Putin ni mwamba kuliko Trump

Putin ni mwamba kuliko Trump

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
10,488
Reaction score
16,646
Sisi yetu ni macho tu kushuhudia laana inayoendelea kuwapata madhalimu duniani.
Kwa sasa taifa la Marekani chini ya Trump linayumba sana na halijielewi linakoelekea.
Trump amewahi kudai pesa taslim za kile kilichotajwa kuwa ni misaada kwa Ukraine.Aliwahi kufokea mbele ya Kamera na Zelensky halafu akamkaribisha tena ikulu akacheka nae na kumuahidi vitu hewa.

Kiongozi huyo wa taifa kubwa amewahi kuzuia silaha nyeti kuipa Ukraine na baadae ikazitoa bila kuleta mabadiliko yoyote kwa kumegwa kwa ardhi ya Ukraine ambapo Urusi imekuwa ikizidungua moja baada ya nyengine.

Karibuni hivi raisi Trump amekuwa akionesha mahoka ya hali ya juu pale anapotoa makeke kwa Putin wa Urusi baadae kuomba tena urafiki naye.Kichekesho zaidi ni pale alipotoa agizo la mwezi mmoja na nusu kwa Putin afanye makubaliano na Zelensky kumaliza vita.Putin wala hakufanya hivyo.

Siku chache baadae Trump akapeleka nyambizi mbili za nyuklia karibu na Urusi na Putin akampuuza kabisa..Baada ya hapo Trump akapunguza mwezi mmoja na nusu mpaka siku 12.Nazo zimepita bila Putin kutikishika.

Kichekesho kikubwa ni sasa raisi Trump kupanga kukutana na Putin ana kwa ana na kuna tetesi anataka amwachie ardhi za Ukraine ambazo Putin amezinyakuwa kutoa Ukraine.

Trump akubali tu kuwa vita walivyovifadhili vimewashinda na Putin ni mwamba kuliko yeye.
 
Sisi yetu ni macho tu kushuhudia laana inayoendelea kuwapata madhalimu duniani.
Kwa sasa taifa la Marekani chini ya Trump linayumba sana na halijielewi linakoelekea.
Trump amewahi kudai pesa taslim za kile kilichotajwa kuwa ni misaada kwa Ukraine.Aliwahi kufokea mbele ya Kamera na Zelensky halafu akamkaribisha tena ikulu akacheka nae na kumuahidi vitu hewa.

Kiongozi huyo wa taifa kubwa amewahi kuzuia silaha nyeti kuipa Ukraine na baadae ikazitoa bila kuleta mabadiliko yoyote kwa kumegwa kwa ardhi ya Ukraine ambapo Urusi imekuwa ikizidungua moja baada ya nyengine.

Karibuni hivi raisi Trump amekuwa akionesha mahoka ya hali ya juu pale anapotoa makeke kwa Putin wa Urusi baadae kuomba tena urafiki naye.Kichekesho zaidi ni pale alipotoa agizo la mwezi mmoja na nusu kwa Putin afanye makubaliano na Zelensky kumaliza vita.Putin wala hakufanya hivyo.

Siku chache baadae Trump akapeleka nyambizi mbili za nyuklia karibu na Urusi na Putin akampuuza kabisa..Baada ya hapo Trump akapunguza mwezi mmoja na nusu mpaka siku 12.Nazo zimepita bila Putin kutikishika.

Kichekesho kikubwa ni sasa raisi Trump kupanga kukutana na Putin ana kwa ana na kuna tetesi anataka amwachie ardhi za Ukraine ambazo Putin amezinyakuwa kutoa Ukraine.

Trump akubali tu kuwa vita walivyovifadhili vimewashinda na Putin ni mwamba kuliko yeye.
Yaani jamaa huyu atabiriki hata
kidogo na kwa kuwa sijui jana au juzi alipigiwa simu na Viongozi wa EU na Uingereza ambao ni wanafiki wakubwa wenye nia ya kuweka Monkey SPANA kwenye mazungumzo kati ya Trump na Putin, huwezi kujua walimwambia nini Trump cha kubadirisha mawazo ya Trump kumuhusu Putin na Taifa la Urusi, ukweli ni kwamba genge hili alitaki mkutano huo ufanikiwe, kwa maneno mengine hawataki vita hii isitishwe.

Binafsi naona kuondoa mzizi wa fitina ni afadhali Zelensky aondolewe madarakani kwa kitumia mbinu zozote zile bila ya kufanya hivyo nawahakikisheni hakuna litakalo fanikiwa huko Ukraine - hata Trump na Putin wakifikia muhafaka bado Viongozi wa EU na Uingereza wataendeleza
mambo ya Ugaidi mipakani mwa Urusi au ndani ya Urusi yenyewe kwa kuwatumia makomando wa SAS wa Uingereza labda na Waufaransa na
Ukraine yenyewe, bila ya kuwepo vita kamili baina ya Urusi na Ukraine na kuiteka Ukraine nzima nzima hakuna litakalo badirika.

Narudia kusema Urusi iiteke Ukraine yote na kuifanya jimbo lake kiutawala, bila ya kufanya mbinu hizo ENEO hilo hapatakuwepo amani hata kidogo.
 
