Rais Kikwete ana SIRI!

Rais Kikwete ana SIRI!

Hivi kwanini hasikuteuwe uwe hata Msaidizi wa Rais badala ya kumteuwa January au Jairo? naamini kama angekupa U-PS Nishati na Madini kwa maneno haya husinge diriki kuwapa hongo Wabunge kwa ajili ya kupitisha Bajeti hata kama ungekuwa damdam nae labda hapo hatua zinge anza kwenda mbele maana ndipo gari lilipo kwama hapo Mkuu.

Nimejidhiirisha kuwa hata kama angekupa U-waziri kama kuna kosa la kuwajibika husinge katikalia ofisini kama Ngereja na Hussein bin Mwinyi kama watanzania wangepiga kelele ujiuzulu maana hapo pia ndipo panapotukwamisha mara zote Mkuu Ivuga!


Sasa basi nakubaliana nawe kuwa Rais ni wa mwisho katika utendaji lakini ni kwanza na mwisho katika Maamuzi makuu ya kusonga mbele; pale anaposhindwa kuchukuwa hatua basi wananchni wote wanakata tamaa na kuanza kulia maana mkiona kitu kimemshinda Baba basi mjue hakuna jinsi ni kulia tu "NO WAY" Urais pia ni kazi rahisi sana lakini mpaka upate wasaidizi makini na wenyewe uwezo nadhani hapa ndipo alipo kosea mara zote mpaka leo hadi kesho.

Pia Urais unahitaji ujasiri na hata kiapo cha Urais kinatambua hilo lakini pia kama binadamu ujasiri unaweza kupotea pale ambapo wewe mwenyewe umekwisha kujidhalilisha na kushiriki katika mambo ambayo unatakiwa kuyakemea hivyo unapoteza uwezo na ujasiri wa kukemea, maana kama kila siku unagongana na wanao hotelini umelewa na kimada pembeni hakika lazima ukose ujasiri wakuwa kemea juu ya tabia ya ulevi na Uzinzi maana kama ni kinara wewe ni namba moja; hapa pia ndipo palipo mkwamisha Mkuu wetu baada ya kukubali na kujikuta kuingia katika mitego na dili za Ufisadi kwa kusaidia na rafiki zake wakubwa Jairo, EL, RA, & Chenga... ila naona kama hasingefanya kosa ange kuteuwa St. Ivuga labda haya yote yasingetokea, mathalani alipouliza kama hatuna wasomi yeye tokea ameingia madaraka amediri kuwatumia wasomi mara ngapi katika mambo yake au kwake Urafiki unanguvu kuliko Usomi? maswali ni mengi sana ila kwa kifupi alipokosea ndipo hapo hapo wewe unapomsifia nashindwa kukuelewa hata kidogo..........Leo jogoo anawika ndio wanapiga kelele Lowasa ni fisadi lakini haya maneno yalisemwa na Nyerere 1995 bado yeye bila aibu akamteuwa kuwa PM wake? huoni pale alipojikwaa kama huoni basi fumbuwa macho ...

Hatuwezi kufanya na hatuta fanya mambo ambayo si wajibu wa kifamilia, kama unaongea mamabo ambayo ni wajibu wakifamia tunafanya kila siku nandio maana wanapata kodi ya kuiba na kutumia kifisadi wajibu wetu namba moja kwa serikali ni kulipa kodi tunalipa hapo ndipo serikali ingeweza kutulaum lakini kama tuanalipa kodi lakini hanashindwa kuzisimamia na pia anashindwa kuzipangia development priority kwanini hasiondoke ampishe mwingine atakaye weza?!
 
siriziki na uongozi wake hata kidogo .. na siwezi kumkubali Lowasa hata siku moja .. wote hao ni wamoja...lakini kwa nini tutake kutafuniwa kila kitu? Kikwete hana tatizo hata moja.. tatizo ni watanzania and <u><b>even small

kid can prove this i swear</b></u>
<br />
<br />

Mbona unaji-contradict? Hawezi kuwa hana tatizo halafu usiridhike na uongozi wake!
 
<br />
<br />

Mbona unaji-contradict? Hawezi kuwa hana tatizo halafu usiridhike na uongozi wake!
kwani bandiko limebase upande mmoja?...unajua stori ya kalumakenge?...safari moja ilianzisha safari nyingine..
 
kwani mmesahau rais wa nchi hii amepewa kweli mamlaka ya kufikiri badala ya watz. Hamwoni anayoyafanya kwa niaba yenu? Angalia teuzi zake na maamuzi yake kadhaa.
 
