Rais Magufuli avunja ratiba yake na kwenda kumjulia hali Mzee Kazimoto. Je, ni nani huyu Mzee Kazimoto?

leonaldo

JF-Expert Member
Oct 26, 2014
2,585
3,179
DOCkIqtW4AAICOQ.jpg:large.jpeg

Rais Magufuli akiomba pamoja na Mzee Kazimoto na wanafamilia.
Mzee kazimoto ni mkazi wa Kayanga karagwe katika eneo la Bugene.
Mzee huyu wakati wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Kyaka Bugene alikuwa ni miongoni mwa watu ambao nyumba zao zilipaswa kuvunjwa ili mradi uweze kutekelezwa, Mzee Kazimoto alipinga ubomoaji huo ndipo walipokutana na Rais Magufuli wakati huo akiwa waziri wa ujenzi.

Ubomoaji ulifanyika chini ya usimamizi wa waziri kipindi hicho na kusababisha kuharibika kwa mahusiano kipindi hicho lakini baadae mzee huyo alikuja kubaini nia nzuri ya Serikali kuhusiana na maendeleo na hivi sasa ni marafiki.

Rais Magufuli abaini kuugua kwa mzee huyo baada ya kuuliza uwepo wake kwenye ufunguzi wa barabara hiyo,na baadae kupata taarifa kuwa mzee huyo ni mgonjwa na kuamua kwenda kumjulia hali.

Maendeleo hayana adui asante rais kulitambua hilo.
 
Mzee kazimoto ni mkazi wa Kayanga karagwe katika eneo la Bugene.
Mzee huyu wakati wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Kyaka Bugene alikuwa ni mipngoni mwa watu ambao nyumba zao zilipaswa kuvunjwa ili mradi utekelezwe,mzee kazimoto alipinga ubomoaji huo ndipo walipokutana na Rais magufuli wakati huo akiwa waziri wa ujenzi.
Ubomoaji ulifanyika chini ya usimamizi wa waziri kipindi hicho na kusababisha kuharibika kwa mahisiano kipindi hicho lakini baadae mzee huyo alikuja kubaini nia nzuri ya serikali kuhusiana na maendeleo na hivi sasa ni marafiki.
Rais magufuli abaini kuugua kwa mzee huyo baada ya kuuliza uwepo wake kwenue ufunguzi wa barabara hiyo,na baadae kupata taarifa kuwa mzee huyo ni mgonjwa na kuamua kwenda kumjulia hali,
Marndeleo hayana adui asante rais kulitambua hilo.
Was that proper in a democratic and rule of law abiding country?
 
Huyu mzee nadhani atakuwa maarufu na ukoo mpana Karagwe. Nimesoma Karagwe na darasani nilikuwa na Kazimotos mawili, ila shule nzima kulikwa na Kazimotos zaidi ya watano.

Ngoja wenyeji waje kumwaga historia.
Taja majina yao ya kwanza
 
Wewe ni kazi moto na mimi ni moto kazi lazima nyumba yako ivunjwe! Ndiyo maneno alisema nimedokezwa kutoka kwa clinical officer wangu
 
Mara paap, Kagera Sugar inazinduliwa...watu weweeeeeee!
Lazima hapo akazindue kiwanda maana nasikia kuna vyerahani vinne vimeletwa kwa ajili ya kushona uniform za wafanyakazi wa kiwanda cha sukari! Tayari hicho ni kiwanda cha ushonaji, hivyo lazima Rais aende akazindue!!
 
Aende na tabora watu wamekufa kwa presha ya kuvunjiwa nyumba zao
 
Dk Magufuri mwema sna sema kuna watu wanamvuruga
Tuseme ukweli hapo anataka kumsanifu tu maana alipokuwa Waziri wa Ujenzi alimueleza wewe ni kazimoto na mimi ni moto kazi nyumba yako lazima ivunjwe. Sasa urafiki umetoka wapi? Hili unalijua leonaldo ? Usisahau Kazimoto wakati huo alikuwa Chadema kindakindaki. Haya nimeelezwa na Cleanical Officer rafiki wa Retired
 
Back
Top Bottom