Rais Magufuli anafanya siasa za maendeleo bila kubagua

JPM hafanyi siasa za ubaguzi, bali anafanya siasa za maendeleo kwa mustakabali wa taifa

Na Hamis Shimye

KUMEKUWEPO na kampeni ya kitoto kwenye mitandao ya kijamii inayoongozwa na viongozi wa vyama vya upinzani nchini ambavyo vinadai Rais Dk. John Magufuli ni mbaguzi, ambapo wanafanya hayo ili waweze kuungwa mkono na hatimaye kupata kura za huruma kwa wananchi kwa hoja za kubumba zisizokuwa na mashiko.

Kabla ya kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020, wapinzani wameanza kuonekana kuishiwa hoja na badala yake wamekuwa watu wa kudandia matukio na kumzushia uongo na uzandiki hata pale anapokuwa anataniana na mtu wao wanaichukulia ni kauli rasmi ya Rais wakati sio kweli huku wakishindwa kung'amua ukweli wake kuwa anafanya maendeleo kwa ajili ya jamii nzima ya watanzania.

Mambo makubwa aliyoyafanya Rais Dk. Magufuli katika kipindi cha miaka mitano angekuwa MBAGUZI angeyafanyia nyumbani kwake, leo mkoani Kigoma pekee kuna barabara lukuki, amesaidia wakulima wa michikichiki, kuna mradi wa Uwanja wa Ndege unataka kuanza, kuna vituo vya afya na Hospitali zinajengwa huku barabara nazo wakandarasi wako 'site'. Huu ni ubaguzu gani wanaomzungumzia Rais anautenda?.

Rais Dk. Magufuli amefanya makubwa katika kipindi chake chote cha awamu ya kwanza kinachokwenda kumalizika na ametoa shahuku kubwa ya kuendelea kupigiwa kura za kishindo kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba, ambao ameshaumaliza mapema kutokana na utendaji kazi wake na si kwa porojo ya UBAGUZI wanayoiaminisha wapinzani ambao hawana maono na uthubutu.

Uimara na uthubutu wake, ndio unafanya kuwa moja ya sababu kuu ya Rais Dk. Magufuli kupata kura nyingi na za kishindo kwenye uchaguzi mkuu unaokuja kwa kuwa amekuwa kiongozi mwanamageuzi mwenye kuleta maendeleo makubwa kwa taifa na hata kuipeleka nchi kwenye uchumi wa kati, ambapo kwa jitihada zake amekuwa mkombozi kwa taifa ambalo lilikuwa linanyonywa kwa kiasi kikubwa na hatatengeneza TABAKA lolote kwa mtu yeyote kwa kuwa amekuwa na sera ya UMOJA na sio UBAGUZI.

Dk. Magufuli amekuwa msaada tosha kwa nchi hasa kutokana na kuitoa nchi kiuchumi kutoka asilimia 6.2 hadi asilimia 6.9 kwa mwaka huu, ambapo ameweza kuboresha huduma za kijamii kwa kiwango kikubwa na hata kuondoa umasikini kwenye kaya mbalimbali maeneo yote ya nchi kuanzia Lindi, Mtwara hadi Kilimanjaro huko kote kuna miradi mikubwa ya serikali inatekelezwa.

Rais Dk. Magufuli ameshamaliza uchaguzi mapema kutokana na kuwa kiongozi anayetatua shida za wananchi wake waliompa kura na ndio maana amekuwa akikerekwa na umaskini wao na sio kitu kingine na sababu hiyo ndiyo inayompa ushindi wa kura nyingi za NDIYO Rais Dk. Magufuli katika uchaguzi huu kwa kuweza kusambaza umeme kwenye vijiji vyote nchini na kuwa historia kubwa ambao hadi sasa vijiji 9112 vina umeme wa uhakika na hata kuondoa matatizo ya kukosekana kwa umeme ambao baadhi yao toka tulipopata Uhuru walikosa kupata umeme wa uhakika. Sasa hapo amefanya UBAGUZI gani?

Pia, kumekuwepo na mafanikio makubwa kwenye sekta ya viwanda, ambayo ilikuwa ni msingi wake mkuu wakati wa uchaguzi mkuu wa 2015 ambayo aliahidi kufufua viwanda na amefanikiwa kwa viwanda 61,110 kupatikana katika kipindi cha miaka mitano na kufanya kuwepo na msingi mkubwa kuelekea uchumi wa kati 2025, ambapo viwanda vipo kwenye kila mkoa huku Pwani ikiwa inaongoza. Je tuwaulize wapinzani makanjanja huo ni UBAGUZI wa Rais ambaye anatoka Kanda ya Ziwa anayepeleka maendeleo Pwani?