Mtaji wa CCM kuwa madarakani ni ujinga na ukondoo wa watanzania,haingii akilini kuwa madhila yote haya km nchi kuwa gizani bado JK na viongozi wa CCM wanaweza kukusanya watu na wakawasikiliza bila japo kuwazomea. CCM KUWA MADARAKANI NI JANGA KUBWA KWA TAIFA HILI.
 
<span style="font-family: arial narrow"><font color="#000080"><font size="4">Sijaona siri yoyote ya ikwete hapa...!!</font></font></span>
<br />
<br />
Labda anataka kuuza nchi. H
 
Thats why there is a leader and a follower,kiongozi akiyumba au akiwa hovyo kama Jakaya lazima wanaoongozwa watayumba na kiongozi akiwa imara kama Kagame lazima wanaongozwa wataimarika,kwa Tanzania labda utulaumu wananchi kwa kutofanya mapinduzi ya kumwaga damu dhidi ya utawala dhaifu usio na malengo wala tija kwa mustakbar wa nchi.
 
Thats why there is a leader and a follower,kiongozi akiyumba au akiwa hovyo kama Jakaya lazima wanaoongozwa watayumba na kiongozi akiwa imara kama Kagame lazima wanaongozwa wataimarika,kwa Tanzania labda utulaumu wananchi kwa kutofanya mapinduzi ya kumwaga damu dhidi ya utawala dhaifu usio na malengo wala tija kwa mustakbar wa nchi.
siwezi kuwalaumu kwa kumwaga damu mtalaumiwa na vizazi vyenu kwa kuirudisha ccm madarakani kwa kupitia box la kura
 
Saint Ivuga,

Binadamu wote hawawezi kufanana na ndio maana mambo yanakwenda hivi tuonavyo, na ndio maana basi;

...walizaliwa ili waolewe na kuishi na waume zao,

...walizaliwa ili waoe na kuishi na wake zao,

Kwahiyo basi, wakuolewa atakapolazimisha kuoa na wakuoa atakapolazimisha kuolewa matokeo yake ndo kama haya!!!!! ni

lazima majukumu yatamshinda na Kila mtu atajua alaaa, kumbe huyu ni wa kuolewa... sasa kwanini jamaa/ndugu zake

waliamua kumpa mke badala ya Mume?
 
Ni article nzuri sana, lakini angalia upande mwingine wa shillingi. Mazingira ya nyumbani ni frustrating, hata mtu angekuwa na PhD 20 baada ya kurudi tanzania ni lazima PhD yake itaota kutu. Nchi ambayo haina sera chanya za kuleta maendeleo unategemea wasomi hao wangefanya miujiza bila kuwezeshwa na serikali. Ukombozi wa kifikra inabidi uanzie kwa viongozi, waache ufisadi na waweke maslahi ya taifa mbele. Rais Kagame ni mfano wa kuigwa, lakini siyo raisi wetu uliyemtaja hapo kwenye article yako, hana hiyo vision.
......tusimjudge rais wetu ama mtu yeyote yule...mayb ana vision lkn peer groups ni kikwazo cha yeye kuwa responcbo....i think he z afraid of his frndz kuwa anastaafu soon.......then akiwasaliti itakuwaje?....our president anahitaji kuwa na more self-confidence...dic z juc a fact
 
Hiyo siyo siri nzito ya Mhe. Rais, haya ni mawazo yako ila umeamua kumsemea Mhe.
Umesema mengi sana. Mengine ni ya msingi, ila yanataka mtu au kiongozi ayasimamie utekelezaji wake.
Ukiwa kiongozi maana yake uwe mbunifu na msimamizi mzuri wa maamuzi uliyo/mliyoyafikia
 
St Ivuga leo nimependa sana thread yako. Huwa napata hasira sana nikiona watu wanatupa taka barabarani or anywhere pasipo takiwa.
We are human beings and not animals. God gave us the ability to think and differentiate the right from wrong.
We should have the ability to see the poor old lady sweeping the road to keep it clean. And some person comes right behind her and drop gamba la ndizi or an empty bottle of maji ya kunywa.
 
St Ivuga leo nimependa sana thread yako. Huwa napata hasira sana nikiona watu wanatupa taka barabarani or anywhere pasipo takiwa.
We are human beings and not animals. God gave us the ability to think and differentiate the right from wrong.
We should have the ability to see the poor old lady sweeping the road to keep it clean. And some person comes right behind her and drop gamba la ndizi or an empty bottle of maji ya kunywa.
bora umeona kuna wengine walianza kunilaumu eti namtetea rasi....sasa sijui hadi mikakati ya kuzoa matakataka barabarani Rais aje ate tamko..
 
