JacksonMichael
JF-Expert Member
- Mar 22, 2012
- 339
- 61
Kweli mapenzi yakizidi unakuwa kama kichaa, sasa wa kupewa pongezi hapo nani kama sio Rais na mwenyekiti wa CCM?
Kama hii habari niyaukweli basi inamaanisha serikali ya CCM haiwezi kuwajibika mpaka watu waandamane japokua wao wanadai maandamano ni kuharibu amani? Mbona sasa kama ni kweli wahusika wamerudishiwa mashamba yao si juzijuzi tu raia hawa waliandama mpaka kwa mkuu wa mkoa Maggesa!!!! Basi maandamano ndio dawa ya kuleta maendeleo na haki kwa kizazi cha sasa hivi nchini Tanzania.
Baada ya maandamano ya zaidi ya wananchi 5,000 wa kata ya Moshono na Mlangarini mwanzoni mwa mwezi huu kwenda kwa mkuu wa mkoa Magesa Mulongo kufuatilia fidia iliyoota mbawa ama kurejeshewa eneo lililotekwa na JWTZ hatimaye Mkuu huyo wa mkoa amewaeleza wananchi hao jana kuwa rais ameamua kuwarejeshea wananchi eneo hilo.
Shukran kwa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) na mbunge wa Arusha mjini Bw Lema waliokuwa nyuma ya hiyo 'land protest' ndivyo wananchi wanavyosema...
Mkuu eneo la T/Packers kama linavyojulikana kilkuwa kiwanda cha nyama zamani za WORLD WAR TWO (1945).Nyama ilikuwa inasafirishwa toka Arusha TZ kwenda England Europe kama auxiliary supply ya jeshi na watu wa Ulaya. Eneo hilo lilikuwa na watu hasa waliokuwa employees wa hicho kiwanda walio settle kwenye eneo hilo baada ya kiwanda kufungwa!!! Pia kuna wenyeji wa hapa hasa Waarusha na Wamasai ndio wenyeji wa hapo T/Parkers, Kiseriani, Olomitu na Mungushi, hivyo halikuwahi kuwa poli eneo hilo!!!!Wenyeji wana haki ya kulipwa kama serikali inataka kuwahamisha, bahati nzuri kama Raisi amewarudishia hayo maeneo basi Jeshi wangoe mabango na iwe kwenye writing kwa kumbukumbu za baadae!!!!!Hapa JWTZ inaingiaje? JWTZ ni serikali, JWTZ ilikuwepo maeneo hayo miaka mingi (ikiwa ni mapori), angalieni makambi yote, yalikuwa yako mbali na makazi ya wanainchi. Makaazi ya wananinchi yamefata makambi ya jeshi. Wakulaumiwa siyo jeshi, ila ni serikali kwa maana ya mipango miji na wizara ya ardhi. Uwajibikaji hakuna, ramani haziheshimiwi, ujenzi holela unaendelea kwa sana. sasa unazungumzia maeneo ya duka bovu. Mnasahau jeshi lenu linahitaji maeneo ya kufanyia mazoezi. ipo mizinga inayopiga umbali zaidi ya km 30, sasa wapi maeneo kama kila mahala wanajeshi wanafurushwa. hatua hiyo naona inaendekezwa sana kwa minajili ya solution za muda mfupi (kisiasa) lakini, madhara yake ni kulivua nguo jeshi, kulifanya kuwa kibogoyo na kuwa na gharama kubwa ya kuliendesha kiasi jeshi linaishia kuhangaika na mambo ya utawala zaidi ambayo uendeshaji wake unakuwa ni mkubwa kila siku. Pilika na harakati za wanasiasa zidhibitiwe na ikiwezekana jeshi liweke msimamo wake ambao utakuwa ni endelevu.