Kukua kwa mapato kutoka sh Bilioni 850 kwa mwezi mwaka 2015 hadi Sh Trilioni 1.3 kwa mwezi mwaka 2020 ni hatua moja kubwa kwa taifa kupiga hatua kubwa kimaendeleo na hata kuondokana na umaskini ambapo Rais Dk. Magufuli amesimamia nchi kujiendesha kimapato na kuondokana na umaskini huku mapato hayo yakiwa wazi na matumizi yake yanaonekana kwa taifa huku yakitumika kwa shughuli za maendeleo bila ubaguzi wowote.

Wapinzani wanapaswa kutambua uongo na maneno ya kitapeli wanayoyatoa hayana uwezo wa kubadilisha fikra na mawazo ya watanzania kumpa kura Rais Dk. Magufuli kwa kuwa sababu kubwa inayofanya kupewa kura nyingi za NDIYO zinatokana na utendaji kazi wake uliotukuka na hata kuwa na matumaini makubwa kwa watanzania ambao amewatendea haki katika kuleta mapinduzi ya kimkakati katika nchi ya Tanzania bila UBAGUZI wowote.

Amefanikiwa kupunguza umasikini kutoka asilimia 28.2 kwa mwaka 2015 hadi asilimia 26.4 kwa mwaka 2020, ambapo hayo yametokana na uthubutu wa utendaji kazi wa Rais Dk. Magufuli kutumia rasilimali zilizopo katika kuleta maendeleo kwa taifa na 2020 ni sehemu ya yeye kupewa kura za heshima za NDIYO kama shukurani za Watanzania ambao wanaongozwa kwa USAWA na bila UBAGUZI wowote.

Rais Dk. Magufuli amefanya makubwa ikiwemo ujenzi wa miradi ya kimkakati kwa fedha za ndani ikiwemo reli ya kisasa ya standad gauge, ununuzi wa ndege mpya kwa ajili ya Shirika la Ndege ATCL na ujengaji wa bwawa la umeme la Mwalimu Julius Nyerere. Haya ni matunda ya kuwa na rais mwenye maono ya kuleta maendeleo kwa taifa letu na asiye kuwa na UBAGUZI kama wanauhubiri wapinzania uchwara.

Chemchem ya mafanikio haya yanapaswa kuenziwa kwa kila mtanzania na heshima pekee anayopaswa kupewa Rais Dk. Magufuli ni kura nyingi za NDIYO ambazo zitakuwa chachu ya kuendelea kutupa maendeleo makubwa watanzania ambao awali ilikuwa ndoto kuyapata maendeleo hayo hasa kutokana na urasimu uliokuwepo ambapo jamii ilikuwa inakosa kupata maendeleo kutokana na ubabaishaji uliokuwepo.

Uthubutu na utayari wake wa kuwatumikia watanzania ni sifa moja kuu ya Rais Dk. Magufuli kuwa ni mzalendo namba moja mwenye shahuku ya kuwatumikia watanzania kwa moyo wa kizalendo na ndio maana amekuwa mstari wa mbele katika kusimamia maendeleo ya nchi kwa moyo mkubwa licha ya uwepo wa changamoto za wasaliti ambao sasa "wanampakazia" maneno kuwa ni MBAGUZI wakati katika mioyo yao wanaamini kuwa mtu huyu ni jembe lenye kuleta maendeleo kwa jamii.

Oktoba 2020 ni wakati wa kwenda kutoa shukuran za dhati kwa Rais Dk. Magufuli juu ya utendaji kazi wake kwa watanzania ambapo amejitoa kwa hali na mali kwenye shida na kwenye tanuri la moto pale mabeberu walipotaka kutukwamisha kwa maslahi yao yeye alisimama imara kama askari shupavu namba moja kwenye kuleta maendeleo ya taifa la Tanzania na wala si mzandiki kama walivyo wanasiasa wa UPINZANI.

Kwa mantiki hiyo, huu ni wakati wa kila mtanzania siku ya uchaguzi kwenda kumpa kura nyingi za NDIYO Rais Dk. Magufuli kama ishara ya kumshukuru kwa kuonyesha vitendo tafsiri ya kiongozi imara na mwenye maono makubwa kwa taifa letu la Tanzania katika kuleta maendeleo kwa kila mwananchi na bila UBAGUZI wowote ule kama wanavyoeneza wanasiasa wa upinzani waliofilisika sera za kuzungumza kwa jamii.

Maendeleo hayana chama.

Chagua ccm ili upate maendeleo.

Kauli mbili za Magufuli zinazokinzana.
 
Uzuri wa Magufuli ubaguzi wake anauobesha hadharani bila chenga. Anautangaza mwenyewe majukwani kweupeee ili waimba pambio wake mpate tabu zaidi kumtetetea. Ni sawa na kumtetea shetani kuwa hana dhambi
 
Back
Top Bottom