Yapo mambo ambayo mwananchi anawajibika kuyafanya,bila msaada wa serikali kwa mtizamo mwepesi,lakini mwisho wa siku hadithi ni ile ile ya Karumekenge alikataa kwenda shule.
 
[h=3]Rais Kikwete ana SIRI![/h]




Kuna siri nzito ambayo mh. JK anayo na ninaamini inamtesa sana. Siri yenyewe ni kama ifutavyo:

Kwamba watu anatuongoza hatutoi msaada kwake. Ninavyoelewa mimi ni kwamba kazi ya Rais sio kufikiri kwa niaba ya watu anaowaongoza. Kazi yake ni kusimamia mahitaji na matakwa ya watu anaowaongoza. Lakini kwa Tz ni tofauti. Kazi ya rais imekuwa ni kufikiri kwa niaba yetu.

Mwl. Nyerere wakati anadai uhuru, aliamini kuwa watanzania ni wanadamu wenye utashi. Akataifisha mali ya wageni na kuwakabidhi wazawa, akiamini tunaelewa kama yeye alivyokuwa. Akatukabidhi viwanda, mashamba, nk. Lakini badala ya kwenda mbele, vikafa. Akashangaa, allah! nilidhani hawa jamaa tu kitu kimoja, kumbe!, akaamua kung'atuka.

Mh. JK akaja na style tofauti. Akasema ngoja niwachokoze, maana siwaelewielewi!
Akaenda kutuombea vyandarua, akiamini kwamba tutalipuka na kusema, haiwezekani, yaani tuombewe vyandarua?! Alitegemea pia kwamba tunatambua kwamba hivyo vyandarua baada ya muda fulani, vitachanika na hivyo tutajiuliza swali, Je! aende kutuombea tena? Lakini cha ajabu, kimyaaa! wote kwa ujumla wetu! Sasa anajiuliza, atumie njia gani ya kutufikishia ujumbe kwamba alitutania/alituchokoza tu ili tuzinduke? Na HATUJAZINDUKA! TUMELALA USINGIZI MZITO! Hivi ni kweli tunafikiri kwamba vikichakaa ataenda tena kutuombea?

Mwanadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu na tumeumbwa tuvitawale viumbe vyote(kulingana na maandiko matakatifu). Je! sisi watz tumo? Kama tumo mbona mbu ametushinda? Utashi wetu uko wapi? Kama malaria ndio inaongoza kwa kuleta vifo hapa nchini, tunashindwa nini kumdhibiti mbu na uchafu?

Ukiangalia mbinu tunazotumia kukabiliana na maradhi, utashangaa kabisa! Kuna jamaa walijenga hospitali ya kipindupindu pale buguruni, ajabu! (sina uhakika, lakini inawezekana ni nchi ya kwanza dunia kukijengea kipindupindu ghala la kuhifadhia badala ya kukikomesha). Watanzania mpo!? Kweli mpo?!

Hivi ni kweli tunajisikiaje, kila rais wetu akikaa na marais wenzake, yeye ni kulia kila siku malaria inatumaliza. Si wanashangaa kwamba nchini kwake hana watu? Ni bahati mbaya wengi wetu huwa hatukai chini tukatafakari. JK amekuwa akiuliza maswali kadhaa ambayotungekuwa makini, yangetuumiza. Mojawapo aliwahi kusema, hivi wataalam tunaowapeleka nje ya nchi kusoma, huwa wanasoma nini? Kama ulishawahi kupelekwa nje ya nchi, jiulize ulienda kusomea nini? Kila mtu ajiulize! Baada ya kurudi amefanya nini? Inawezekana vya darasani hukuvielewa, vya kuona pia umesahau? Watu wa mazingira, mpo! wa afya nanyi mpo? manispaa Je!? wa fani nyingine nanyi mliona nini? mliumwa na mbu kule? mliumwa malaria kule? Kama hamkuumwa, mlijiliza ni kwa namna gani mkirudi mtatatua hilo tatizo? Au niwatanie kwamba wengi wetu tukirudi fikra zetu zinabaki kuwaota wazungu na kutamani kuwa kama wao wanavyoonekana na si wanavyotenda. Ndio maana sasa hivi ukitafuta mtu halisi unaweza kupata wakati mgumu.

Nywele kama wazungu! Rangi kama wazungu! Ni hayo tu ndio nayaona tumefanikiwa sana! Wenzetu walishajitambua thamani yao na ndio maana wakajipambanua na kujitofautisha na wanyama wengine kwa sababusi class ya wanyama wengine.

