Rafiki yangu anaomba ushauri, Mpenzi wake anamnyima penzi

kwetumasoko

JF-Expert Member
Aug 24, 2016
866
510
Kuna kesi nimeletewa na rafiki yangu wa karibu sana kuhusu mahusiano yanayoendelea kati yake na mpenzi wake, hivyo anaomba ushauri kutoka kwangu.

Kaniambia kuwa katika mahusiano yao, wamedumu kwa muda wa miaka miwili lakini bado hawajafunga ndoa, hivyo wanaishi tofauti kila mmoja kwake lakini wilaya moja.

Mpenzi wake ni mtu wa kusafirisafiri wilaya mbalimbali kulingana na kazi anayofanya, anaweza kukaa huko field kwa muda wa wiki moja au hata zaidi.

Mara nyingi wamekuwa na mawasiliano mazuri na jamaa kwa muda wote awapo mbali, hata arudipo kutoka huko na mambo mengi wamekuwa wakishauriana kwa pamoja, na vilevile mpenzi wake huyo anaposhauriwa ni mwepesi kupokea ushauri.

Unajua huyo rafiki yangu yeye hanywi pombe ya aina yoyote, isipokuwa huyo mpenzi wake anakunywa pombe, na wakati mwingine hunywa na kulewa! Kwa upande wa pombe akimwambia aache kunywa sana, anamwambia kama unaona nakunywa pombe sana ni afadhali uniache.

Mbali na hapo analalamika kuwa mpenzi wake akienda kulala nyumbani kwake huwa anamwambia hajisikii kabisa kufanya mapenzi, inshort anamnyima kabisa. Ameniambia kuwa amekuwa akimfanyia hivo kwa muda mrefu, na akimhitaji huwa anaenda kulala, lakini mapenzi no. anamkatalia kabisa. Kwa hiyo kaja kwangu analalamika na kuomba ushauri.

Nami nawasilisha kwenu waungwana, niombe ushauri jinsi ya kumshauri huyo rafiki yangu.
 
okey demu ndiyo mlevi? kama ni ndiyo basi mwambie achukue ushauri wa kumuacha sababu hawatafika mbali
 
mwanaume ajitoe ambadilishe pole pole au akubaliane naye
Unajua mtu mzima mpaka akaamua kuja kwangu kuomba ushauri, ujue yamemkuta. Amenieleza kwa kirefu sana, mpaka imefika mahala nikakosa jibu, na ndo maana nimelileta humu jukwaani nikijua kuna ushauri ambao tunawezashare ili niweze kumpa rafiki yangu.
 
Unajua mtu mzima mpaka akaamua kuja kwangu kuomba ushauri, ujue yamemkuta. Amenieleza kwa kirefu sana, mpaka imefika mahala nikakosa jibu, na ndo maana nimelileta humu jukwaani nikijua kuna ushauri ambao tunawezashare ili niweze kumpa rafiki yangu.
kwa mfano mimi nakunywa ila mwenzangu hana tatizo na hilo na tunakunywa wote na mambo mengine yanaenda ni ngumu sana kukaa na mtu mnywaji wakati wewe hunywi
 
Seems like mwanamke anakauwezo flani hivi yaani ni mtu ambae anaweza kula, kupanga, kuvaa kwa hela yake, ndio maana anajiamini sana. Hategemei msaada wowote tuko kwa mwanaume, thats where the problem is. Ila kama jamaa ataona vipi aachane tu na huyo mwanamke maana hakuna future hapo. Mwanamke akishakujibu hivyo ni dhahidi kuwa ana plan b katika maisha. Mwambie rafikiyo ajiongeze tu, hakuna namna.
 
kwa mfano mimi nakunywa ila mwenzangu hana tatizo na hilo na tunakunywa wote na mambo mengine yanaenda ni ngumu sana kukaa na mtu mnywaji wakati wewe hunywi
Kunywa unaweza ukanywa, lakini sio unakunywa mpaka ukafika mahali ikawa ni tatizo, miss chagga unajua ninavyosema kuwa inaweza kuwa tatizo?
 
Kama hapa JF tunatumia fake ID bado watu wanaogopa kufunguka,
Je zingekuwa real si kuna watu wasingejiunga kabisa.
 
Mmmmh... aseee hapa naona mapenzi ya upande mmoja.. na jamaa ndo anampenda sana huyo mwanamke.. me kama harufu ya pombe ni kero kwangu harafu nimwambie mpenzi au mke wangu aache kunywa then akate tena kwa jibu lile sidhani kama ntamuelewa.. pia huyo mpenz wake naona kama hamjari maana kama anajari angeacha pombe ili kutomletea kero mpenz wake..
Issue ya kutofanya mapenzi nayo ni tata.. sijajua anamkatalia kwa sababu ipi.. labda kama anamkatalia kwa kigezo kuwa hajamuoa anasubiri ndoa.. ni bora akaeleza sababu ili kama hajisikii na ni tatzo waangalie namna ya kutatua tatzo ikibidi wamuone mtaalam.. vinginevyo hapo hakuna mapenz ya kweli... ajiongeze achukue hamsini zake.
 
Huyo mwanamke bado hajafungua moyo kuwa na huyo jamaa...Na kama kwenye uchumba tu jamaa ananza kuteseka afikirie itakuwaje wakiingia kwenye ndoa itakayo walazimu kuishi pamoja kwa miaka 50....Asi lazimishe sana mapenzi..
 
huyo rafiki yako kwa kuwa hanywi ila mpenziwe ndie anakunywa mi naona ni vema aachane nae coz hawataweza kudumu ktk mahusiano mpaka jamaa nae aamue kunywa ndipo wataendana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom