ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,681
Wadau,
Nawasalim...
Leo naomba tuongelee madirisha.
New trend in Europe ni utumiaji wa madirisha ya plastic a.k.a plastic windows or PVC windows. Katika nchi hizi madirisha haya yana manufaa zaidi pale yanapowekewa vioo vya layers na kuacha hewa katikati ambayo husaidia kuzuia baridi lisiingie ndani au joto lisitoke nje - isulation.
Madirisha ya plastic kiujumla yana muonekano unaovutia na yako imara sana.
Madirisha ya plastic yanaweza kutengenezwa kwa mitindo mbalimbali ya ufungukaji kama vile kufunguka kwa nje/ndani, ku flip kwa juu au kuslide.
Sijaona nchini Tanzania madirisha haya yakitengenezwa au kuuzwa kwa wingi. Mojawapo wa suppliers wa madirisha haya ni kiwanda kinachomilikiwa na wawekezaji kutoka Uturuki kilichopo Mbezi Beach karibu na SHAMO. (Jina la kiwanda nimelisahau ila lina name PVC na ukipita utaona madirisha haya yamewekwa).
Kama uko kwenye ujenzi na unapenda kuwa na kitu tofauti, jaribu madirisha haya. Hata hivyo ni vyema kutambua kuwa uchache wake unaweza kusababisha bei yake kuwa ya juu kama kawaida ya vitu hadimu.
What is interesting? Utengenezaji wa madirisha ya plastic hautofautiani na ule wa aluminium, lakini for unclear reasons nchini kwetu madirisha ya aluminium peke yake ndio yaliyoshamiri.
Nadhani kwa waliokula chumvi nyingi watakumbuka kuwa madirisha ya aluminium yalipoingia bei yake ilikuwa haikamatiki, lakini siku hizi hata magenge ya kuuza samaki yanatengenezwa kwa madirisha ya aluminium. Hii ni changamoto kwa wawekezaji wa sekta ya ujenzi. Atakayeanzisha kuleta madirisha ya plastic kwa wingi atanufaika sana kabla bei yake haijaporomoka.
Niwatakie siku njema...
Nawasalim...
Leo naomba tuongelee madirisha.
New trend in Europe ni utumiaji wa madirisha ya plastic a.k.a plastic windows or PVC windows. Katika nchi hizi madirisha haya yana manufaa zaidi pale yanapowekewa vioo vya layers na kuacha hewa katikati ambayo husaidia kuzuia baridi lisiingie ndani au joto lisitoke nje - isulation.
Madirisha ya plastic kiujumla yana muonekano unaovutia na yako imara sana.
Madirisha ya plastic yanaweza kutengenezwa kwa mitindo mbalimbali ya ufungukaji kama vile kufunguka kwa nje/ndani, ku flip kwa juu au kuslide.
Sijaona nchini Tanzania madirisha haya yakitengenezwa au kuuzwa kwa wingi. Mojawapo wa suppliers wa madirisha haya ni kiwanda kinachomilikiwa na wawekezaji kutoka Uturuki kilichopo Mbezi Beach karibu na SHAMO. (Jina la kiwanda nimelisahau ila lina name PVC na ukipita utaona madirisha haya yamewekwa).
Kama uko kwenye ujenzi na unapenda kuwa na kitu tofauti, jaribu madirisha haya. Hata hivyo ni vyema kutambua kuwa uchache wake unaweza kusababisha bei yake kuwa ya juu kama kawaida ya vitu hadimu.
What is interesting? Utengenezaji wa madirisha ya plastic hautofautiani na ule wa aluminium, lakini for unclear reasons nchini kwetu madirisha ya aluminium peke yake ndio yaliyoshamiri.
Nadhani kwa waliokula chumvi nyingi watakumbuka kuwa madirisha ya aluminium yalipoingia bei yake ilikuwa haikamatiki, lakini siku hizi hata magenge ya kuuza samaki yanatengenezwa kwa madirisha ya aluminium. Hii ni changamoto kwa wawekezaji wa sekta ya ujenzi. Atakayeanzisha kuleta madirisha ya plastic kwa wingi atanufaika sana kabla bei yake haijaporomoka.
Niwatakie siku njema...