Vita ikisuluhishwa iishe wanaopata faida ni watu wa kawaida wanaouawa kila siku,

Trump huko kwake hana shida ya vita ni wananchi wa Russia na Ukraine ndio wanapata shida,

Tatizo na yeye Zelensky ameshaona vita ikiisha kutakuwa na uchaguzi anaoweza kutolewa, ndio maana hataki iishe,
 
Kwa uwezo wa kawaida kabisa wa kifikra, utulivu na ushawidhi bwana Trump yupo nyuma sana km 500 nyuma ya bwana Putin.
Putin kwanza hababaiki kujibu maswali ya kiuchonganishi!
Putin hajai upepo wa hasira kwa haraka!
Putin haropoki ovyoovyo.
Hebu msiojua jikumbukishen kilichotokea mwaka 2018 walipokutana watu hawa
 
Hilijambo trump uchaguzi ujao Chali ,democratic watashinda ili wamalizie vita walkpokuwa wameishia
 
Kwa uwezo wa kawaida kabisa wa kifikra, utulivu na ushawidhi bwana Trump yupo nyuma sana km 500 nyuma ya bwana Putin.
Putin kwanza hababaiki kujibu maswali ya kiuchonganishi!
Putin hajai upepo wa hasira kwa haraka!
Putin haropoki ovyoovyo.
Hebu msiojua jikumbukishen kilichotokea mwaka 2018 walipokutana watu hawa
Wakumbushe wasiojua
 
Yaani jamaa huyu atabiriki hata
kidogo na kwa kuwa sijui jana au juzi alipigiwa simu na Viongozi wa EU na Uingereza ambao ni wanafiki wakubwa wenye nia ya

Narudia kusema Urusi iiteke Ukraine yote na kuifanya jimbo lake kiutawala, bila ya kufanya mbinu hizo ENEO hilo hapatakuwepo amani hata kidogo.
Kwa hiyo unaunga mkono nchi moja kuiteka nchi ingine huru na kuimiliki kama sehemu ya nchi yake?
 
Kwa hiyo unaunga mkono nchi moja kuiteka nchi ingine huru na kuimiliki kama sehemu ya nchi yake?
Mnataka Putin pamoja na Viongozi wenye busara kama Trump wajirudie mara ngapi kuzungumza kwamba wa address kwanza tatizo la eneo hilo linasababoshwa na nini.

Trump na wasaidizi wake ambao unawatuma mara kwa mara kwenda kuchunguza kiundani mgogoro wa eneo hilo unasabishwa na kitu gani hasa? baada ya kufanya uchunguzi wanakuja na mapendekezo yao na kumpatia Trump ili ayapitie na kujiridhisha, ndio maana unamsikia Trump anazingumzia masuala ya give and take, yaani Ukraine ikubali kupoteza baadhi ya maeneo yao na Urusi ikubali kuirudishia Ukraine baadhi ya maeneo Urusi iliyo yateka vitani, it is that simple but fair, lakini Zelensky akileta ubishi bishi husio na maana basi akae akijua kwamba Urusi ikihamua ina uwezo mkubwa wa kuiteka na kuikalia Ukraine nzima na wala Trump hataingilia kati kumsaidia Zelensky kutokana na ubishi bishi na kiburi cha Zelensky kisicho kuwa na mantiki hata kidogo!!
 
Your brain is dull
Its Better If My Brain Is Dull But A little Bit Functioning,than Your Paralyzed Body Coordination System
No Body Electrical Conduction,your Synapses Lack (NA K) Ions Pumps
So your brain doesn't Charge at all.
YOUR A WALKING DEAD,IDIOT.
 
Yaani jamaa huyu atabiriki hata
kidogo na kwa kuwa sijui jana au juzi alipigiwa simu na Viongozi wa EU na Uingereza ambao ni wanafiki wakubwa wenye nia ya kuweka Monkey SPANA kwenye mazungumzo kati ya Trump na Putin, huwezi kujua walimwambia nini Trump cha kubadirisha mawazo ya Trump kumuhusu Putin na Taifa la Urusi, ukweli ni kwamba genge hili alitaki mkutano huo ufanikiwe, kwa maneno mengine hawataki vita hii isitishwe.

Binafsi naona kuondoa mzizi wa fitina ni afadhali Zelensky aondolewe madarakani kwa kitumia mbinu zozote zile bila ya kufanya hivyo nawahakikisheni hakuna litakalo fanikiwa huko Ukraine - hata Trump na Putin wakifikia muhafaka bado Viongozi wa EU na Uingereza wataendeleza
mambo ya Ugaidi mipakani mwa Urusi au ndani ya Urusi yenyewe kwa kuwatumia makomando wa SAS wa Uingereza labda na Waufaransa na
Ukraine yenyewe, bila ya kuwepo vita kamili baina ya Urusi na Ukraine na kuiteka Ukraine nzima nzima hakuna litakalo badirika.

Narudia kusema Urusi iiteke Ukraine yote na kuifanya jimbo lake kiutawala, bila ya kufanya mbinu hizo ENEO hilo hapatakuwepo amani hata kidogo.
Wewe unaota ndoto ukisukumwa zaidi na imani za kidini kuliko uhalisia. Wewe hujui kwamba nia ya kwanza kabisa ya dikteta Putin ilikuwa ni kuinyakua Ukraine yote ili apandikize kibaraka kama alivyofanya Belarus lakini uwezo ukawa mdogo ndipo akaenda kubana huko mashariki mwa Ukraine.
 
Back
Top Bottom