Tukichukua mfano, jiulize kwanini taka zimezagaa kila mahali hasa kwenye miji mikubwa. Taka za kuzagaa zinatakiwa zionekane zile tu zinazozalishwa na mijusi au viumbe visiyokuwa na akili. Wewe mwanadamu unatakiwa utumie akili yako na kuhakikisha kuwa taka unazozalisha huzitupi ovyo. Sasa angalia ambavyo hatutumii akili. Zile taka unaitupa ovyo ukidai huoni dustbin. Taka zile zinazagaa, zingine zinaanguka na kujaa kwenye mitalo. Mvua ikinyesha, maji machafu yanazagaa na kutuletea magonjwa. Tukienda hospital dawa hamna, tunalalamika. Lakini CHANZO CHA TATIZO NI WEWE MWENYEWE! Hapo ndipo wenzetu wanapotucheka, hawa jamaa vipi? utashi wao uko wapi?Ukiwaambia magari yote ya abiria yawe na dustbins, utaambiwa ooh! magari ya wakubwa. Sasa wakubwa si ndio hasa wanatakiwa watuonyeshe njia? Kuliwahi kutokea tangazo la tigo la jamaa kuachwa na gari wakati akichimba dawa, na watu hatukuona tatizo/udhalili wa lile tangazo. Hivi kweli walishindwa hata kusema jamaa akiachwa akimshangaa pundamilia!!!

Niliwahi kuongea na Mh. mmoja kwamba wajitahidi kuwaelimisha watu na kusimamia taratibu zilizowekwa kwa kuwa sasa hivi tuna vituo vingi vya TV na radio, akaniambia ni gharama! Nikashangaa! Tangu lini elimu ikawa rahisi? Au kwa sababu tulisoma bure?Basi tujaribuni ujinga kwa kuwa elimu ni gharama!!!




Tufike mahali tujitambue thamani yetu na kusema tumechoshwa na kunyanyaswa na magonjwa badala ya kila siku tukiumwa, tunakimbilia hospitali bila kujiuliza kwanini tunaumwa. Kauli mbiu ya miaka 50 ya uhuru, kwamba tumethubutu, tumeweza, sijui nini! Huwa najiuliza, tumeweza katika sekta ipi? Vitu vya wachina kujaa madukani ndio kuweza? Used cars za wajapan zilizojaa barabrani ndio kuweza? Elimu down, umaskini juu, magonjwa juu, uchafu juu, vifo juu, michezo down, viwanda down, njaa juu, tumeweza wapi? Kama tumeshindwa hata kufagia, tunaweza nini? Kama unashika ganda la muwa au chungwa na ukalitupa tu ovyo, unaweza nini? Utashi wako uko wapi? Tumelogwa, au ni pepo!?

Kwa mtazamo wangu, badala ya kusema tumeweza, tulipaswa kusema tumetambua tulipoangukia, sasa tunasimama na kuanza hatua ya kwanza. Jamani tutokomeze maradhi kwa kuweka mazingira safi. Kila mtu ajione ni mjinga pale anapotupa taka iwe ni dirishani mwa gari, iwe ni kwenye mtalo, iwe ni kukojoa ovyo, nk. Bila kujitambua sisi wenyewe na kuacha tabia za uchafu kwa mtu mmoja mmoja, magonjwa yataendelea kututesa daima na juhudi zinazofanywa na mamlaka za kufanya usafi kila Jumamosi ya mwanzo wa mwezi hazitaweza kufanikiwa kwa kuwa unaweza ukafagia sasa na mimi nikatupa uchafu dakika 2 zijazo na kufanya usafi uliofanya ukawa bure. Tuwe tunathubutu kuwakumbusha wenzetu pale tunapoona wanakwenda kinyume.

Tatizo kubwa ninaloliona ni kwamba tunaogopa kuthubutu. Kwa mfano jiji la Dar, utaambiwa ni jiji kubwa hivyo ni vigumu. Mimi naona ni rahisi sana. Hivi tukiwachukua wale vijana wanaopiga debe, tuwakawapa vitambulisho na kuwakabidhi hilo jukumu la kuwawajibisha watu, unadhani watashindwa? Cha muhimu ni kuwajulisha wahusika kwamba hao vijana watakuwepo mtaani kwa ajili ya kazi hiyo na kila mtu ajue hivyo. Baada ya hapo ni utekelezaji.Nadhani hawawezi kushindwa.Wanachohitaji ni kibali tu na waambiwe wakimkamata wachukue kiasi gani kwa huyo mtu na akibisha wampeleke wapi.

