RAI - Nguvu ya Hoja?

HAKUNA shaka hata kidogo kwamba gazeti la uchambuzi wa masuala ya siasa la Rai, linalokuwa mitaani kila Alhamisi, kwa miaka mingi limejipambanua kuwa moja ya magazeti makini na yanayoheshimiwa na wasomaji wengi.

Hata hivyo ni ukweli ulio bayana kuwa, katika siku na miezi ya hivi karibuni, heshima ambayo gazeti hilo liliijenga kwa miaka mingi imekuwa ikiporomoka.

Miongoni mwa sababu ambazo zimechangia kuporomoka huko kwa Rai ni mwenendo usiofaa wa mhariri wake wa sasa, Deodatus Balile, ambaye amekuwa bingwa wa uandishi na uhariri unaoongozwa na misingi ya hisia, badala ya miiko na maadili ya uandishi wa habari.

Watu wanaomfahamu Balile vyema kama tulivyo sisi, ni mashahidi wa namna ambavyo mwanahabari huyo amekuwa akifanya kazi zake kwa kuwafurahisha ‘mabwana’ zake ambao kwa bahati mbaya katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakikabiliwa na tuhuma nzito za ufisadi.

Katika kutimiza malengo yake hayo, Balile amekuwa akifanya kila linalowezekana kuwashambulia kwa hoja za kuzusha, kejeli na wakati mwingine matusi, watu wote ambao anadhani wamekuwa chanzo au msingi wa matatizo yanayowakabili wanasiasa wa kundi fulani, ambao amekuwa akiwaabudu kwa mfano wa miungu watu.

Ili kufanikisha kazi hiyo ambayo hakuna shaka amekuwa akiifanya kwa maelekezo mahususi yaliyojengwa katika misingi ya kulipa kisasi, kukomoa, kutukana na hata kuchafua watu, Balile amegeuka kibaraka wa hoja, sambamba na kuwa mtumwa wa ushawishi wa wanasiasa wa kundi hilo ambao wamejeruhiwa kimamlaka, kwa makosa ambayo ama waliyafanya wao moja kwa moja au yalifanywa na ofisi walizopewa dhamana ya kuziongoza.

Miongoni mwa wanasiasa ambao amekuwa akifanya juhudi kubwa za kujaribu kuwasafisha kutokana na majina yao kuchafuka baada ya kutajwa katika kashfa kadha wa kadha za kifisadi katika miezi ya hivi karibuni, ni pamoja na Rostam Aziz na Edward Lowassa.

Historia inaonyesha na kuthibitisha wazi kwamba, Balile amekuwa kinara na mmoja wa wanahabari ambao wamekuwa wakimpamba Lowassa tangu mwanasiasa huyo alipokuwa Waziri wa Maji na Mifugo, zama za Serikali ya Awamu ya Tatu na akaendelea na kazi hiyo, ama kwa kujipa mwenyewe au kwa maelekezo, hata alipokuwa waziri mkuu kabla hajalazimika kujiuzulu Februari mwaka huu, wakati jina lake lilipotajwa katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

Katika kutimiza azima yake hiyo, Balile amekuwa akitumia vibaya mamlaka ya uhariri aliyonayo kuwapaka matope watu wote na taasisi ambazo amekuwa akiamini kuwa zilichangia katika kuwaangusha na kuwafikisha pale walipo leo wanasiasa hao wa kundi lake.

Ushahidi wa hili ni rahisi kabisa, kwani tangu akabidhiwe gazeti hilo akiwa mhariri, habari nyingi kubwa zinazoandikwa zimekuwa zikiwalenga kwa maana ya kuwashambulia kina Freeman Mbowe, Dk. Willibrod Slaa, Zitto Kabwe na John Mnyika, ambao ni viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho kimekuwa mstari wa mbele katika vita dhidi ya ufisadi kwa takriban mwaka mmoja sasa.

Ni wazi kwamba kwa namna ya kishabiki, Balile amekuwa akishindwa kuficha hisia zake, hali iliyosababisha awe akikitaja chama hicho cha upinzani na viongozi wake kuwa watu walioshiriki katika kile anachokiita kuwazushia watu uongo, kuwapaka matope na hata kusababisha wang’atuke.

