Rais Magufuli anayajua haya kuhusu Muhimbili? Hata uweke Mkurugenzi gani kazi ni bure!

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,252
8,003
Jana Rais alitembelea hospitali yetu ya taifa Muhimbili kumtembelea Mufti mkuu sheikh Aboubakar Zuber, lakini wakati wa safari yake hapo akadakwa na kina mama ambao walikua wakiuguza ndugu zao waliokwishajifungua hospitalini hapo, ndipo Rais alipoamua kuwasikilaza na kuongozana nao hadi wodi ya wazazi na kukuta idadi kubwa ya kinamama wamelala kiholela chini.


Binafsi nimekaa hospitalini hapo muda mrefu sana wakati nikimuuguza kaka yangu aliyekua amelazwa wodi ya mwaisela kiasi kwamba nilifikia mpaka kufahamiana na matabibu wengi na wauguzi na kujihisi kama mwenyeji.
Lakini kwa udukuzi wangu wa mambo ilibidi nijue niñi hua kinaisibu hospitali hiyo mpaka huduma kuzorota?

TATIZO

Ndani ya hospitali hiyo kuna idara nyigi sana na kurugenzi zake ambazo zinawajibika moja kwa moja kwa Mkurugenzi mkuu wa hospitali, lakni cha ajabu ni kwa wakuu wa idara hizi hukalia nafasi zao kwa muda mrefu mfano idara ya uuguzi,tiba, utumishi, fedha,ufundi,maabara,Radiolojia nk, hawa wakuu wa idara wengi wao hawatoi taarifa za kuaminika kwa Mkurugenzi mkuu ili aweze kushughulikia kama kuna matatizo, wamekua wakitoa taarifa za kumridhisha mkurugenzi tu tofauti na uhalisia.Wakuu hawa wa idara zote wamekalia nafasi zao kwa muda mrefu na wengine hujirudia mara kwa mara hali iliyowanya kufanya kazi kwa mazoea na ndio maana fiksi zinakua nyingi.
Kuna mzee mmoja Daktari hospitalini hapo waliniambia kwa mfano kuna idara kama ya ufundi vifaa zinaibiwa sana lakini uongozi uko kimya, idara ya tiba iko kimya ilihali kuna wagonjwa wanafika hospitalini hapo wanatibiwa na kupona lakini wanacheleweshwa kuruhusiwa na kubaki kulipia tu kila siku tu na kusababisha msongamano wodini.


TATIZO LA KINA MAMA KULALA CHINI!


Hapa tatizo liko idara ya tiba ambapo hata wale wagonjwa wasiokua na complicated cases za kupelekwa Muhimbili lakini wanalekwa na kupokelewa badala ya matatizo yao kushughulikiwa hata kwenye vituo vya afya huko, maana wanaopenda Muhimbili wagonjwa wasiostahili kupelekewa pale unategemea wenye hali mbaya wanaostahili kwenda pale wakipokelewa watalala wapi kama sio chini?
Kiingine ni Madaktari kuchelewa kuwaruhusu wagonjwa ambao waliokwisha pona hali inayopelekea wale wapya waokuja kulala chini.

Idara ya fedha nayo inalalamikiwa kwa kujumlishia wagonjwa bili ya gharama kubwa tofauti na gharama halisi alizotumia mgonjwa.


Kwahiyo Rais wangu Magufuli tumbua majipu badili idara zote na kurugenzi zote ndani ya hospitali hiyo! Hiyo kazi hata mawaziri wako wanaweza kufanya maana lasivyo utatwanga maji kwenye kinu miaka yako yote mitano bila mafanikio! Mbona Prof Sarungi aliiweza hospitali ya taifa Muhimbili?
 
Kama hakuna pesa tusitegemee huduma bora, sasa mkurugenzi angetoa pesa yake mfukoni kuboresha muhimbili? Yeye magu mbona wizara ya ujemzi ilikuwa hovyo!
 
Jana Rais alitembelea hospitali yetu ya taifa Muhimbili kumtembelea Mufti mkuu sheikh Aboubakar Zuber, lakini wakati wa safari yake hapo akadakwa na kina mama ambao walikua wakiuguza ndugu zao waliokwishajifungua hospitalini hapo, ndipo Rais alipoamua kuwasikilaza na kuongozana nao hadi wodi ya wazazi na kukuta idadi kubwa ya kinamama wamelala kiholela chini.


Binafsi nimekaa hospitalini hapo muda mrefu sana wakati nikimuuguza kaka yangu aliyekua amelazwa wodi ya mwaisela kiasi kwamba nilifikia mpaka kufahamiana na matabibu wengi na wauguzi na kujihisi kama mwenyeji.
Lakini kwa udukuzi wangu wa mambo ilibidi nijue niñi hua kinaisibu hospitali hiyo mpaka huduma kuzorota?

