Rais Kikwete kwenye ziara ya kiserikali nchini Ufaransa

Mbona taarifa haijitoshelezi,haina list kamili ya alioandamana nao?
 
Aibu gani hii watanzania tunayotwikwa ameshindwa kushughulikia sakata la mtwara huyoooooo kiguu na njia.

------ hataki taabu, akiona kuna matatizo huyoooo anakwea pipa anakwenda kutalii anawaacha wadanganyika wanaandamana kulilia gesi!!
 
Nilitaka kushangaa asiende Davos,maswali ya msingi.
1.Kwanini anatumia Swiss air?ndege ya serikali imekuwaje?
2. Wametuambia watuL atakaokutana nao lakini madhumuni ya yeye kukutana nao ni nini?
3. Kurugenzi ya mawasiliano mnaposema raisi ataendelea na ratiba ngumu katika siku ya pili mnamanisha nini?au ni ujumbe gani mnatupatia?kama ni ngumu nani kampangia?na baada ya nyie kiliona Hilo umechukua hatua gani?
4. Vipi Mmemwandaa kujibu maswali ya wanahabari huko ulaya kihusu Ile ripoti ya watu wa haki za binadamu?asije tokwa na povu kama Canada.
Mwenye majibu plz
Labda anataka kuzuga kuwa anapunguza gharama.

Sijui nafsi yake inamsuta?
 
Anapokelewa na waziri wakati yeye ni Rais..ila Hollande akija hapapiga ua yeye Mwenyewe atakuepo Airport!!
 
Umenona NIMELALAMIKA??? kwanini WAJIHAMI?

Alaa sasa mbona wewe ndiye unayejihami? mkuu nngu007 lugha za kishairi zinaeleweka ni tangu lini unaweka jema la mh. kikwete mpaka leo nishangae?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli hasa ikizingatiwa kuwa wanaoongozana nae wengi wanatia aibu licha ya hasara. Unategemea nini kwa mtawala wa kiswahili asiyezingatia ethics? Usishangae kuna akina mashangshaazi watoto wa mjomba na mashoga wa mkewe wanaokwenda kushangaa shangaa na kufanya shopping uchwara. Namna hii kwanini deni la taifa lisiumke?

Mbona umewashau waganga?
 
Great mind discuss ideas,simple mind discuss events and low mind discuss people
 
Hilo tangazo la Ikulu lina kasoro nyingi sana. Binafsi natilia shaka kama kweli Kikwete amealikwa na Rais wa Ufaransa. Shaka yenyewe iko kuanzia kwenye mapokezi na nafasi za watu atakaokutana nao pamoja na taasisi atakazotembelea. Nahisi hapo amejipenyeza tu (amezuga) kwa muda lakini safari halisi ni kwenda Davos Uswisi kwenye huo mkutano wa World Economic Forum.

Lakini kwenye hilo tangazo hata pasipo kuumiza kichwa, kwa ujumla limekosa umakini katika uandishi. Kwanza kitu kama MTENDAJI MKUU WA MFUKO PRIVATE FUND na SHIRIKA LA UCHUMI DUNIANI (WEF)ni taasisi ambazo hazipo na ukiambiwa maandishi kama hayo yameandikwa na mtu anayefanyakazi IKULU hiyo ni aibu kwa Taifa. Tangu lini World Economic Forum (WEF) ikawa Shirika la Uchumi Duniani. WEF ni kongamano linalokutanisha watu mbalimbali kujadili masuala ya kiuchumi duniani. Ama ukiwauliza hao watu wa Ikulu Mfuko Private Fund uko wapi na unaendeshwaje sijui watajibu nini. Hata hilo jina la huyo mtendaji inaonekana limekosewa.

Ni muhimu kuwa makini katika mambo ya msingi japo kwa wengine wanaona ni mambo madogo, kwa wenzetu unapokosea japo herufi moja kwenye jina la mtu inaweza ikaleta madhara makubwa sana
 
Hana faida yoyote kwa nchi hii!!!!!!! Ameenda kuhamisha 10% yake ya Uswis maana anajua chochote chaweza kutokea!!!
 