Si hao tu, Balile amekuwa akilishutumu Bunge na akafikia hatua ya kumwandama waziwazi, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, si kwa hoja, bali kama ajenda zinazoonyesha hasira ya namna taasisi hiyo ilivyoshiriki kikamilifu katika kile anachokiona kuwa ni kuwaangusha, kuwanyamazisha na kuwahujumu wanasiasa wa kundi analoonekana kuliabudu.

Akitumia mwelekeo huo huo, Balile katika toleo la jana la gazeti la Rai, baada ya kuona juhudi zake za kuwashambulia wanasiasa hazitoshi na pengine zimeshindwa kuzaa matunda, akaamua kuliingiza gazeti hili la Tanzania Daima katika propaganda zake chafu za kuwasafisha wanasiasa wake hao na kuwachafua wale wanaoonekana kuwa wabaya wao.

Kwa namna ya kujidhalilisha na pengine kujikana mwenyewe, mhariri huyo wa Rai akaandika habari moja iliyoanzia ukurasa wa kwanza inayomshutumu Mbowe na CHADEMA, akiwatuhumu kulitumia Tanzania Daima kuwachafua wanasiasa na baadhi ya viongozi wa serikali ya Kikwete.

Katika kuonyesha kwamba ni mtu aliyechanganyikiwa, Balile ambaye kabla ya kujiunga na Rai akitokea masomoni Uingereza alikuwa Mhariri Mkuu wa kwanza wa Tanzania Daima, akafikia hatua ya kuliita gazeti hili kuwa ni la CHADEMA, ilhali akijua kuwa yeye mwenyewe alishiriki kikamilifu kulisajili.

Katika hali hiyo inayoonyesha hulka ya uongo iliyojengeka ndani mwake, akafanya hivyo akisahau kwamba, ni yeye mwenyewe ambaye wakati akiwa mhariri wa gazeti hili alipata kuandika kwa zaidi ya mara moja tahariri akipinga maneno ya watu waliokuwa wakijaribu kulihusisha gazeti hili na chama cha siasa ambacho leo anakihusisha na chombo alichoshiriki kukianzisha. Huu ni unafiki unaovuka mipaka.

Katika kujistawisha kiuongo, katika tahariri ya Rai ya jana, Balile alifikia hatua ya kulizushia uongo mwingine Tanzania Daima, akidai kuwa, ndilo lililohusika kumwangusha Lowassa, na kwamba limekuwa likiwatukana watu matusi ya nguoni.

Hakuna shaka kwamba, maandishi ya namna hii ni ya uzushi na kimsingi ni matusi, si kwa Tanzania Daima tu, bali hata kwa taasisi za umma ambazo tunaamini zinafanya kazi ya kuhakiki mwenendo na kazi za kila siku za vyombo vya habari nchini, na kuhakikisha vinaendesha shughuli zake kwa kuzingatia maadili ya kazi ya uandishi wa habari.

Sisi wa Tanzania Daima tunaamini kwamba, taasisi zinazosimamia maadili ya kazi ya uandishi wa habari hazitakaa kimya pasipo kuchukua hatua zinazostahili dhidi ya gazeti la Rai, wamiliki wake na hususan mhariri wake, ambaye hakuna shaka, amejipambanua kuwa mwanahabari aliyechanganyikiwa, na mtu aliye tayari kugharamia kupoteza thamani ya utu wake kwa sababu tu ya kuangalia masilahi yake. Hakika huyu ni mchumia tumbo.

Wakati tukiamini kwamba kilio chetu dhidi ya Rai na hususan Balile kitakuwa kimefika mahali panapostahili, sisi wa Tanzania Daima tunapenda kueleza bayana kwamba, tumeamua kwa dhati kushughulika ipasavyo na umamluki wa aina hii wa uandishi wa habari kwa kufuata taratibu za kitaaluma na kisheria, ili jambo hili liwe fundisho kwa watu wengine wenye hulka za namna hii, ambazo hatuna shaka ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya taifa letu. Mungu ibariki Tanzania.
Source: Tanzania Daima: ijumaa, 19 septemba 2008

Waberoya: Mhariri wa Tanzania Daima Amenifurahisha!!Big Up Kibanda



Waberoya
‘’I have come to the conclusion that politics are too serious a matter to be left to the politicians’’. Charles De Gaulle (1890 - 1970
 
mhariri wa TZ daima na balile wote ni makanjanja tu!Balile anawatumikia kina RA na kikosi chake na wa TZ daima anawatumikia kina Mbowe na kikosi chake!1+1=1
Wote wale wale!
 