TATIZO

Ndani ya hospitali hiyo kuna idara nyigi sana na kurugenzi zake ambazo zinawajibika moja kwa moja kwa Mkurugenzi mkuu wa hospitali, lakni cha ajabu ni kwa wakuu wa idara hizi hukalia nafasi zao kwa muda mrefu mfano idara ya uuguzi,tiba, utumishi, fedha,ufundi,maabara,Radiolojia nk, hawa wakuu wa idara wengi wao hawatoi taarifa za kuaminika kwa Mkurugenzi mkuu ili aweze kushughulikia kama kuna matatizo, wamekua wakitoa taarifa za kumridhisha mkurugenzi tu tofauti na uhalisia.Wakuu hawa wa idara zote wamekalia nafasi zao kwa muda mrefu na wengine hujirudia mara kwa mara hali iliyowanya kufanya kazi kwa mazoea na ndio maana fiksi zinakua nyingi.
Kuna mzee mmoja Daktari hospitalini hapo waliniambia kwa mfano kuna idara kama ya ufundi vifaa zinaibiwa sana lakini uongozi uko kimya, idara ya tiba iko kimya ilihali kuna wagonjwa wanafika hospitalini hapo wanatibiwa na kupona lakini wanacheleweshwa kuruhusiwa na kubaki kulipia tu kila siku tu na kusababisha msongamano wodini.


TATIZO LA KINA MAMA KULALA CHINI!


Hapa tatizo liko idara ya tiba ambapo hata wale wagonjwa wasiokua na complicated cases za kupelekwa Muhimbili lakini wanalekwa na kupokelewa badala ya matatizo yao kushughulikiwa hata kwenye vituo vya afya huko, maana wanaopenda Muhimbili wagonjwa wasiostahili kupelekewa pale unategemea wenye hali mbaya wanaostahili kwenda pale wakipokelewa watalala wapi kama sio chini?
Kiingine ni Madaktari kuchelewa kuwaruhusu wagonjwa ambao waliokwisha pona hali inayopelekea wale wapya waokuja kulala chini.

Idara ya fedha nayo inalalamikiwa kwa kujumlishia wagonjwa bili ya gharama kubwa tofauti na gharama halisi alizotumia mgonjwa.


Kwahiyo Rais wangu Magufuli tumbua majipu badili idara zote na kurugenzi zote ndani ya hospitali hiyo! Hiyo kazi hata mawaziri wako wanaweza kufanya maana lasivyo utatwanga maji kwenye kinu miaka yako yote mitano bila mafanikio! Mbona Prof Sarungi aliiweza hospitali ya taifa Muhimbili?
Asante mkuu kwa mchanganuo mzuri nina hakika wahusika watakuwa wanapitapita huku na watalifanyia kazi....siku zote yanatakiwa mawazo kama haya ili kulipeleka taifa letu mbele sio wale wanaofurahia kuona mambo yakienda kombo ili wapate mradi wa kisiasa.....ubarikiwe sana mkuu...
 
Asante mkuu kwa mchanganuo mzuri nina hakika wahusika watakuwa wanapitapita huku na watalifanyia kazi....siku zote yanatakiwa mawazo kama haya ili kulipeleka taifa letu mbele sio wale wanaofurahia kuona mambo yakienda kombo ili wapate mradi wa kisiasa.....ubarikiwe sana mkuu...
Mkuu hii ni nchi yetu sote! Lazima mtu unapokutana na kitu useme ukweli.
 
Jana Rais alitembelea hospitali yetu ya taifa Muhimbili kumtembelea Mufti mkuu sheikh Aboubakar Zuber, lakini wakati wa safari yake hapo akadakwa na kina mama ambao walikua wakiuguza ndugu zao waliokwishajifungua hospitalini hapo, ndipo Rais alipoamua kuwasikilaza na kuongozana nao hadi wodi ya wazazi na kukuta idadi kubwa ya kinamama wamelala kiholela chini.


Binafsi nimekaa hospitalini hapo muda mrefu sana wakati nikimuuguza kaka yangu aliyekua amelazwa wodi ya mwaisela kiasi kwamba nilifikia mpaka kufahamiana na matabibu wengi na wauguzi na kujihisi kama mwenyeji.
Lakini kwa udukuzi wangu wa mambo ilibidi nijue niñi hua kinaisibu hospitali hiyo mpaka huduma kuzorota?