Hilo tangazo la Ikulu lina kasoro nyingi sana. Binafsi natilia shaka kama kweli Kikwete amealikwa na Rais wa Ufaransa. Shaka yenyewe iko kuanzia kwenye mapokezi na nafasi za watu atakaokutana nao pamoja na taasisi atakazotembelea. Nahisi hapo amejipenyeza tu (amezuga) kwa muda lakini safari halisi ni kwenda Davos Uswisi kwenye huo mkutano wa World Economic Forum.

Lakini kwenye hilo tangazo hata pasipo kuumiza kichwa, kwa ujumla limekosa umakini katika uandishi. Kwanza kitu kama MTENDAJI MKUU WA MFUKO PRIVATE FUND na SHIRIKA LA UCHUMI DUNIANI (WEF)ni taasisi ambazo hazipo na ukiambiwa maandishi kama hayo yameandikwa na mtu anayefanyakazi IKULU hiyo ni aibu kwa Taifa. Tangu lini World Economic Forum (WEF) ikawa Shirika la Uchumi Duniani. WEF ni kongamano linalokutanisha watu mbalimbali kujadili masuala ya kiuchumi duniani. Ama ukiwauliza hao watu wa Ikulu Mfuko Private Fund uko wapi na unaendeshwaje sijui watajibu nini. Hata hilo jina la huyo mtendaji inaonekana limekosewa.

Ni muhimu kuwa makini katika mambo ya msingi japo kwa wengine wanaona ni mambo madogo, kwa wenzetu unapokosea japo herufi moja kwenye jina la mtu inaweza ikaleta madhara makubwa sana

Baba mwenye nyumba sio makini, utategemeaje watoto wawe makini?
 
Kati ya Kikwete, Obama na Cameron nani ana risk kubwa ya kushambuliwa. Mbona Cameron akienda nje (kutoa Afgan na Iraq) nchi inajulishwa anaenda wapi na wajumbe gani? Vile vile Obama anapotembelea nchi nyingine kwa ziara ya kiserikali nchi inajulishwa anaambatana na nani. Ni usalama gani anaogopa Kikwete?

Mkuu, katika ziara zao zote Obama na Cameron walipokuwa wanaenda Afghanstan na Iraq na taarifa hazikutolewa mpaka walipotua sehemu hizo na pia wanapomaliza ziara hizo ambazo huwa ni za ghafla walipoondoka haikutangazwa.

Nao pia ni binadamu na wana wanaogopa kufa ingawa kifo chaweza kutokea wakati wowote.
 
Kwa mujibu wa ratiba, kesho, Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo na Mama Frannie Leautiera mbaye ni Mtendaji Mkuu wa Mfuko Private Fund.


Huyu mama ni mtaalam wa mambo mengi ikiwemo umeme utokanao na vyanzo za asili hasa gesi.

Sasa nafikiri kuna muunganisho unafanywa ili mheshimiwa raisi apate elimu kuhusu nishati itokanayo na gesi kwamba Ufaransa wanao utaalam huo na wapo tayari kutoa semina ya siku mbili tatu kuhusu gesi na namna inavyodhibitiwa.

Kama inavyoeleweka kwamba suala la gesi Mtwara bado linasumbua vichwa kwahio zinafanywa jitihada za nguvu kutatua tatizo hilo. Hivyo kuna uwezekano wa kupata mwekezaji ambae atasaidiana na aliepo Tanzania katika kuzalisha gesi na kudhibiti eneo la uzalishaji.

Kwahio raisi na timu yake (katika siku chache hizo) watajifunza namna ya kutengeneza masoko ya nishati hiyo, mfumo wa biashara hiyo na matatizo yatokanayo na uzalishaji wa nishati hiyo.

Kwahio inawezekana wakaenda pale University of Electricité de France kufanya semina hiyo na huyu mama inawezekana ndie anaeratibu sehemu ya ziara hiyo.

Nafikiri kale kainzi ketu katanisaidia kwa taarifa zaidi.
 
Kwa taarifa ya Ikulu hapa chini, pia nimeweza kupata Mawaziri watatu (Prof.Sospeter Muhongo, Dr. John Magufuli na Bernard K Membe)watakaoambatana na Rais Kikwete ziara yake ya Ufaransa na Uswisi kama ilivyoelezewa. Nimeona nitaje hao Mawaziri kwa vile taarifa ya Ikulu haikuwa wazi ni viongozi wapi kaandamana nao ukiachia mbali na Mama Salma Kikwete ( First Lady) na mashushushu wake!