TAFAKARI NA UCHUKUE HATUA!
  1. Makala nzuri,
  2. Ni kweli watanzania wengi (haswa viongozi) ni wavivu wa kufikiri, na hili ndilo linalomletea shida Mh. Rais ktk uongozi wake, kasi yake ya uongozi na staili zinatofautiana kwa kiasi na baadhi ya viongozi (Mf. Mh. Lukuvi juzi bungeni, Yule mbunge Mh. Simbachawene "eti Rais anatukanwa wakati watz wamechoka na maisha wanatoa challenge kwa Rais).
  3. Na hii imepelekea kuwa na viongozi wafuasi wa Rasi badala ya viongozi watendaji.
  4. Na kwa upande wa raia (Watz) wao hatuwezi walaumu sana kwani sasa hivi wapo busy na kufikiri jinsi gani maisha yatakuwa bora, haswa baada ya elimu ya uraia iliyotolewa na vyama vya upinzani.
 
tujaribuni ujinga kwa kuwa elimu ni gharama!!! hapa nimepapenda sana na muomba JK afanye hivyo
 
siriziki na uongozi wake hata kidogo .. na siwezi kumkubali Lowasa hata siku moja .. wote hao ni wamoja...lakini kwa nini tutake kutafuniwa kila kitu? Kikwete hana tatizo hata moja.. tatizo ni watanzania and <u><b>even small kid can prove this i swear</b></u>
<br />
<br />

Nimekuelewa vizuri ivuga tatizo ni sisi watanzania kuamua kumchagua kwa mara ya pili hali tunajua ufanisi wake uko chini.
 
<br />
<br />

Nimekuelewa vizuri ivuga tatizo ni sisi watanzania kuamua kumchagua kwa mara ya pili hali tunajua ufanisi wake uko chini.
imekupigia makofi.. wewe jamaa una akili nyingi sana...hited the point
 
siwezi kuwalaumu kwa kumwaga damu<font size="3"><u><b> mtalaumiwa na vizazi vyenu kwa kuirudisha ccm madarakani kwa kupitia box la kura</b></u></font>
<br />
<br />
Ingekuwa ni rahisi kuwatoa CCM kwa barrot box basi neno 'kuchakachua' lisingekuwa maarufu kama ilivyo sasa ndio maana nikasema tulaumiwe kwa kutofanya mapinduzi ya nguvu kuing'oa CCM
 
Tanzania ni moja ya nchi rahisi sana kuendeleza kwa kiongozi mwenye ufahamu na vision. Kuna ardhi ya kutosha yenye rutuba, watu wasio na fujo, watiifu na woga, kuna madini kila mahali. Hebu fananisha mambo hayo na jirani zetu wa Rwanda, Kenya au hata DRC.
Mambo matatu tu kiongozi akiyafanya Tanzania itaendelea hata katika kipindi cha miaka 20 ijayo.
Kiongozi awe na nidhamu yeye mwenyewe halafu aweke nidhamu kwa taifa, ikilazimu hata kwa viboko. (nidhamu: doscipline, namaanisha katika mambo yote, ya fedha, ya utawala bora na siasa za maendeleo)
2- Asimamie elimu kiasi kila Mtanzania apate elimu bora ya kisasa hadi angalau form 6 (Hakuna kufukuzana darasa la saba n.k.)
3- Awezeshe asilimia 90 ya Watanzania wawe na umeme.(hakuna nchi iliyoendelea bila umeme)
Haya ni mambo yanayowezekana tena kwa muda mfupi sana kama kiongozi atakuwa na vision na atajua priorities.
Kama kiongozi atafuata haya, basi moja kwa moja hatafanya yafuatayo-
-Hataruhusu rushwa kwa mtu yeyote, si mwanasiasa, askari au hata raia wa kawaida na hatakubali kununuliwa.
-Kwa kila shilingi itakayotumika atahakikisha inatumika kwa sababu moja tu- ya kuleta shilingi nyingine. Hivyo hakutakuwa na misafara ya kuaga au kuamkia.
-Hatakuwa mvivu. Siku zote atafuatia mambo. atachagua watu waaminifu na hatasita kumfukuza yeyote, kutaifisha mali yake au kumfunga ikibidi hivyo.
Jee, kuna kiongozi yeyote wa Tanzania, including Mwalimu, aliyafanya haya? Mfano wa karibu wa mtu aliyeyafanya haya ni Kagame. Na Kimataifa ni
Lee Kuan Yew wa Singapore, na pia viongozi wa China.
Hakuna jambo la ajabu katika maendeleo, wala si uchawi- ni akili timamu iliyo na lengo na uaminifu. Bongo tunachezeana tu.
 
Back
Top Bottom