TATIZO

Ndani ya hospitali hiyo kuna idara nyigi sana na kurugenzi zake ambazo zinawajibika moja kwa moja kwa Mkurugenzi mkuu wa hospitali, lakni cha ajabu ni kwa wakuu wa idara hizi hukalia nafasi zao kwa muda mrefu mfano idara ya uuguzi,tiba, utumishi, fedha,ufundi,maabara,Radiolojia nk, hawa wakuu wa idara wengi wao hawatoi taarifa za kuaminika kwa Mkurugenzi mkuu ili aweze kushughulikia kama kuna matatizo, wamekua wakitoa taarifa za kumridhisha mkurugenzi tu tofauti na uhalisia.Wakuu hawa wa idara zote wamekalia nafasi zao kwa muda mrefu na wengine hujirudia mara kwa mara hali iliyowanya kufanya kazi kwa mazoea na ndio maana fiksi zinakua nyingi.
Kuna mzee mmoja Daktari hospitalini hapo waliniambia kwa mfano kuna idara kama ya ufundi vifaa zinaibiwa sana lakini uongozi uko kimya, idara ya tiba iko kimya ilihali kuna wagonjwa wanafika hospitalini hapo wanatibiwa na kupona lakini wanacheleweshwa kuruhusiwa na kubaki kulipia tu kila siku tu na kusababisha msongamano wodini.


TATIZO LA KINA MAMA KULALA CHINI!


Hapa tatizo liko idara ya tiba ambapo hata wale wagonjwa wasiokua na complicated cases za kupelekwa Muhimbili lakini wanalekwa na kupokelewa badala ya matatizo yao kushughulikiwa hata kwenye vituo vya afya huko, maana wanaopenda Muhimbili wagonjwa wasiostahili kupelekewa pale unategemea wenye hali mbaya wanaostahili kwenda pale wakipokelewa watalala wapi kama sio chini?
Kiingine ni Madaktari kuchelewa kuwaruhusu wagonjwa ambao waliokwisha pona hali inayopelekea wale wapya waokuja kulala chini.

Idara ya fedha nayo inalalamikiwa kwa kujumlishia wagonjwa bili ya gharama kubwa tofauti na gharama halisi alizotumia mgonjwa.


Kwahiyo Rais wangu Magufuli tumbua majipu badili idara zote na kurugenzi zote ndani ya hospitali hiyo! Hiyo kazi hata mawaziri wako wanaweza kufanya maana lasivyo utatwanga maji kwenye kinu miaka yako yote mitano bila mafanikio! Mbona Prof Sarungi aliiweza hospitali ya taifa Muhimbili?
Kigwangwala na safari zote zile wagonjwa bado wanalala chini?
Kigwangwala ni jipu pia
 
Muhimbili tatizo ni hospitali ya Taifa
inatakiwa iwe hospitali ya Dar tu
zingine zijengwe kila mkoa au kila kanda
huwezi kuwa na hospitali moja inayotegemewa na watu milioni 50
utegemee huduma bora
 
ngoja tutimue kwanza..
maana tumegundua
siasa ya bongo ni misifa hata kama ni ya kujisaidia barabarani.. roho za watanzania zimejaa kutu ambazo husafika kwa mateso ya ndugu zao..
ila sasahivi wamepoteza nguvu ya kusema hapa kazi tu,sasa hivi hawana hata wa kumpiga mzinga.
 
kama ndivyo basi Ndg. Rais yuko sahihi kabisa. Kama mkurugenzi unapewa taarifa za uongo ofisini kwako na hufanyi chochote, au huchukui jitihada za kukagua hata kwa kupitapita kwenye vitengo vyako kujiridhisha hali halisi ilivyo basi huna maana. Naamini wakuu wa vitengo wanapangwa na ofisi ya uongozi wa hospitali ukiongozwa mkurugenzi mwenyewe sasa kama kuna tatizo kuna shida gani kuwaweka pembeni?
Nkisema mkurugenzi ama kiongozi mwenye dhamana ananufaika na uzembe huo kwa namna moja ama nyingine ntakuwa nasema urongo? Magufuri anafanya vizuri kabisa, timua wakubwa ambao wameshindwa hata kupanga safu zao za kiutendaji vizuri basi.
 
Tuliwaambia kwamba zile hela zilizosemekana kuwa zimeokolewa na kupelekwa kununulia vitanda ni uongo, watu wakabisha na kumsifia Magu eti amenunua vitanda! Vile vitanda vilikuwa ni vya taasisi ya MOI na vilishawekewa oda muda mrefu, sema tu mzee wa opportunity akapita akafanya kama vile yeye ameagiza! Sasa mbona bado wagonjwa wanalala chini?
 
