Rais Magufuli asante kwa Reli ya Kisasa.

Rais Magufuli asante kwa Reli ya Kisasa.

Kumbe hujui kinachoendelea hiyo 100% ni fedha zetu na tayari kandarasi fedha ipo tayari 50%.
Sasa kama ni pesa zetu wananchi kwanini tumpongeze magu?? Kwanini tusijipongeze sisi kwa kodi zetu?? Maana yeye hata kodi halipi!!
 
Elimu bure hakuna kabisa..CCM mlikopi Sera tu

Mikopo ya Elimu ya juu mmeshindwa

Afya ni hatari nchi nzima

Dawa mpaka za chanjo hakuna
Ulishasikia watu wameandamana kwa kukosa mikopo kama awamu iyopita? Acha longolongo wewe. Pesa zipo na wanapewa.
 
Hakuna uhakika wala mahali pa kuthibitisha kuwa ujenzi wa reli utayaleta hayo unayoyasema yakiwemo kushuka kwa bei za kusafirisha bidhaa kutoka point A kwenda either point katika nchi hii.

Hii dhana sijaitoa ulaya, ni humu humu na nitakupa mifano kuntu na jadidi ya faragua mlengo wangu.

Tuliambiwa gesi asilia ya kule msimbati mtwara itapunguza bei kama sio kuufanya umeme kuwa wa uhakika nchini. Kiko wapi????

Treni sio njia au namna nzuri ya kupunguza bei za usafirishaji bidhaa. Nenda railway stations yoyote uliza bei ya kusafirisha Kg moja ya bidhaa fulani ni shilingi ngapi halafu ingia kwa wadau kwa mtaa uone kama bei za railway sio za usafiri wa kianasa.

Tuliwahi kuambiwa barabara ikikamilika nauli zitashuka kutoja point A to either points. Tena wakajibasibu kuwa hata muda wa kusafiri utapungua. Sitaki kuongea mengi bei za nauli zinajulikana na muda unaotumika umekuwa mara dufu na tochi nazo zimeongeza mapato kuliko TRA.

Hasara za ujenzi wa miundombinu hii ni kuongezeka kwa deni la taifa, madalali kuvuna hela za kutosha, ajali na watu kupoteza makazi na hicho ndicho huharibu uchumi hasa katika ngazi ya familia.

Hapo ndipo Prof. wangu unaweza m-google anasema "as concurred to previous premise that, do not trust those guys the only and only if truth that they can utter are neither their names as powered by bashite'z sagga"
Usafiri pekee wenye gharama nafuu duniani kote ni Reli.
 
Kuliko hii reli ni mara elfu angeboresha huduma za Afya.

Hali ni mbaya sana..

Nilikuwa Ocean Road leo.. Hiyo foleni ya wagonjwa wa Kansa kupata tiba ya mionzi inatisha.
Nchi nzima mashine ya mionzi moja..
SHAME.

Hosp ya Mkoa wa Mtwara huduma za maabara zimesimamishwa sababu hakuna maji..
Only Maji yamesababaisha maabara kusifanye kazi.
Hamna maji hospital nzima.

Hospital zote hali ni mbaya.. Mbaya.. Mbaya.
AIBU.

Sisapoti kabisa hayo maproject ya treni za umeme wakati umeme wa uhakika wa majumbani tu wala sio wa viwandani HATUNA..

SHAME on you CCM Government.
Shame.
Tuanze na Reli then changamoto za umeme zitashughulikiwa tayari tukiwa na Reli. Hata hivyo kwa swala umeme serikali imejitahidi kwa sisi tunaishi vijijini tunashukuru maana hata bibi zetu nao wana enjoy.
 
Acha upu,,mbav

Watanzania wote wana vyama?

Dawa Hospitalini hakuna

treni ya umeme bila Umeme...Treni itatumia Power bank?

Gesi ya Mtwara...Iko wapi?

Umeme bei ghali kuliko umeme wa maji

Ethiopia umeme upo wa kutosha

Acha ushamba wewe

Mtu akitoa maoni unamuweka kwenye siasa....Mshamba wa Kolomije wewe
Hii treni inatumia umeme na mafuta ndugu.
 
Rais wangu mpendwa John Pombe Magufuli Salaam. Napenda kuchukua fursa hii kukushukuru kwa zawadi nzuri ya Reli uliyotupatia sisi watanzania wanyonge. Naona baadhi ya watu wanabeza jitihada zako lakini najua ipo siku watakukumbuka na kudai tume kumiss. Binafsi nimependezwa sana na kuanza kwa ujenzi wa Reli na najua ikikamilika itafungua fursa nyingi za kiuchumi hasa kwa wafanyabishara wadogo. Na niwahakikishie watanzania wa hali ya chini katika kipindi hiki cha utawala wa John Pombe Magufuli ndo wakati wa kunemeeka cha msingi ni kuchapa kazi. Reli hii itatuwezesha kusafiri na kusafirisha mizigo kwa bei nafuu tofauti na tunavyogongwa hivi sasa na wenye Malori na Mabasi.
mavi ya kuku haya kula hiyo reli
 
mavi ya kuku haya kula hiyo reli
[emoji1] [emoji1] Reli itajengwa hata kama ni kwa style ya Mkoloni. Maana Mkoloni ametupa uzoefu na hata hivyo wakati anarudi kwao hakuondoka nayo. Lakini pia jua hiyo Reli inayoitwa ya Mkoloni kuna watu waliumia leo sisi ndo tunafaidi. Kiongozi mzuri ni yule anayejiami na anasimamia maamuzi yake ili mradi kile anachokiamini kiwe sahihi hata kama ni Unpopular decision. Baadaye mtamuelewa tu Rais wetu John Pombe Magufuli
 
Watu hawajui shida zilizopo huko mahosptalini..ndio maana mnapongezana!...
 
Watu hawajui shida zilizopo huko mahosptalini..ndio maana mnapongezana!...
Sekta ya Afya huboreshwa kila mwaka. Mwaka huu Rais ameajiri madaktari. Sasa sijui unataka iboreshwe sekta ya Afya iboreshwe vipi.
 
Back
Top Bottom