Swali kwangu ni kama ziara hii itakuwa na tija kwa Taifa. Nimeona ziara nyingi za Kikwete but huwa sipati vizuri matunda yake!!



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS


Telephone: 255-22-2114512,2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com / press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,DAR ES SALAAM
Tanzania

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RAIS wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anaanza ziara rasmi ya Kiserikali nchini Ufaransa leo, Jumamosi, Januari 19, 2013, kwa mwaliko wa Rais wa Ufaransa, Mheshimiwa Francois Hollande.

Rais Kikwete na ujumbe wake aliondoka nchini usiku wa kuamkia leo, Jumamosi, kwa ndege ya Shirika la Ndege la Uswisi kuelekea Ulayakwa ajili ya ziara hiyo.

Mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Charles DeGaul mjini Paris leo jioni, Rais Kikwete ambaye anafuatana na Mama Salma Kikwete atapokelewa rasmi katika Ufaransa kwa gwaride nakupokelewa na Waziri wa Misaada ya Maendeleo wa Ufaransa, Mheshimiwa Paschal Canfin.

Kwa mujibu wa ratiba, kesho, Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo na Mama Frannie Leautiera mbaye ni Mtendaji Mkuu wa Mfuko Private Fund na baadaye atakutana na Mama Marie Christine Saragosse, Mtendaji Mkuu wa Redio France International (RFI).

Mkutano huo utafuatiwa na kikao kati ya Rais Kikwete na Jumuiya yaWatanzania wanaoishi nchini Ufaransa.

Keshokutwa, Jumatatu, Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Francois Hollande, Rais wa Ufaransa kwenye Kasri ya nchi hiyo ya Elysee Palace.

Mazungumzo kati ya Rais Kikwete na Rais Hollande yatafuatiwana chakula cha mchana ambako Rais Kikwete atakaribishwa na Waziriwa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Mheshimiwa Laurent Fabius. Baada ya chakula hicho cha mchana, Rais Kikwete atakutana na kuzungumza na Bwana Yves Louis Darricarere, Rais wa Kampuni ya Mafuta yaKimataifa ya Total.

Mazungumzo hayo yatafuatiwa na mazungumzo mengine kati yaRais Kikwete na Kiongozi wa Madhehebu ya Ismailia Duniani H.H TheAga Khan na baada ya hapo, Rais Kikwete atakwenda Kasri la Luxemburg kukutana na kuzungumza na Rais wa Bunge la Seneti la Ufaransa, Mheshimiwa Jean Pierre Bel.

Usiku wa Jumatatu, RaisKikwete atakula chakula cha usiku naRais wa zamani wa Ufaransa, Mheshimiwa Valery Giscard d’Estaingambaye ni Mwenyekiti waTanzania Wildlife Conservation Foundation. Jumanne, Rais Kikwete atakuwa na siku nyingine yenye shughuli nyingi ambako miongoni mwa mambo mengine atakutana nakufanya mazungumzo na mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zaokatika Ufaransa, na atakutana na Mheshimiwa Abdou Diouf, KatibuMkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Nchi Zinazongumza Lugha yaKifaransa na Rais wa zamani wa Senegal.

Rais Kikwete pia atashiriki majadiliano kuhusu masuala yakimataifa yaliyoandaliwa na Taasisi ya Mahusiano ya Kimataifa yaUfaransa – Institute Francais Des Relations International (IFRI) naatakutana na kuzungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika laMaendeleo ya Kimataifa la Ufaransa (AFD).

Rais Kikwete ataondoka nchini Ufaransa Jumatano, Januari 23,2013, kwenda Uswisi ambako atatembelea Makao Makuu ya Shirikishola Soka Duniani (FIFA) mjini Zurich na baadaye kwenda Davoskuhudhuria mkutano wa mwaka huu wa Shirika la Uchumi Duniani – World Economic Forum (WEF).

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
Dar es Salaam.
19 Januari, 2013
 
Back
Top Bottom