Jana Rais alitembelea hospitali yetu ya taifa Muhimbili kumtembelea Mufti mkuu sheikh Aboubakar Zuber, lakini wakati wa safari yake hapo akadakwa na kina mama ambao walikua wakiuguza ndugu zao waliokwishajifungua hospitalini hapo, ndipo Rais alipoamua kuwasikilaza na kuongozana nao hadi wodi ya wazazi na kukuta idadi kubwa ya kinamama wamelala kiholela chini.


Binafsi nimekaa hospitalini hapo muda mrefu sana wakati nikimuuguza kaka yangu aliyekua amelazwa wodi ya mwaisela kiasi kwamba nilifikia mpaka kufahamiana na matabibu wengi na wauguzi na kujihisi kama mwenyeji.
Lakini kwa udukuzi wangu wa mambo ilibidi nijue niñi hua kinaisibu hospitali hiyo mpaka huduma kuzorota?

TATIZO

Ndani ya hospitali hiyo kuna idara nyigi sana na kurugenzi zake ambazo zinawajibika moja kwa moja kwa Mkurugenzi mkuu wa hospitali, lakni cha ajabu ni kwa wakuu wa idara hizi hukalia nafasi zao kwa muda mrefu mfano idara ya uuguzi,tiba, utumishi, fedha,ufundi,maabara,Radiolojia nk, hawa wakuu wa idara wengi wao hawatoi taarifa za kuaminika kwa Mkurugenzi mkuu ili aweze kushughulikia kama kuna matatizo, wamekua wakitoa taarifa za kumridhisha mkurugenzi tu tofauti na uhalisia.Wakuu hawa wa idara zote wamekalia nafasi zao kwa muda mrefu na wengine hujirudia mara kwa mara hali iliyowanya kufanya kazi kwa mazoea na ndio maana fiksi zinakua nyingi.
Kuna mzee mmoja Daktari hospitalini hapo waliniambia kwa mfano kuna idara kama ya ufundi vifaa zinaibiwa sana lakini uongozi uko kimya, idara ya tiba iko kimya ilihali kuna wagonjwa wanafika hospitalini hapo wanatibiwa na kupona lakini wanacheleweshwa kuruhusiwa na kubaki kulipia tu kila siku tu na kusababisha msongamano wodini.


TATIZO LA KINA MAMA KULALA CHINI!


Hapa tatizo liko idara ya tiba ambapo hata wale wagonjwa wasiokua na complicated cases za kupelekwa Muhimbili lakini wanalekwa na kupokelewa badala ya matatizo yao kushughulikiwa hata kwenye vituo vya afya huko, maana wanaopenda Muhimbili wagonjwa wasiostahili kupelekewa pale unategemea wenye hali mbaya wanaostahili kwenda pale wakipokelewa watalala wapi kama sio chini?
Kiingine ni Madaktari kuchelewa kuwaruhusu wagonjwa ambao waliokwisha pona hali inayopelekea wale wapya waokuja kulala chini.

Idara ya fedha nayo inalalamikiwa kwa kujumlishia wagonjwa bili ya gharama kubwa tofauti na gharama halisi alizotumia mgonjwa.


Kwahiyo Rais wangu Magufuli tumbua majipu badili idara zote na kurugenzi zote ndani ya hospitali hiyo! Hiyo kazi hata mawaziri wako wanaweza kufanya maana lasivyo utatwanga maji kwenye kinu miaka yako yote mitano bila mafanikio! Mbona Prof Sarungi aliiweza hospitali ya taifa Muhimbili?
E ni jipu na usitudanganye kuwa ulikuwa unamhudumia ndugu yako,wewe ni daktari na ni mmoja wa wanaoharibu uzuri wa MNH na zaidi ya hapo ilikosa madaraka ndo maana una kijeba cha roho.
 
E ni jipu na usitudanganye kuwa ulikuwa unamhudumia ndugu yako,wewe ni daktari na ni mmoja wa wanaoharibu uzuri wa MNH na zaidi ya hapo ilikosa madaraka ndo maana una kijeba cha roho.
Mkuu Mimi fani yangu ni mwalimu na mwandishi sio daktari na wala sina utaalam wowote wa afya, ni nexpert member sana humu! Wengi wanamjua. Ila Mimi hua nikienda mahali nina tabia ya kulifanyia utafiti jambo mpaka nilijue ukizingalltia nimemuguza ngugu yangu hapo muda mrefu nimepata marafiki wengi wataalamu.Niliyoyapewa ndio hayo na nimetoa maomi tu.
 
