ukiwa mbumbumbu utabeza, ukiwa kama nyumbu utaliwa na fisi, mamba ,chui na simba bila kujijua.
mh Kikwete ni rais wa aina yake. hembu pitia hapa na kama wewe nigreat thinker basi utakubali bila kubururuzwa.
1. UTAWALA WA SHERIA.
Wengi hawafahamu namna kikwete alivojitahidi kuweka utawala wa sheria. mfano tu sasa hivi kuna magazeti na TV hazisemeki na watu wanapaswa kulitambua. pia haki za binadamu zimeboreshwa na watu wengi hiv sasa wanatambua haki zao ukilinganisha na zamani. Katika utawala wa kikwete Said Mwema aliunda hadi polisi jamii lengo likiwa kulinda haki za binadamu.
:
wapinzani saivi wajipange maandamano ya kipuuzi ndio mwisho. saiv mikutano ya hadhara imezuiliwa na bado polisi watakuwa na zero tolerance kwa wakorofi
2.KUPAMBANA NA RUSHWA NA UBADHIRIFU.
Kikwete alipoingia aliwakamata mawaziri wawili kwa rushwa, wafanyazi wengi sana walikamatwa, ameunda Takukuru kuchunguza wezi, pia kuruhusu CAG kupeleka ripoti yake bungeni. mazuzu wasioelewa hawajui ni jambo kubwa sana alilolifanya rais kikwete kwani ubadhirifu serikalini uliwekwa wazi na wabunge kuchukua hatua.
3.ALIPIGANIA USTAWI NA AMANI YA WAZANZIBAR
Kikwete hakulala alipoona wazanzibar wakigombana wenyewe kwa wenyewe. alisimamia muafak hadi Leo upo. zanzibar a man IPO na wamepiga hatua kubwa na kupunguza mivutano na uhasama.
4. KUANZISHA MCHAKATO WA KATIBA MPYA
Kikwete alifanya jambo la kijasiri kuanzisha mchskato wa katiba mpya ambayo inasubiriwa ipigiwe kura Tanzania kwa miaka 50 ipate katiba mpya
5. KUWAJALI WAPINZANI WAKE
Kikwete alimteua Mh Mbatia kuwa mbunge.lakini shukran ya punda ni mateke.
bila shaka wapinzani na wanaomshutumu Kikwete hawana muda mrefu watamkumbuka kwa mema mengi aliyoyafanya.
let us discuss ideas and issues not people.