Ndio mjue media bongo ni fake fake! mie nilifikiri ni nukuu kutoka kwa katibu kata wa CCM anatoa hotuba katika ufunguzi wa kampeni za ujumbe wa shina?! kumbe ni mhariri wa gazeti tena linajiita binafsi? Bongo kweli kila kitu kinawezekana.

Binafsi naona hakuna haja ya kubishana na RAI zaidi tutakuwa tunalipa promo wakati linaelekea kufa liacheni lijifie na tusinunue tu! kama kuna haja tununue kampuni inayolichapisha kwa michango ya wana JF
 
First Lady una uhakika na ulichokisema? Nathani umekosea kwani to some extent Mtz daima wanawakilisha mawazo ya jamii ya Wadanganyika.
 
hilo gazeti lingine litakuwa ni mwanahilisi!maana wamesema linatoka kwa wiki then la wapambe wao!mhuuu sasa kwa nini wameogopa kulitaja hilo gazeti lingine?
ndo ukajanja huu!
 
hilo gazeti lingine litakuwa ni mwanahilisi!maana wamesema linatoka kwa wiki then la wapambe wao!mhuuu sasa kwa nini wameogopa kulitaja hilo gazeti lingine?
ndo ukajanja huu!
LoL,

FL umeniacha hoi kwa kubahatisha kwako. Probably litakuwa hilo. Halafu umeangalia uandishi wa makala yenyewe? Japo anawaona wengine kuwa vilaza na mamluki wa habari lakini naye anaonekana pamoja na usomi wake hayuko makini na kazi yake. Re-read!
 
Ni kawaida yake kuandama watu badala ya masuala. Alipokuwa Tanzania Daima alimwandama sana Dr Makongoro Mahanga (Mbunge wa Ukonga) wakati huo akiwa Naibu Waziri wa Miundo Mbinu hata kwa shimo dogo tu la barabarani maeneo ya Ukonga na Kitunda. Alikuwa anakaa Kitunda.
 
Katika kuonyesha kwamba ni mtu aliyechanganyikiwa, Balile ambaye kabla ya kujiunga na Rai akitokea masomoni Uingereza alikuwa Mhariri Mkuu wa kwanza wa Tanzania Daima, akafikia hatua ya kuliita gazeti hili kuwa ni la CHADEMA, ilhali akijua kuwa yeye mwenyewe alishiriki kikamilifu kulisajili.
Sasa ishaanza kuwa ni Tanzania Daima vs Rai... Nawashauri wayaongelee pembeni na kumalizana na wakubaliane kuwa siasa za kubeba 'watu flani' hazitotupeleka popote. Mwisho wa umaarufu wao utafika lakini ujuzi wenu kama waandishi utabaki, fedheha itawekwa wapi?

Taifa mbele!
 
Wana JF,

Naona sasa waandishi wameamua kuchambuana wenyewe. Yetu macho na masikio.
Hii ni Tahariri ya Tanzania Daima Sept 19, 2008.

Mhariri Rai amechanganyikiwa

HAKUNA shaka hata kidogo kwamba gazeti la uchambuzi wa masuala ya siasa la Rai, linalokuwa mitaani kila Alhamisi, kwa miaka mingi limejipambanua kuwa moja ya magazeti makini na yanayoheshimiwa na wasomaji wengi.

Hata hivyo ni ukweli ulio bayana kuwa, katika siku na miezi ya hivi karibuni, heshima ambayo gazeti hilo liliijenga kwa miaka mingi imekuwa ikiporomoka.

Miongoni mwa sababu ambazo zimechangia kuporomoka huko kwa Rai ni mwenendo usiofaa wa mhariri wake wa sasa, Deodatus Balile, ambaye amekuwa bingwa wa uandishi na uhariri unaoongozwa na misingi ya hisia, badala ya miiko na maadili ya uandishi wa habari.

Watu wanaomfahamu Balile vyema kama tulivyo sisi, ni mashahidi wa namna ambavyo mwanahabari huyo amekuwa akifanya kazi zake kwa kuwafurahisha ‘mabwana’ zake ambao kwa bahati mbaya katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakikabiliwa na tuhuma nzito za ufisadi.