Mkuu MAHANJU;
Umesema mengi sana lakini nakuunga mkono hilo la wamama wasio na complications kukubaliwa kuja kujifungulia hapo. Sasa hii hospitali imekuwa badala ya kituo cha afya?? Hakuna daktari mwenye akili timamu atakaye thubutu kumrudisha mja mzito kuwa aende kwingine. Sasa hao mama zetu wanakimbilia Muhumbili hata kama hana tatizo. Wamama jihurumieni wenyewe. Muhumbili iwe kweli n Referal Hospital si kituo cha Afya.
Serekali, iongeze hadhi ya vituo vya afya vinavyoizunguka Muhumbili. Daktari akipiga sim huko akaambiwa kuna nafasi awapeleke wamama wengine huko kujifungua.
Wapeni wananchi haswa wamama elim watafurahia pia kujifungulia nje ya Muhumbili
 
ushauri mzuri mkuu,
watafutwe watu wenye mizigo mioyoni mwao juu ya umaskini na hali mbaya ya tanzania.

Ila kabla ya kuwafukuza hao watendakazi waliothiliwa na mifumo mibovu iliyopita, wanaweza kupewa nafasi ya pili.
Lakini Magufuli anapaswa kuwapa Mawaziri KPI na inatakuwa kuwa distributed hadi level za watendaji wadogo.
wote watakaocheza nje ya hapo nafasi zao zinatangazwa wanatafutwa watu wengine, nchi imejaa vijana wakiume na wakike wanatembea na bahasha maofisini kusaka hata ukarani, wapewe nafasi wengine ila baada ya kupewa vipimo vipya vya utendaji na kushindwa kuleta matokeoo yenye tija.
 
Mkuu MAHANJU;
Umesema mengi sana lakini nakuunga mkono hilo la wamama wasio na complications kukubaliwa kuja kujifungulia hapo. Sasa hii hospitali imekuwa badala ya kituo cha afya?? Hakuna daktari mwenye akili timamu atakaye thubutu kumrudisha mja mzito kuwa aende kwingine. Sasa hao mama zetu wanakimbilia Muhumbili hata kama hana tatizo. Wamama jihurumieni wenyewe. Muhumbili iwe kweli n Referal Hospital si kituo cha Afya.
Serekali, iongeze hadhi ya vituo vya afya vinavyoizunguka Muhumbili. Daktari akipiga sim huko akaambiwa kuna nafasi awapeleke wamama wengine huko kujifungua.
Wapeni wananchi haswa wamama elim watafurahia pia kujifungulia nje ya Muhumbili
Mkuu hii tabia inaendekezwa na watumishi wasiokua waaminifu, sidhani kama mtumishi mwenye uelewa wa fani yake anaweza kupokea wagonjwa tu bila utaratibu, nafikiri wataalamu wa afya wanajua ni yupi wa kwenda Muhimbili na kwa tatizo lipi! Hapa kuna tatizo tu ndo maana nalaumu sana tu idara ya tiba.
 
E ni jipu na usitudanganye kuwa ulikuwa unamhudumia ndugu yako,wewe ni daktari na ni mmoja wa wanaoharibu uzuri wa MNH na zaidi ya hapo ilikosa madaraka ndo maana una kijeba cha roho.
Bila shaka wewe ndie uliyetembea kwa Miguu kutoka Mwanza kuja kumsalimia Magu
 
Mahanju umeeleweka Kwa hiyo hapo Muhimbili yabidi Mhe Raid awake timu maalum kufuatilia matatizo hapo.
 
Mkuu hii tabia inaendekezwa na watumishi wasiokua waaminifu, sidhani kama mtumishi mwenye uelewa wa fani yake anaweza kupokea wagonjwa tu bila utaratibu, nafikiri wataalamu wa afya wanajua ni yupi wa kwenda Muhimbili na kwa tatizo lipi! Hapa kuna tatizo tu ndo maana nalaumu sana tu idara ya tiba.

Mkuu MAHANJU:
Kama unataka kibarua kiote majani kabla ya jua kutua, kataa kumhudumia mama mjamzito. Yaani ni kama kukalia kiti cha mh. rais alicho andaliwa kukaa ili ahutubie taifa.
Hao wamama ni moto wa kuotea mbali. Na wanavyojua kukutafutia lawama usiombe kabisaaaa. Wamama hao waelimishwe kuwa sio sifa tena kujifungulia Muhumbili. Wakiamini hivyo, hutakaa uone foleni pale
 
Suluhisho siyo matamko ya zima moto,panahitajika maboresho makubwa ya maslahi ya wauguzi na Doctors kwa upande mmoja na ununuzi wa vifaa tiba vya kutosha.
 
Back
Top Bottom