CAMARADERIE
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 4,419
- 1,929
Si mara zote mkuu, wakati mwingine inategemeana na vipaombele vya mtu, pia ujue kuwa neno uwezo wa kifedha ni subjective term.Vitu vya kifahari ni kwa ajili ya wenye uwezo kifedha. Jambazi anapokwenda kwa mwenye fedha hana shida na madirisha, yeye anapita mlangoni, tena family yote ikiwa nyumbani
Si mara zote mkuu, wakati mwingine inategemeana na vipaombele vya mtu, pia ujue kuwa neno uwezo wa kifedha ni subjective term.
Wamesema wenyewe sq meter moja ni shs laki mbili na elfu thelathini. Au nimesoma makengeza?
Kwani haya madirisha yanauzwa kwa sq. metre au linauzwa dirisha kamili lilikamilika lenye style fulani ya kufunguka?
Watu wengi hukosea sana kwenye grille (sio grill) designs......pitieni humu!.....bila kujali kingledha cha fundi na sifanyi promo
Savei Metal Art & Aluminium Works: maua ya kisasa kwa ajili ya grill za madirisha
Mkuu,
Nimetembelea hiyo page lakini sijaona huo u-kisasa wa hayo maua aliyochora. Kitu kinapoitwa cha kisasa, inabidi kiwe tofauti na vitu vilivyofanywa na watu wa middle ages, sasa katika hayo maua sijaona kitu ambacho hakikuwepo enzi za Roman empire. Au labda neno "ya kisasa" tunalielewa tofauti!
Vileviel umuhimu wa kuweka grill au grille ni kujaribu kufanya uwezekano wa mwizi kuingia kuwa mgumu/mdogo. Sasa haya maua ambayo yanaweka curves ndefu yanapoteza maana kwa sababu mwizi anaweza kuyabend kirahisi zaidi. Kwahiyo pamoja na kutaka urembo lakini lengo kuu la kuweka grille lisisahauliwe.
Pole mkuu na wengine wote.......jaribuni hii....ina mawazo mengi ya finishing pia
Security Window Grill Design Ideas, Pictures, Remodel, and Decor - page 4
Kwani haya madirisha yanauzwa kwa sq. metre au linauzwa dirisha kamili lilikamilika lenye style fulani ya kufunguka?
Dirisha la kawaida lina sq. m angalau 3 kwa maana ya 1.5 X 2. Kwahiyo bei yao si mchezo!Hii ni kurahisisha hesabu. Dirisha lako likiwa meter sq 2 basi bei ni mara mbili bei iliyotajwa.
Aluminium bomba.
Houzz naijua na ni member wa muda mrefu sana.
Angalia style yao ya majiko. Hiyo ndio new trend ya kutengeneza "kisiwa" jikoni.
Thanks.
Marcopolo, nakubaliana na wewe kabisa dirisha za PVC ni nzuri sana kuliko za Alminium, tatizo ni gharama. na madirisha haya yanauzwa kwa kutegemea sq.meter moja, mfano square meter moja kwa Alminium ni kama 120,000- 180,000, PVC square meter moja ni kama 250,000-350,000, na itategemea unataka dirisha lako lifungukaje. wakati nataka kuweka alminium kwenye nyumba yangu, gharama ya madirisha yote ilikuwa kama 5.3m, nilipokwenda pale mbezi beach karibu na Shamo, nilipewa gharama ya 13,200,000 tena baada ya kupunguziwa. Hivyo tatizo ni gharama, ila ni mazuri sana na yanapendezehsa nyumba.
Mkuu, Hapo kw ahesabu za haraka haraka ni kama mara mbili ya dirisha la aluminium. Pale shamo wale waturuki wana kiwanda standard cha kisasa. Nadhani hilo pia linachangia kwenye bei kuwa ya juu. May be vijana wetu wakichangamka wakaanzisha workshops za kitaa gharama itapungua, ingawa kuna risk ya kwenda sambamba na kiwango. Tuendelee kuwa pamoja mkuu...Marcopolo, nakubaliana na wewe kabisa dirisha za PVC ni nzuri sana kuliko za Alminium, tatizo ni gharama. na madirisha haya yanauzwa kwa kutegemea sq.meter moja, mfano square meter moja kwa Alminium ni kama 120,000- 180,000, PVC square meter moja ni kama 250,000-350,000, na itategemea unataka dirisha lako lifungukaje. wakati nataka kuweka alminium kwenye nyumba yangu, gharama ya madirisha yote ilikuwa kama 5.3m, nilipokwenda pale mbezi beach karibu na Shamo, nilipewa gharama ya 13,200,000 tena baada ya kupunguziwa. Hivyo tatizo ni gharama, ila ni mazuri sana na yanapendezehsa nyumba.