Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,344
- 9,845
Kuna kamanda tulikuwa nae BAVICHA tukipanga mikakati na kuhamasishana juu ya kuimarisha chama, kuongeza makamanda na mambo kibao.
Umepita kama mwezi hivi bila kuonana kwa kuwa nilisafiri. Jana nikakutana na kamanda, amekuwa mpole, amenyong'onyea, hajiamini. Nikampiga kwanza ofa ya samaki na ndizi rost kwenye kibanda umiza. Kidogo akaanza kufunguka kwa wasiwasi,".. Jamaa yangu, nimehamia CCM!" Halafu akatulia kuangalia reaction, sikuonyesha chochote.
Kisha akaendelea "...Wife amejifungua, sina kazi, nimejaribu kila issue inagoma. Hali yangu ni mbaya kiukweli. CCM wamemwaga yale mahela ya wizi, naweza angalau kupona".
Nilisikia tumbo limenivuruga, Nikakosa swali la kumuuliza, ila baada ya muda nikamuuliza, mnamnadi mgombea gani? Mna uhakika wa kushinda? Akasema "Mimi sijui mgombea wala mambo ya kushinda, wao wenyewe wanajua watashindwa, mimi nashabikia tu kila kitu chao."
Mteja wangu wa kuku akanipigia simu, ikabidi niahirishe mazungumzo na kamanda.
Sasa leo tunakutana, jamani nimwambieje?
Naomba ushauri..
Umepita kama mwezi hivi bila kuonana kwa kuwa nilisafiri. Jana nikakutana na kamanda, amekuwa mpole, amenyong'onyea, hajiamini. Nikampiga kwanza ofa ya samaki na ndizi rost kwenye kibanda umiza. Kidogo akaanza kufunguka kwa wasiwasi,".. Jamaa yangu, nimehamia CCM!" Halafu akatulia kuangalia reaction, sikuonyesha chochote.
Kisha akaendelea "...Wife amejifungua, sina kazi, nimejaribu kila issue inagoma. Hali yangu ni mbaya kiukweli. CCM wamemwaga yale mahela ya wizi, naweza angalau kupona".
Nilisikia tumbo limenivuruga, Nikakosa swali la kumuuliza, ila baada ya muda nikamuuliza, mnamnadi mgombea gani? Mna uhakika wa kushinda? Akasema "Mimi sijui mgombea wala mambo ya kushinda, wao wenyewe wanajua watashindwa, mimi nashabikia tu kila kitu chao."
Mteja wangu wa kuku akanipigia simu, ikabidi niahirishe mazungumzo na kamanda.
Sasa leo tunakutana, jamani nimwambieje?
Naomba ushauri..