MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,171
- 23,996
Wakati wa utawala wa Rais Kikwete, tulikuwa tunaaminishwa kuwa ni Rais dhaifu asiyechukua maamuzi.
Kila kashfa iliyokuwa ikitokea nchini alibebeshwa Rais Kikwete na kudaiwa hachukui maamuzi kama Rais wa nchi ili kuzuia kashfa mbali mbali. Hata Lowassa mpaka leo anajitetea na kusema, kashfa ya Richmond anaifahamu vizuri Rais Kikwete.
Waeneza propaganda hawakutaka kutuambia kama Rais Kikwete ameziacha taasisi zifanye kazi zake kwa sababu kama wangesema hivyo basi hata hoja yao ya kusema Rais ni dhaifu ingekuwa haina nguvu.
Kimantiki, waeneza propaganda walikuwa wanatuambia Rais Kikwete lazima awe ‘’one man show’’ ili kuhakikisha kashfa hazitokei nchini. Kosa la Rais Kikwete lilikuwa ni kuziacha taasisi za nchi zifanye maamuzi yake bila kuingiliwa na taasisi ya Rais.
Uamuzi wa Rais Kikwete uliwawezesha waeneza propaganda kupata hoja mbali mbali za kisiasa ambazo zilikuwa zinasababishwa na uwepo wa taasisi/idara legelege.
Leo hii waeneza propaganda wamebadilisha tena malengo yao baada ya malalamiko yao kujibiwa kimatendo na wameanza kutuaminisha Rais Magufuli ni ‘’one man show’’ na kwa sababu hiyo wanataka taasisi au idara za serikali zisiingiliwe na taasisi ya Urais katika utendaji kazi wake.
Tulimsikia Tundu Lissu akisema bora wakati wa utawala wa Rais Kikwete kwa sababu hakuziingilia taasisi katika maamuzi yake.
Kwa maana nyingine wapiga propaganda wanatuambia Rais Magufuli lazima awe kama Rais Kikwete ili nchi irudi kwenye kashfa zinazosababishwa na uwepo wa taasisi/idara legelege zilizosababisha kashfa kama za Richmond,Dowans,Kagoda,Meremeta,Escrow, nk.
Ikumbukwe ni hawa hawa kwa miaka zaidi ya nane walituambia kuwa Lowassa ni fisadi na hafai kuwa Rais wa Tanzania lakini kilichotokea baadaye kinafahamika.
Ibara ya 33(1-4) ya Katiba ya Tanzania inasema,
33-(1) Kutakuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano.
(2) Rais atakuwa Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.
(3) Mamlaka yote ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano juu ya mambo yote ya Muungano katika Jamhuri ya Muungano, na pia juu ya mambo mengineyo yote yahusuyo Tanzania Bara, yatakuwa mikononi mwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
(4) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii, madaraka ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano yatatekelezwa ama na Rais mwenyewe moja kwa moja au kwa kukasimu madaraka hayo kwa watu wengine wenye madaraka katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Ukichambua kwa undani utagundua Ibara ya 33(1-4) ndiyo imebeba nguvu na madaraka ya Rais wa Tanzania.
Hii ibara haikuwekwa kwa bahati mbaya bali waliyoiweka walifahamu vizuri muundo wa nchi ambao unachagizwa na uwepo wa taasisi/idara ambazo ni legelege.
Kama Rais Magufuli atakubaliana na kelele za wale wanasema hawataki Rais ambaye ni ‘’one man show’’ basi ajiandae pia kutumbukia kwenye kashfa mbali mbali kama ilivyotokea kwa Rais Kikwete.
Rais Magufuli lazima ayakumbuke pia maneno ya Mwl. Nyerere aliposema, ‘’mtu yeyote mwenye akili timamu akikupa mawazo ya kipumbavu na wewe una akili timamu na unajua ni ya kipumbavu na ukayakubali, atakudharau’’.
Kila kashfa iliyokuwa ikitokea nchini alibebeshwa Rais Kikwete na kudaiwa hachukui maamuzi kama Rais wa nchi ili kuzuia kashfa mbali mbali. Hata Lowassa mpaka leo anajitetea na kusema, kashfa ya Richmond anaifahamu vizuri Rais Kikwete.
Waeneza propaganda hawakutaka kutuambia kama Rais Kikwete ameziacha taasisi zifanye kazi zake kwa sababu kama wangesema hivyo basi hata hoja yao ya kusema Rais ni dhaifu ingekuwa haina nguvu.
Kimantiki, waeneza propaganda walikuwa wanatuambia Rais Kikwete lazima awe ‘’one man show’’ ili kuhakikisha kashfa hazitokei nchini. Kosa la Rais Kikwete lilikuwa ni kuziacha taasisi za nchi zifanye maamuzi yake bila kuingiliwa na taasisi ya Rais.
Uamuzi wa Rais Kikwete uliwawezesha waeneza propaganda kupata hoja mbali mbali za kisiasa ambazo zilikuwa zinasababishwa na uwepo wa taasisi/idara legelege.
Leo hii waeneza propaganda wamebadilisha tena malengo yao baada ya malalamiko yao kujibiwa kimatendo na wameanza kutuaminisha Rais Magufuli ni ‘’one man show’’ na kwa sababu hiyo wanataka taasisi au idara za serikali zisiingiliwe na taasisi ya Urais katika utendaji kazi wake.
Tulimsikia Tundu Lissu akisema bora wakati wa utawala wa Rais Kikwete kwa sababu hakuziingilia taasisi katika maamuzi yake.
Kwa maana nyingine wapiga propaganda wanatuambia Rais Magufuli lazima awe kama Rais Kikwete ili nchi irudi kwenye kashfa zinazosababishwa na uwepo wa taasisi/idara legelege zilizosababisha kashfa kama za Richmond,Dowans,Kagoda,Meremeta,Escrow, nk.
Ikumbukwe ni hawa hawa kwa miaka zaidi ya nane walituambia kuwa Lowassa ni fisadi na hafai kuwa Rais wa Tanzania lakini kilichotokea baadaye kinafahamika.
Ibara ya 33(1-4) ya Katiba ya Tanzania inasema,
33-(1) Kutakuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano.
(2) Rais atakuwa Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.
(3) Mamlaka yote ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano juu ya mambo yote ya Muungano katika Jamhuri ya Muungano, na pia juu ya mambo mengineyo yote yahusuyo Tanzania Bara, yatakuwa mikononi mwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
(4) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii, madaraka ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano yatatekelezwa ama na Rais mwenyewe moja kwa moja au kwa kukasimu madaraka hayo kwa watu wengine wenye madaraka katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Ukichambua kwa undani utagundua Ibara ya 33(1-4) ndiyo imebeba nguvu na madaraka ya Rais wa Tanzania.
Hii ibara haikuwekwa kwa bahati mbaya bali waliyoiweka walifahamu vizuri muundo wa nchi ambao unachagizwa na uwepo wa taasisi/idara ambazo ni legelege.
Kama Rais Magufuli atakubaliana na kelele za wale wanasema hawataki Rais ambaye ni ‘’one man show’’ basi ajiandae pia kutumbukia kwenye kashfa mbali mbali kama ilivyotokea kwa Rais Kikwete.
Rais Magufuli lazima ayakumbuke pia maneno ya Mwl. Nyerere aliposema, ‘’mtu yeyote mwenye akili timamu akikupa mawazo ya kipumbavu na wewe una akili timamu na unajua ni ya kipumbavu na ukayakubali, atakudharau’’.