Katika kutimiza malengo yake hayo, Balile amekuwa akifanya kila linalowezekana kuwashambulia kwa hoja za kuzusha, kejeli na wakati mwingine matusi, watu wote ambao anadhani wamekuwa chanzo au msingi wa matatizo yanayowakabili wanasiasa wa kundi fulani, ambao amekuwa akiwaabudu kwa mfano wa miungu watu.

Ili kufanikisha kazi hiyo ambayo hakuna shaka amekuwa akiifanya kwa maelekezo mahususi yaliyojengwa katika misingi ya kulipa kisasi, kukomoa, kutukana na hata kuchafua watu, Balile amegeuka kibaraka wa hoja, sambamba na kuwa mtumwa wa ushawishi wa wanasiasa wa kundi hilo ambao wamejeruhiwa kimamlaka, kwa makosa ambayo ama waliyafanya wao moja kwa moja au yalifanywa na ofisi walizopewa dhamana ya kuziongoza.

Miongoni mwa wanasiasa ambao amekuwa akifanya juhudi kubwa za kujaribu kuwasafisha kutokana na majina yao kuchafuka baada ya kutajwa katika kashfa kadha wa kadha za kifisadi katika miezi ya hivi karibuni, ni pamoja na Rostam Aziz na Edward Lowassa.

Historia inaonyesha na kuthibitisha wazi kwamba, Balile amekuwa kinara na mmoja wa wanahabari ambao wamekuwa wakimpamba Lowassa tangu mwanasiasa huyo alipokuwa Waziri wa Maji na Mifugo, zama za Serikali ya Awamu ya Tatu na akaendelea na kazi hiyo, ama kwa kujipa mwenyewe au kwa maelekezo, hata alipokuwa waziri mkuu kabla hajalazimika kujiuzulu Februari mwaka huu, wakati jina lake lilipotajwa katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

Katika kutimiza azima yake hiyo, Balile amekuwa akitumia vibaya mamlaka ya uhariri aliyonayo kuwapaka matope watu wote na taasisi ambazo amekuwa akiamini kuwa zilichangia katika kuwaangusha na kuwafikisha pale walipo leo wanasiasa hao wa kundi lake.

Ushahidi wa hili ni rahisi kabisa, kwani tangu akabidhiwe gazeti hilo akiwa mhariri, habari nyingi kubwa zinazoandikwa zimekuwa zikiwalenga kwa maana ya kuwashambulia kina Freeman Mbowe, Dk. Willibrod Slaa, Zitto Kabwe na John Mnyika, ambao ni viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho kimekuwa mstari wa mbele katika vita dhidi ya ufisadi kwa takriban mwaka mmoja sasa.

Ni wazi kwamba kwa namna ya kishabiki, Balile amekuwa akishindwa kuficha hisia zake, hali iliyosababisha awe akikitaja chama hicho cha upinzani na viongozi wake kuwa watu walioshiriki katika kile anachokiita kuwazushia watu uongo, kuwapaka matope na hata kusababisha wang’atuke.

Si hao tu, Balile amekuwa akilishutumu Bunge na akafikia hatua ya kumwandama waziwazi, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, si kwa hoja, bali kama ajenda zinazoonyesha hasira ya namna taasisi hiyo ilivyoshiriki kikamilifu katika kile anachokiona kuwa ni kuwaangusha, kuwanyamazisha na kuwahujumu wanasiasa wa kundi analoonekana kuliabudu.

Akitumia mwelekeo huo huo, Balile katika toleo la jana la gazeti la Rai, baada ya kuona juhudi zake za kuwashambulia wanasiasa hazitoshi na pengine zimeshindwa kuzaa matunda, akaamua kuliingiza gazeti hili la Tanzania Daima katika propaganda zake chafu za kuwasafisha wanasiasa wake hao na kuwachafua wale wanaoonekana kuwa wabaya wao.

Kwa namna ya kujidhalilisha na pengine kujikana mwenyewe, mhariri huyo wa Rai akaandika habari moja iliyoanzia ukurasa wa kwanza inayomshutumu Mbowe na CHADEMA, akiwatuhumu kulitumia Tanzania Daima kuwachafua wanasiasa na baadhi ya viongozi wa serikali ya Kikwete.

Katika kuonyesha kwamba ni mtu aliyechanganyikiwa, Balile ambaye kabla ya kujiunga na Rai akitokea masomoni Uingereza alikuwa Mhariri Mkuu wa kwanza wa Tanzania Daima, akafikia hatua ya kuliita gazeti hili kuwa ni la CHADEMA, ilhali akijua kuwa yeye mwenyewe alishiriki kikamilifu kulisajili.

