nakiri hadharani kumkubali sana mbunge wa chama chako, mh. Hussein Bashe kwani anaonyesha ni mbunge makini,mzalendo na mwenye uchungu na nchi hii na mwenye uelewa mzuri wa maswala ya fedha na uchumi.


Ukimsikiliza Hussein Bashe utagundua kabisa kuwa anaongea kwa uchungu tena kutoka moyoni na anajua ni nini cha kufanya kurekebisha mapungufu yaliyopo ila ni bahati mbaya tu hayuko katika nafasi inayomuwezesha kutekeleza mawazo yake zaidi ya kushauri tu.

Mh.nakuomba ujaribu kufikiria kumpa nafasi ya kumsaidia Waziri wa Fedha kwa kumteua kuwa Naibu Waziri kwani ninaamini atakuwa na mchango mkubwa sana katika kuleta mabadilko na tija katika wizara hiyo iwapo atapata hiyo nafasi na pia hataingiliwa au kukwamisha na mamlaka za juu katika utendaji wake.

Mh.Raisi,Hussein Bashe ni hazina ndani ya chama chako kama walivyo kina Tundu Lissu ndani ya upinzani hivyo itumie hiyo hazina kwa manufaa ya nchi hii.

Ni ushauri tu.
 
Raisi Magufuli,japo mimi si mwana-CCM,lakini nakiri hadharani kumkubali sana mbunge wa chama chako, mh. Hussein Bashe kwani anaonyesha ni mbunge makini,mzalendo na mwenye uchungu na nchi hii na mwenye uelewa mzuri wa maswala ya fedha na uchumi.


Ukimsikiliza Hussein Bashe utagundua kabisa kuwa anaongea kwa uchungu tena kutoka moyoni na anajua ni nini cha kufanya kurekebisha mapungufu yaliyopo ila ni bahati mbaya tu hayuko katika nafasi inayomuwezesha kutekeleza mawazo yake zaidi ya kushauri tu.

Mh.nakuomba ujaribu kufikiria kumpa nafasi ya kumsaidia Waziri wa Fedha kwa kumteua kuwa Naibu Waziri kwani ninaamini atakuwa na mchango mkubwa sana katika kuleta mabadilko na tija katika wizara hiyo iwapo atapata hiyo nafasi na pia hataingiliwa au kukwamisha na mamlaka za juu katika utendaji wake.

Mh.Raisi,Hussein Bashe ni hazina ndani ya chama chako kama walivyo kina Tundu Lissu ndani ya upinzani hivyo itumie hiyo hazina kwa manufaa ya nchi hii.

Ni ushauri tu.
Kampuni aliyoachiwa na Rostam imemshinda sembuse unaibu waziri wa fedha?halafu kwa kipi hadi Bashe apewe uwaziri ?mwache awe mpiga kelele wetu backbencher
 
Wewe unajiandikia tu ili mradi umeandika!

Kabla ya kuandika utumbo lazima uelewe kuwa wizara zinazohusu Muungano lazima waziri au naibu Waziri atoke upande mmoja wa muungano.

Sasa kama unataka Bashe awe Naibu Waziri wa Fedha, nani kutoka Zanzibar atakuwa Waziri wa fedha.

Halafu kwa akili zako unadhani kuongea sana ndiyo ueledi wa kazi
 
Wewe unajiandikia tu ili mradi umeandika!

Kabla ya kuandika utumbo lazima uelewe kuwa wizara zinazohusu Muungano lazima waziri au naibu Waziri atoke upande mmoja wa muungano.

Sasa kama unataka Bashe awe Naibu Waziri wa Fedha, nani kutoka Zanzibar atakuwa Waziri wa fedha.

Halafu kwa akili zako unadhani kuongea sana ndiyo ueledi wa kazi

Hako kajamaa kamekuwa ni karopokaji tu siku hizi.

Kutwa kucha kanaandika pumba tu humu.
 
Good Thinking.

Hussein Bashe anajitambua, upeo wake ni mkubwa sana, anaelewa maana ya uongozi na pia ni Mzalendo.Hakwenda Bungeni kwa kubahatisha.Ukiwa na sifa hizi nchini basi CCM haitokaa ikuelewe na pia unaonekana mshamba.

Hata watumwe Mitume na Manabii kuiambia CCM una sifa hizo hapo juu, haitokaa ikuelewe.Anafaa kuwa kiongozi mkubwa nchini, si kuishia kuwa mbunge tu, hata Uwaziri Mkuu unamfaa.Tatizo ni pale mawazo yake yanapokinzana na Akili za CCM.Na asipoangalia ataweza kufanyiwa abrakadabra na chama chake asirudi tena bungeni.

Inaonekana hakuwa mwanasiasa wa kubahatisha, na wala hana bahati ya kuwa mwanasiasa ila Taifa ina bahati ya kumpata kiongozi kama yeye.Si wapiga makofi kama walivyo wanasiasa wengine bungeni.

Yupo rafiki yangu mmoja anapenda kuniambia, Huyu jamaa ni Upinzani.Sijui huwa nanamaanisha nini?.
 
Back
Top Bottom