Rais Kikwete kustaafu rasmi Novemba 5, 2015

Rais Kikwete kustaafu rasmi Novemba 5, 2015

Mapengo 17

R I P
Joined
Mar 28, 2014
Posts
1,228
Reaction score
618
RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa atastaafu rasmi kama Rais wa Nne wa Jamhuri ya Muungano Alhamisi ya Novemba 5, mwaka huu, wakati Rais mpya na wa tano atakapoapishwa.

Aidha, Rais Kikwete ambaye jana alipanga foleni kwa kiasi cha takriban dakika 5 pamoja na wapiga kura wengine wa kijiji cha kwao cha Msoga wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani kwa ajili ya kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika jana.

Rais Kikwete akifuatana na Mama Salma Kikwete, aliwasili katika Kituo cha Kupigia Kura cha Hospitali ya Msoga saa 6:21 mchana na kwenda moja kwa moja kwenye foleni ya wapigakura akiwa na watu kiasi cha 12 mbele yake.

Rais Kikwete aliwaambia waandishi wa habari kuwa tarehe yake rasmi ya kustaafu ni Alhamisi ya Novemba 5, mwaka huu, siku 11 kutoka leo, wakati Rais mpya wa Tanzania, Rais wa Tano atakapoapishwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

"Kwa bahati mbaya bado iko mbali na nalazimika kusubiri mpaka Novemba 5, wakati nitakapokabidhi madaraka kwa Rais wetu ajaye" alisema Rais Kikwete.
 
Aende tu.

Ametutia aibu sana huyu mzee.
 
hiyo aibu umetiwa peke yako. wengine tunam-rank kama rais bora kuliko watangulizi wake wote. hatujui tu ajaye kama ataweza kumfunika. pole.

Wewe ni sawa na wananchi anapotokea yeye.

Hakuna elimu wala huduma za jamii.
 
Sitashangaa jamaa kwa siku hizi chache akapiga ka tripu Marekani nakupita kuaga Argentina
 
haijalishi. vumilia tu hata kama inakuuma. siamini hata hiyo elimu unayojinasibu hata kama tunafanana. again pole.

Wewe ni sawa na wananchi anapotokea yeye.

Hakuna elimu wala huduma za jamii.
 
Kila la kheri JK. Mungu akulinde huko mtaani
 
Back
Top Bottom