Katika hali hiyo inayoonyesha hulka ya uongo iliyojengeka ndani mwake, akafanya hivyo akisahau kwamba, ni yeye mwenyewe ambaye wakati akiwa mhariri wa gazeti hili alipata kuandika kwa zaidi ya mara moja tahariri akipinga maneno ya watu waliokuwa wakijaribu kulihusisha gazeti hili na chama cha siasa ambacho leo anakihusisha na chombo alichoshiriki kukianzisha. Huu ni unafiki unaovuka mipaka.

Katika kujistawisha kiuongo, katika tahariri ya Rai ya jana, Balile alifikia hatua ya kulizushia uongo mwingine Tanzania Daima, akidai kuwa, ndilo lililohusika kumwangusha Lowassa, na kwamba limekuwa likiwatukana watu matusi ya nguoni.

Hakuna shaka kwamba, maandishi ya namna hii ni ya uzushi na kimsingi ni matusi, si kwa Tanzania Daima tu, bali hata kwa taasisi za umma ambazo tunaamini zinafanya kazi ya kuhakiki mwenendo na kazi za kila siku za vyombo vya habari nchini, na kuhakikisha vinaendesha shughuli zake kwa kuzingatia maadili ya kazi ya uandishi wa habari.

Sisi wa Tanzania Daima tunaamini kwamba, taasisi zinazosimamia maadili ya kazi ya uandishi wa habari hazitakaa kimya pasipo kuchukua hatua zinazostahili dhidi ya gazeti la Rai, wamiliki wake na hususan mhariri wake, ambaye hakuna shaka, amejipambanua kuwa mwanahabari aliyechanganyikiwa, na mtu aliye tayari kugharamia kupoteza thamani ya utu wake kwa sababu tu ya kuangalia masilahi yake. Hakika huyu ni mchumia tumbo.

Wakati tukiamini kwamba kilio chetu dhidi ya Rai na hususan Balile kitakuwa kimefika mahali panapostahili, sisi wa Tanzania Daima tunapenda kueleza bayana kwamba, tumeamua kwa dhati kushughulika ipasavyo na umamluki wa aina hii wa uandishi wa habari kwa kufuata taratibu za kitaaluma na kisheria, ili jambo hili liwe fundisho kwa watu wengine wenye hulka za namna hii, ambazo hatuna shaka ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya taifa letu. Mungu ibariki Tanzania.
 
Waandishi wa habari sasa lazima wasome mathematics ili wawe analytical

Ballile amejitakia, hawezi kutukana gazeti ambalo amelianzisha yeye na pia katika tahariri yake ameandika makosa ya Tanzania Daima mwaka 2005, kipindi ambacho yeye alikuwa mhariri mkuu wake na ndiye aliyeandika tahariri nyingi kuelezea jinsi gazeti hilo lilivyo huru. KAma angetaka kusema angewaomba radhi kwanza Watanzania kwa kuwadanganya wakati huo na sasa ndipo asema anayotaka kusema tena kwa ushahidi na si maneno ya hisia. Ballile ana taaluma lakini kwa bahati mbaya haitumii kabisa
 
Ile thread ya Mhariri wa Rai ingeunganishwa humu.

Kwa maoni yangu hii ni dalili kwamba mambo yameiva na siku si nyingi tutaanza kula uhondo. Nilishasema tuna laana na narudia tena penye laana panahitajika sadaka na mara nyingi sadaka inalazimika iambatane na KAFARA, tunalazimika kutoa KAFARA ili laana tuliyonayo iondoke.
 
Balile umetukana wakunga na ukasahau uzazi ungalipo.......
Ngoja hao ulio wakumbatia wachache ziishe uone utakuwa mgeni wa nani...umesha chafua hali ya hewa sijui utakimbilia wapi au utarudi huko Hull?
Kumbe ulikuwa mhariri wa Tanzania Daima saizi unajifanya umesahau shauri yako.
 
hilo gazeti lingine litakuwa ni mwanahilisi!maana wamesema linatoka kwa wiki then la wapambe wao!mhuuu sasa kwa nini wameogopa kulitaja hilo gazeti lingine?
ndo ukajanja huu!


wewe upo upande gani maana unaonekana kama bendera......Uhuru na Mzarendo nini?
 
Back
Top Bottom